Mkuu, sijui sasa nikuite nani wewe, Samia ni rais pekee ambaye anafanya jambo ambalo halijawahi kufanywa na mtu mwingine yeyote kwa nchi yetu. Kama wewe, kwa sababu zako mwenyewe hulioni hili, usipende kufanya na wengine wasilione uhalisia wake ulivyo.Samia anayofanya ni muendelezo wa yale yale aliyofanya hayati JPM na watangulizi wengine wanne.
Tatizo ni siasa zinazojificha nyuma ya maamuzi yake haya ya sasa, pia ni nguvu kubwa ya mataifa makubwa inayotumika kupinga suala hili la bandari.
Mashambulizi kutoka kila upande yanawezeshwa na pesa za hao wanaoona Tanzania inakwenda kupaa kiuchumi, hivyo hayashangazi hata kidogo.
Upotoshaji wa suala zima hili la DPW ni mkakati wenye kueleweka vilivyo. Wanasheria wameshatumia nguvu kubwa sana katika kuelezea mkataba huu kifungu kwa kifungu lakini upingaji wanaokutana nao unakuwa ni mkubwa kwani nguvu iliyo nyuma yake ni kubwa.
Ni vita ya kiuchumi kama alivyowahi kusema hayati JPM lakini Tanzania itaibuka mshindi.
Nyaraka si hiyo hapo mnayopenda kuiita "makubaliano"?
Sasa kama wewe unasoma na kuona hakuna ubaya wowote na nyaraka hiyo, wacha nasi wengine tutumie akili zetu alizotujaalia Mwenyezi Mungu kuisoma nyaraka na kuielewa ilivyo andikwa.
Sisi tunasoma na kuelewa maandishi hayo kama yalivyowasilishwa na kuona ubaya uliomo ndani yake.
Kuwa Rais wa nchi hakumfanyi huyu rais kutufanya tusiwe na akili za kuelewa anayonuia kuyafanya juu ya nchi yetu. Huyu rais hakupewa madaraka ya kutunyamazisha, au kuziba akili zetu; kama asivyokuwa na mamlaka ya kuzuia asiondolewe madarakani kama anavuruga nchiyetu. Uwezo huo hana.