- Part ya 1 ya mada yako, kosa la Dr. Slaa.
Kosa la Dr. Slaa alikuwa msaliti, alinunuliwa na CCM akaenda kufichwa hotelini, kisha akapewa ulinzi na TISS.
Alikuwa msaliti pia kwasababu, wakati wa kumpokea Lowassa alikuwepo, akajua yote yatakayotokea, lakini ghafla akabadilika na kuifuata njia ya CCM.
Nafahamu alinunuliwa na CCM ili apunguze nguvu ya Chadema kwa wakati ule, bahati nzuri licha ya kuhama kwake, bado Chadema ilishinda uchaguzi mkuu 2015 lakini wakaibiwa kura na wakina Nape na Makamba.
- Part 2 kumsimamisha Lowassa.
Alikuwa mgombea mwenye ushawishi kwa wakati ule, hili linathibitishwa na idadi ya kura za urais ilizopata Chadema zaidi ya milioni sita, licha ya kuibiwa kura nyingine na wakina Makamba.
Suala la ruzuku nalo ni sahihi, kwasababu chama kinapopata kura nyingi kwenye uchaguzi, matokeo yake huwa ni kupata ruzuku nyingi pia inayokiwezesha kuendesha chama.
Lowassa aliletwa kwa maslahi ya wananchi, na wananchi hao walikuja kuthibitisha kumuunga mkono kupitia idadi ya kura alizopata kama mgombea urais, alipata kura nyingi ambazo hazijawahi kupatikana kwa mgombea yeyote wa upinzani mpaka sasa.
Suala la kuhalalisha tuhuma za ufisadi zilizowahi kutolewa dhidi ya Lowassa, hapa ndipo kuna "collective responsibility", kwasababu rule inasema; he who alledges must prove.
Bahati mbaya wale waliomtuhumu hawakuwahi kuja na ushahidi, na bahati mbaya zaidi yule aliyemtuhumu kwa kulitaja jina lake kwenye list of shame pale Temeke, Mwembeyanga, akawa wa kwanza kukimbilia kwa wale waliomlea Lowassa.
Above all, usidanganyike na kile kinachoitwa "nguvu ya Dr. Slaa", huo ulikuwa ni msemo tu, kumbuka Dr. Slaa huyo mwenye nguvu aliwahi kushindwa uchaguzi dhidi ya Kikwete aliyeonekana dhaifu 2010, sasa utamuitaje mwenye nguvu mtu wa aina hiyo?!
Sent from my SM-G900H using
JamiiForums mobile app