Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Nilikuwa nawaza kwa sauti hii mbinu ya maji...
Lakini nikawa najiuliza kuwa litaulizwa swali uhusiano uliopo baina ya hiyo dawa na maji, kwa nini maji yakiwepo haiwezi kufanya kazi!!
Inakuwa deactivated na maji. Tena yakiwa katika chombo chenye high exposure kama beseni au ndoo ni vyema zaidi. Nitaleta chemistry yake baadae
 
Nakumbuka jirani yetu walishamliza kwa style hi yani walikomba mpaka chaga za vitanda wakamuandikia ukutani "LALA UNONO" yeye na mama watoto wake na watoto pia walishtuka saa 4 asubuhi wamelazwa sakafuni wakiwa na nguo walizovaa tu zingine wameondoka nazo,Jirani alichanganyikiwa akawa kama chizi vile mana wale wezi walikuja na Gari kubeba
Duhh, ndio maana akikamatwa mwizi wengine wanapagawa na jambo au adhabu ya haraka inayowajia kichwani ni kumuua mwizi!
 
Dah tumewahi ibiwa Mara mbili na hao watu wa dawa hadi leo sijui hua wanafanyaje kabla
 
Bwana MUNGU asipoilinda nyumba, wailindao wakesha bure Zaburin127. Dawa yangu ni Zaburn121, nitayainua macho yangu niitazame milima, msaada wangu utatoka wapi?Msaada wangu u katika BWANA aliyezifanya mbingu na nchi.
Sijakuelewa
 
Kwa nini amuweki vifaa vya electronic (alarm) vya kuwalinda, vipo mpaka vya kunusa madawa kama hayo ya cloroform na moshi.
Kweli mkuu. Watu wapo tayari kuyumia gharama yoyote kuweka alarm kwenye gari lakini uhai wake haujali kabisa. Maana mwizi kuingia ngani ukiwa fofo nisawa na kumkabidhi uhai wako maana anaweza kuganya chochote na akatokomea bila hata kuacha alama. Tubadilikeni jamani, zipo alarm za bei chee kabisa. Ukigusa tuu ni kama king'ora cha ambulance au gari za police. Hadi majirani wataamka
 
Daàaaah, umenikumbusha jirani yangu alinunua TV ya m1.25 na subwoofer la nguvu katumia wiki moja wezi wakaja wakawapulizia wakalala usingizi hadi tunawaamsha saa tano asubuhi baada ya kuona kimya sana hiyo nyumba hali tumegana nao usiku wa kulala na hawakuwa na safari yoyote.
Kuwakuta ndani wakaamka kila mmoja akitokea chumba tofauti wezi walibeba na kuwatenganisha mke na mme na kupeleka vyumba tofauti. Wezi ao hao walikula msosi kwanza ndo wakabeba mzigo na hela kidogo iliykuwa around.
Wezi wa namna hii washenzi sana ila dawa yao ni ndogo tu wanapuliza lakini wanakukuta uko macho unakimbizana nao.
Lazima kuna kitu chaziada waliwafanyia na hawakupenda kulisema hilo hadharani maana ni aibu. Kama waliweza hadi kuwatenganisha hadi vyumba, inawezekana walifanya mengi
 
Kuna jamaa walipigwa vitu vyote ndani waliokuwa wamelala wakahamishwa kutoka kitandani wakashushwa chini magodoro yote waliondoka nayo! kwenye friji kulikuwa na vinywaji walivinywa vyote wakachukua mzingo wakasepa
 
Ili kuzuia hyo dawa pindi mnalala achen maji yakiwa waz kwenye ndoo au bakuli.. yaachen aehem mnayolala.. dawa hapo haiwez kufanya kaz.
 
Back
Top Bottom