Ni hatari sana kwa nchi kutegemea ushauri wa Legal Officer (Hamza Johari), na kuiingiza nchi kwenye mkataba

Ni hatari sana kwa nchi kutegemea ushauri wa Legal Officer (Hamza Johari), na kuiingiza nchi kwenye mkataba

Utangulizi:
Katika taaluma ya sheria kote dunia, na kwa kipekee hapa nchini Tanzania, ili mtu akidhi vigezo vya kuwa mshauri, au kuwakilisha watu mahakamani, au kushauri mambo msingi ya kisheria , au kuhakiki nyaraka mbalimbali ni lazima awe na taalum hiyo katika ngazi au nafasi ya uwakili.

Hivyo kwa sababu ni taaluma, ina taratibu zake kuweka kutambulikwa na jumuia wa wataaluma hao katika nchi, kwa mathalani wale waliomaliza shahada za sheria kabla ya 2007 walifanya mitihani iliyotambulika kama bar exams , na wale waliomaliza baada ya 2007 shahada zao, ilianzishwa shule ya sheria kwa vitendo (law school of Tanzania.)

Katika mifumo hiyo yote wanaofaulu wanaomba kupokelewa, na Jaji Mkuu akiwakubalia wanaapishwa na kufanywa kuwa jumuia ya mawakili, wakiwa na majukumu mbalimbali, kama mawakili, mafisa viapo, na waidhinisha nyaraka mbalimbali katika jamii; na mawakili wanaweza kuwa wakujitegemea au mawakili wa serikali.

Kama hujapitia hatua hizo hata ungekuwa una LLD (PhD), LLM. LLB, unaitwa legal officer, na chochote unachotaka kukifanya lazima uwe chini ya wakili (either private or public), kwa sababu hautambuliki kama member in professional fratenity na huna comitment za obligation ya taaluma hiyo. na hivyo ushauri wako sio ushari

Utata:
Ukifuatilia sintofahamu ya Bandari, chimbuko lake kubwa ni mkataba na wala si uwezo wa DP world kama inavyoelezwa na waunga hoja wa waarabu hao, na kimsingi mkataba ni kazi ya sheria moja kwa moja, na yeyote anayetaka kuzungumzia mkataba lazima arejee sheria, au awe na background ya sheria, aidha za mikataba mbalimbali, ikiwepo za ndani na za nje, au uwezo wa kisheria kiujumla.

Kumekuwa na mwanasheria ambaye amejinasibu kuwa alishiriki katika mchakato na kushauri, swali langu Je, "mwanasheria" huyo ni wakili? (private or public) (is he a member of professional fratenity in Tanzania? Jibu ni hapana Hamza Johari si wakili(public or private) inawezekana ni mwanasheria kwa maana labda ana LLD, LLM, LLB, lakini si wakili, na si lawyer by professional, labda ni mwanasheria kwa kumaliza degree za sheria. lakini haonekani katika kanzi data za mahakama (data base) za judiciary.

Kulijua hilo ingia kwenye (tovuti ya mahakama) www.ewakili.judiciary.go.tz. kuna sehemu ya kumjua wakili wako, (know your advocate) ingiza majina utagundua si wakili.

Wale mnaolaumu wanasheria, tujiulize kwanza, Je aliyetoa ushauri wa kisheria ni mwanasheria kwa mujibu wa taaluma yetu ya kisheria?

Na kama si hivyo, aliwezaje kufanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo?Tume
Tunakwenda wapi?
 
Shida ni moja tu, taaluma zina matter only zinapo support agenda ya chama kikuu. Zikianza kupinga zinakuwa ignored, black painted, hata kudharaulika.
Bad news ni kwamba chama husika kinatumia class 7 to do that dirty job
Musukuma.
Lusinde.
Zungu
 
.Wale mnaolaumu wanasheria, tujiulize kwanza, Je aliyetoa ushauri wa kisheria ni mwanasheria kwa mujibu wa taaluma yetu ya kisheria?

Na kama si hivyo, aliwezaje kufanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo?
Very valid arguments, ila kwagu mimi mbona hili ni dogo tuu!.

Katiba ndio sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni sheria batili.

Tanzania tuna wanasheria lukuki, manguli wabobezi na wabobevu wa sheria lakini serikali yetu imetunga muswada wa sheria batili, ukaupeleka Bungeni, kutungwa kuwa sheria.

Bunge letu lililosheheni wanasheria manguli, wabobezi na wabobevu, wakaijenga sheria batili hiyo!.

Mahakama Kuu ikaitamka sheria hiyo ni batili, serikali ikakata rufaa kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu na kupeleka Bungeni muswada wa marekebisho ya katiba kwa hati ya dharura, na kuuchomekea ubatili huo ndani ya katiba yetu!.

Hapa unashangaa nini?. Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?

Nimeuliza Watanzania ni Watu wa ajabu. Wanapigiaje kelele jambo dogo la Bandari, lakini Mambo Muhimu ya Msingi kama Katiba na Uhuru wao wapo Kimya?

Hata TLS walipotoa kauli yao, nikauliza Watanzania ni Watu wa ajabu. Wanapigiaje kelele jambo dogo la Bandari, lakini Mambo Muhimu ya Msingi kama Katiba na Uhuru wao wapo Kimya?
P
 
Tusimlaumu Johari.
Tumlaumu mlinzi mkuu wa rasilomali zetu.
Ikulu imejaa wataalam wa sheria hii imekusudiwa watu wajimilikishe, wamepewa majumba huko nje na wamepewa share kwa DPW ndio maana wameweka gundi masikioni
 
Mpwayungu Village taaluma yako ya ualimu inahitajika kwenye suala hili la Bandari. Tuliza Fujo, weka mazingira ya kama vile unasimamia kituo cha kupiga kura
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Hata mwenye akili ya kutosha kuvuka barabara tu hawezi kukosa kuelewa mhitasari huu uliouweka hapa vizuri kabisa.
 
Utangulizi:
Katika taaluma ya sheria kote dunia, na kwa kipekee hapa nchini Tanzania, ili mtu akidhi vigezo vya kuwa mshauri, au kuwakilisha watu mahakamani, au kushauri mambo msingi ya kisheria , au kuhakiki nyaraka mbalimbali ni lazima awe na taalum hiyo katika ngazi au nafasi ya uwakili.

Hivyo kwa sababu ni taaluma, ina taratibu zake kuweka kutambulikwa na jumuia wa wataaluma hao katika nchi, kwa mathalani wale waliomaliza shahada za sheria kabla ya 2007 walifanya mitihani iliyotambulika kama bar exams , na wale waliomaliza baada ya 2007 shahada zao, ilianzishwa shule ya sheria kwa vitendo (law school of Tanzania.)

Katika mifumo hiyo yote wanaofaulu wanaomba kupokelewa, na Jaji Mkuu akiwakubalia wanaapishwa na kufanywa kuwa jumuia ya mawakili, wakiwa na majukumu mbalimbali, kama mawakili, mafisa viapo, na waidhinisha nyaraka mbalimbali katika jamii; na mawakili wanaweza kuwa wakujitegemea au mawakili wa serikali.

Kama hujapitia hatua hizo hata ungekuwa una LLD (PhD), LLM. LLB, unaitwa legal officer, na chochote unachotaka kukifanya lazima uwe chini ya wakili (either private or public), kwa sababu hautambuliki kama member in professional fratenity na huna comitment za obligation ya taaluma hiyo. na hivyo ushauri wako sio ushari

Utata:
Ukifuatilia sintofahamu ya Bandari, chimbuko lake kubwa ni mkataba na wala si uwezo wa DP world kama inavyoelezwa na waunga hoja wa waarabu hao, na kimsingi mkataba ni kazi ya sheria moja kwa moja, na yeyote anayetaka kuzungumzia mkataba lazima arejee sheria, au awe na background ya sheria, aidha za mikataba mbalimbali, ikiwepo za ndani na za nje, au uwezo wa kisheria kiujumla.

Kumekuwa na mwanasheria ambaye amejinasibu kuwa alishiriki katika mchakato na kushauri, swali langu Je, "mwanasheria" huyo ni wakili? (private or public) (is he a member of professional fratenity in Tanzania? Jibu ni hapana Hamza Johari si wakili(public or private) inawezekana ni mwanasheria kwa maana labda ana LLD, LLM, LLB, lakini si wakili, na si lawyer by professional, labda ni mwanasheria kwa kumaliza degree za sheria. lakini haonekani katika kanzi data za mahakama (data base) za judiciary.

Kulijua hilo ingia kwenye (tovuti ya mahakama) www.ewakili.judiciary.go.tz. kuna sehemu ya kumjua wakili wako, (know your advocate) ingiza majina utagundua si wakili.

Wale mnaolaumu wanasheria, tujiulize kwanza, Je aliyetoa ushauri wa kisheria ni mwanasheria kwa mujibu wa taaluma yetu ya kisheria?

Na kama si hivyo, aliwezaje kufanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo?
Nimekwama hapo-si lawyer by professional.....kosa la usemi wa lugha...paswa iwe si lawyer by profession....lakini pia hoja ingeeleweka kwenye representation mahakamani ndipo ushauri huu uzingatiwe...mambo ya ushauri na tafsiri za Sheria yeyote mwenye llb ambaye hajawahi kupitia TLS anafanya...Sasa johari alihusikaje na Bandari
 
Tatizo la mada hii ni lile lile la watanzania la miaka yote. Kudharau taaluma za watu haswa wale wasiowajua vizuri.

Tunachukulia poa sana elimu za watu na huu ni ushahidi wa sisi wenyewe kuwa na elimu za kubabaisha hivyo tunadhani kila mtu na yeye ni mbabaishaji tu.
Weka hapa huo ushahidi wako, umewekewa link hapo juu huyo unayemtetea yumo?
 
TLS wanasemaje kuhusu uanachama wake na Chama Cha mawakili wa Tanganyika zungumzia suala hili au kwa kuwa amewekwa na Mamlaka za juu ya uteuzi.?
Ili kuepusha maswali na kuleta heshima ya taaluma husika,vigezo na masharti ya Tasnia yazingatiwe wakati wa kufanya uteuzi.
TAAA inachohitajika Mkurugenzi sio lazima awe mwanasheria mnatuchanganya. Hamza wa TAAA alihusika vipi mkataba wa ikulu na DP World
 
Profession ipi kwa mujibu wako wewe?. Alikuwa mwanasheria wa kampuni binafsi kabla hajachukuliwa mamlaka ya anga upande wa haki za wasafiri na baadae akaomba nafasi ya ukurugenzi akaipata enzi za JK.

Wakaweka kwenye makabati recommendations za JK na alipokuja JPM akamuona na kumchukua.

Profession yake anaitetea vyema ndio maana sekta ya anga kwa sasa imesimama kuliko wakati mwingine wowote huko nyuma. Huyo ni sehemu ya viongozi wa taasisi ya kidunia ya sekta ya anga ICAO akiwa ni kiongozi wa bara la afrika.

Unaongelea professionalism ipi labda?, huko kote afanye tu kazi bila ya kujua anafanya nini!

Unarudi kule kule kwenye kutazama haiba binafsi ya mtu badala ya kutazama substance nzima ya kile anachokifanya kwa maslahi ya Tanzania nzima. Tunaibiwa na wezi wanakuja kisomi kwa kutafuta watetezi wao humu jukwaani.

Mleta mada tuliza kichwa chako.
Mnaotumia maneno professional, profession njooni comment hii ipo sahihi Kwa matumizi sahihi
 
Huyu jamaa watu "walimpamba" kama WAKILI MSOMI, kumbe siyo. Hatari sana.
 
Tukubali kwenye mkataba Huu hatukuhitaji serikali pekee pia watu kutoka nje so tuwalaumu wote lkn hata tukilaumu hiyo IGA haisaniniwi upya let us cut the crap
What we can do ni kutangaxa mgogoro kwa mujibu wa mkataba tusuhishe na kwenda vizur jambo ambalo hatuongei na hatulioni ikizingatiwa hii ni saini ya pili dhidi ya DP
Usichanganye au kupotosha maksudi mazima.

'Ratfication' ya IGA kati ya mataifa mawili bado haijakamilishwa.

Bunge liondoe uchafu lililofanya na IGA itakuwa hakuna.
 
Hayati JPM alimkubali sana namna anavyofanya kazi, alikuwa ni mtu wake wa karibu kwa sababu JPM alikuwa mpenda haki na mzalendo wa kweli wa Tanzania.
Ungeyasema haya kuhusu Samia, ambaye alikuwa ni Makamu wa Rais, ningekushangaa; lakini naona umeepana kuangukia kwingine.

Sasa ninakuunganisha na huyo Hamza, pengine itakuwa ni wewe mwenyewe, au uko karibu sana na huyo mtu.
 
Nchi zinazotuzunguka kama Kenya, Uganda, Malawi na Msumbiji hazina haki ya kusimama na Tanzania kwa aina ya utajiri tuliojaliwa na Mungu. Lakini bado tunalo tatizo la weak manpower. Tuna uongozi mwingi dhaifu.
Kati ya yote uliyoandika; hili hapa ninakubaliana nawe kabisa. "Tuna uongozi mwingi dhaifu", tukianzia juu kabisa kwa Samia mwenyewe.

Hayo ya "majungu" na kutulinganisha na nchi jirani ni kelele tu zisizokuwa na maana yoyote.
 
Huwezi kuwa mkurugenzi mkuu wa TCAA yaani anga zima la Tanzania liwe chini yako halafu usiwe professional kwenye kazi yako!. Mikataba mingi ameingia kwa niaba ya serikali huu wa bandari ni maarufu kwa sababu ya unyeti wake.
Duh!
Sikujua kuwa ulikuwa thismuch shallow!
God have mercy upon us.

This is it! Kumbe huna kitu kabisa.
 
Back
Top Bottom