Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Inakuwa deactivated na maji. Tena yakiwa katika chombo chenye high exposure kama beseni au ndoo ni vyema zaidi. Nitaleta chemistry yake baadae
Itakuwa njema...
 
Hakikisha unakuwa na chombo chenye maji chumbani/vyumbani mfano maji kwenye ndoo.ikipulizwa hiyo dawa inakwenda kwenye maji.maji yakikosekana inakimbilia sehemu za unyevunyevu kama puani.utakuwa umeibiwa

Mkuu hivi kweli chloroform ina affinity yoyote na maji?

Remember Chloroform and water are immescible.
Kweli mkuu. Watu wapo tayari kuyumia gharama yoyote kuweka alarm kwenye gari lakini uhai wake haujali kabisa. Maana mwizi kuingia ngani ukiwa fofo nisawa na kumkabidhi uhai wako maana anaweza kuganya chochote na akatokomea bila hata kuacha alama. Tubadilikeni jamani, zipo alarm za bei chee kabisa. Ukigusa tuu ni kama king'ora cha ambulance au gari za police. Hadi majirani wataamka

Ni kweli mkuu mimi ni mtaalamu wa masuala ya Electronics na IT, ambacho uwa kinanishangaza ni watu kujali sana kuibiwa magari yao kuliko kujali usalama wao na familia zao majumbani na alarm zina cost a peanut/gharama ndogo sana.

Lakini mambo mengine ni kutumia common sense tu, niliopo kuwa mtoto mdogo nilikuwa namuona Baba yangu mzazi akipark gari sehemu ambayo usalama wake ni mdogo anafungua bonnet anaondoa rotor kwenye distributor, hivyo mwizi akija na funguo bandia au kukata nyaya na kuunga starter atafanya kazi lakini gari alitawaka hata akiwasha mwaka mzima mpaka aje kugunduwa kwamba tatizo ni rotor ya distributor haipo si rahisi - hiyo ni effective kuliko alarm zote duniani - kila niwashapo gari asubuhi ukumbuka ujanja wa mzee wangu. Hata magari ya siku hizi yanayo tumia electronic distributor kuna njia effective kuliko alarm ambazo zinaweza kuwa disabled kwa kutumia remote control za TV if you know how to go about it, nilikuwa naona vijana wa vilivyo kuwa wanawaiba magari ya matajiri wa kizungu kiulaini kabisa kwa kutumia ujanja huo - magari yenyewe yalikuwa yamesheheni alarm systems za kufa mtu lakini wapi - vijana wakishaona gari ni Ferarri, Aston Martin, Lamboggin, Posche au Maserati ukipark gari kuhasara hasara wanaondoka nayo for a joy ride siyo kwamba wanakwenda kuwauzia watu - nagari ya gharama si rahisi kuuzika utakamatwa.
 
Nilingiaga nyumba ya jamaa mmoja nkakuta kaweka beseni la maji dirishani!
 
Mi huwa nasafiri mara kwa mara, ivo nikiwa nimefunga nyumba wao wakaja iba ndo nataka washawishike kula biscuit.
Usiweke hivo funga mbwa weka na alarm unajua had mwizi aingie kwako lazima anakuwa amepewa mchongo na insider anayejua vzuri mazingira nao huwa hawakurupuki. Vingine kumwomba Mungu tu kuna siku kaka yangu aliponea chupuchupu kuibiwa na aliweka mlinzi ila waliingia ndani Mpaka sebuleni kilichowaokoa ilikua mtoto analia wakaamka na wezi wakakimbia na ameanza kufuga mbwa wengi wa wezi wa vitu vya ndani ni vibaka
 
Naomba kujua ni dawa gani au sumu gani naweza weka kwenye biscut au chakula ambacho mwizi akila kesha yake afe, iwapo ataniibia kwa stail hiyo.
samasion sina uhakika na spelling lakini inatamkwa hivyo
 
Dudu...!, hatar sana aseee. Kama vp nazo zipigwe marufuku kaa zile zingine
 
Kuna mwanajeshi mmoja yeye alikuwa akilala pikipiki yake anaitoa upepo alafu anaimwaga wese lote, sasa siku nahiyo wanyama wakatinga ndani, wakampulizia dawa kama kawaida yao, Walipofika kwenye Honda wakakuta haina upepo, jamaa wakatafuta pump, wakajaza, wakaenda kutafuta mafuta wakaweka, wakaiwasha wakala kona, jamaa asubuhi anaamka anakuta alama za matairi tu, ndio baadhi ya majirani wakasema usiku tulisikia pikipiki ikiwashwa ndani mwako....
Hii ya kutolea mafuta pikipiki/gari usiku alikuwa ananikumbusha sana mzee ila sikujua maana yake hadi siku majambazi walipotutembelea usiku wakata nyaya ili wawashe kitu waondoke ikagoma wese hamna na ndo ikawa salimika ya huo mchuma ilikuwa 1997
 
Lazima kuna kitu chaziada waliwafanyia na hawakupenda kulisema hilo hadharani maana ni aibu. Kama waliweza hadi kuwatenganisha hadi vyumba, inawezekana walifanya mengi
Of course hata mie na hata watu wengine mitaa ile huamini kuwa wezi wale wanatumia mitishamba kwani wakimtembelea mtu mara nyingi hugonga msosi, kuwahamisha watu toka kitandani na kuwapeleka sehem nyingine humo ndani na kisha kutoka na wanachotaka hususani pesa na electronic devices
 
Hii ya kutolea mafuta pikipiki/gari usiku alikuwa ananikumbusha sana mzee ila sikujua maana yake hadi siku majambazi walipotutembelea usiku wakata nyaya ili wawashe kitu waondoke ikagoma wese hamna na ndo ikawa salimika ya huo mchuma ilikuwa 1997
Style nzuri sana hii, ila siku nyengine watakuja na mchuzi juu.
 
Mleta mada sina imani nawe hata kidogo.Kama huna kazi,kalime acha hizo.
Hakuna mwizi wa majumbani aliye na account jf, sure nakwambia. Jf members ni watu ambao wamesoma kwanza mwizi hawezi kukaa na smartphone wala pc. Then mimi ni mtu mwenyekazi yangu nzuri tu! alafu naheshimika katika jamii ninayoishi, ukitaka kunijua mimi. Mimi ni wale tunaokaa viwanja vya serikali , sina shida ya kimaisha ugali ausumbui.
 
Huu uzi pengine mtoa mada ana lengo zuri ila ni vema ukaachwa cz huenda badala ya kujenga ndio tukazidi kubomoa!! Ndani ya michango ya wadau humu inatoa elimu ya wezi kujiboresha zaidi.
Absolute true.
 
Back
Top Bottom