Ni ipi hasa sababu ya Freeman Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa CHADEMA kwa kipindi kirefu hivi?

Ni ipi hasa sababu ya Freeman Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa CHADEMA kwa kipindi kirefu hivi?

Je CHADEMA watu wenye hakuna uwezo wa kuwa wenyeviti ? Mbona kina Mtei na Bob Makani walimuamini inamaana baada ya yeye hakuna mwingine mwenye uwezo ?

Ni kipi kinafanyika kwenye chama chetu CHADEMA kinachoonesha uwepo wa Demokrasia ? Ni miaka zaidi ya 20 mwenyekiti yule yule .

Binafsi kama mwanachama huwa najiuza hili swali nikiuliza najibiwa akiondoka chama kinakufa ,je kweli ?

Je hakuna namna ikawekwa misingi Imara kama ilivyo kwa Republican na Democratic US ?

Au kuna elements za dictatorship kama

Kuamini hakuna mtu mwenye uwezo zaidi yako

Tamaa ya kuendelea kuwepo madarakani ?

Kuna muda naona kama anafanya vitu ambavyo vinaipa faida sana CCM kuliko CDM naona akipumzika akawa Mlezi wa chama kinaweza songa mbele zaidi .
Hata Nyerere ilibidi akae madarakani miaka 22, CDM inamwitaji Mbowe sasa kuliko wakati mwingine wowote!
 
CDM inamwitaji Mbowe sasa na miaka 10 ijayo!
Mfano Mungu kamchukua Mbowe ndio utakuwa mwisho wa chadema?Mbowe Sio kiongozi mwenye maono miaka zaidi ya 20 hauwezi kukosa vijana hata 10 wenye maono na uthubutu wa kuongoza chama, Mbowe hajifunze kwa watangulizi wake akina Bob Makani na Mtei waliongoza miaka 10/10 wakamwachia ingawa alikuwa kijana hasiye na uzoefu wowote wa uongozi.
 
Je CHADEMA watu wenye hakuna uwezo wa kuwa wenyeviti ? Mbona kina Mtei na Bob Makani walimuamini inamaana baada ya yeye hakuna mwingine mwenye uwezo ?

Ni kipi kinafanyika kwenye chama chetu CHADEMA kinachoonesha uwepo wa Demokrasia ? Ni miaka zaidi ya 20 mwenyekiti yule yule .

Binafsi kama mwanachama huwa najiuza hili swali nikiuliza najibiwa akiondoka chama kinakufa ,je kweli ?

Je hakuna namna ikawekwa misingi Imara kama ilivyo kwa Republican na Democratic US ?

Au kuna elements za dictatorship kama

Kuamini hakuna mtu mwenye uwezo zaidi yako

Tamaa ya kuendelea kuwepo madarakani ?

Kuna muda naona kama anafanya vitu ambavyo vinaipa faida sana CCM kuliko CDM naona akipumzika akawa Mlezi wa chama kinaweza songa mbele zaidi .
Politically speaking,
Mi nadhani Mbowe yuko mamlakani muda wote ni kwasababu ya:-

1. werevu wake makini sana wa kizalendo ukilinganisha na yeyote ndani chadema 🐒

2. weledi, subra na ustahimilivu chanya alonao, hakuna Mwingine mwenye hulka hiyo chadema 🐒

3.Ukomavu na uzoefu wake katika siasa za Tz. Huwezi mlinganisha na yeyote ndani ya Chadema na kwahiyo ndio maana yupo mamlakani muda wote huo 🐒

4.Moyo wake wa kujitolea bila kujibakiza kwajili ya Chadema, check wengine ni wabinafsi balaa 🐒

5. Uwezo wake mkubwa sana katika uongozi, kujenga hoja, kutetea hoja na kujieleza taratibu na kwa vituo, ukilinganisha na yeyote ndani ya Chadema. Wengine hubwabwaja hatari 🐒

6. Ujasiri na uungwana wa kiwango cha juu sana katika kuitetea chadema. Wengine waliitoroka chadema na wakatoroka na nchi pia 🐒

7. Si king'ang'anizi kwa yasiyowezekana ukilinganisha na vibaraka 🐒

8. Mbowe can sit on table with opponent and negotiate on lose lose or win win situations otherz within the party can never 🐒

hata hivyo,
I can see Mbowe ready and willing kuachia ngazi but sio hivi karibuni.
He will never ever left the party under hands of intruders with puppetical elements.
That one, Mbowe can never ever allow 🐒
 
Cha ajabu CCM ndio siku zote wanalilia democrasia ndani ya CHADEMA utasikia mbowe sijui hivi mala mbowe vile

waga najiuliza hivi kweli CCM inaipenda sana CDM Kiasi hiki????
Wana lao jambo hao maccm. Wanatafuta fursa ya kuweka kibaraka wao kama walivyo fanikiwa kufanya kwa CUF, ACT, TLP, nk..
 
Wanasema akiachia hicho kiti chama kina kufa!

Ndio kusema siku Mbowe akifa na chama nacho kwa heri
 
Ungekuwa unamawazo mazuli ungepamba na hili kwanza

Selikali imetutangazia bei elekezi ya sukali kilo sh 3000 lkn wafanyabiashara hajajua wapi watanunua sukari kwa bei elwkezi ili waje kuuza kwa sh 3000 kwa maana selikali iwaambie mkanunue sukali mahali fulani,

Ukikutwa nayo sukali na unauza zaid ya sh 3000 unakamatwa bila kujali umenunua sh ngapi ,wale waliokukamata ukiwaambia nipelekeni inauzwa bei elekezi ili ninunue nije kuuza huku hawataki,



Mbowe akapewa chama kutoka kwa mkwe wake ili akiongoze kisiteteleke, sasa kitendo cha mbowe kutoka pele hatujui atakae ingia atakuwa na malengo gani na chama, hii inapelekea mbowe abaki kwa maana ametoka mbali na chama
 
Jibu ni rahisi tu. Tafuta vyama vingine vya upinzani ambavyo vimebadilisha wenyeviti wao kifala bila kuchukua tahadhari ya athari za ccm juu yao kama vipo hai. Hebu imagine km mwenyekiti wa chadema angekuwa lipumba, jaribu kuwaza km mwenyekiti wa chadema angekuwa zitto, jaribu kuwaza km mwenyekiti wa chadema angekuwa halima mdee, jibu unalipata
 
Mbowe ni muhuni tu anawachezea vichwa watanganyika.

Siku watanganyika wakigundua uhuni wa MBOWEEH watamcharanga kwa spoku.
 
Jibu ni rahisi tu. Tafuta vyama vingine vya upinzani ambavyo vimebadilisha wenyeviti wao kifala bila kuchukua tahadhari ya athari za ccm juu yao kama vipo hai. Hebu imagine km mwenyekiti wa chadema angekuwa lipumba, jaribu kuwaza km mwenyekiti wa chadema angekuwa zitto, jaribu kuwaza km mwenyekiti wa chadema angekuwa halima mdee, jibu unalipata
Ujinga mtupu!

Kumbe ni halali DIKTETA kukaa madarakani milele kwa kuwa tu ni kiongozi imara?

Chama bovu hili. CHADRAMA!
 
Kiukweli hili halileti picha nzuri kwa chama kinachojipambanua kwa demokrasia.

Kama chama tu anakaa madarakani miaka 20, nchi itakuwaje?
Hili linawapa sababu CCM ya kuwadhihaki kwa wananchi na ni ukweli ambao haupingiki.


Mbowe ni moja ya wanasiasa mahiri na historia itamkumbuka kwa hilo, lakini mtumbuizaji bora ni yule anayejua muda wa kuondoka jukwaani.
Madam na wewe unatumia “talking points” za CCM? CCM iliyohodhi madaraka kwa “goli ya mkono” tangu uhuru hadi leo ndio iwadhihaki CHADEMA kwa wananchi kwa suala la mwenyekiti wake tu?

Kwanza mazingira yatakayowezesha CHADEMA kupata madaraka ya uRais hayawezi kuwa haya ya leo ya “chama dola” yaliyokumbatiwa na CCM. Ikitokea it will be a completely different scenario. Kama unavyofahamu, leo CHADEMA iko hivyo kutokana na mzingira ya lawlessness na hujuma zinazofanywa dhidi ya vyama vya upinzani tangu 1995. Hazina ya taifa na taasisi za dola zinatumika bila hiyana kwa hiyo kazi chafu

Je, ni vyema Mbowe kupisha wengine? Hakuna ubishi; it better be so. Lakini si kwa msukumo wa propaganda uchwara za CCM. Na mchakato wa kumbadili unatakiwa kuwa makini na wa kimkakati kweli kweli. CCM wako tayari kuchota mabilioni ya Hazina kumuweka sawa mwenyekiti mpya afanye kazi ya kuiparaganyisha CDM ipoteze nguvu ya umma ambayo ndiyo tishio kuu kwa uhai wa CCM inayotegemea zaidi nguvu za dola na machawa. It’s not a simple matter.
 
Kiukweli hili halileti picha nzuri kwa chama kinachojipambanua kwa demokrasia.

Kama chama tu anakaa madarakani miaka 20, nchi itakuwaje?
Hili linawapa sababu CCM ya kuwadhihaki kwa wananchi na ni ukweli ambao haupingiki.

Mbowe ni moja ya wanasiasa mahiri na historia itamkumbuka kwa hilo, lakini mtumbuizaji bora ni yule anayejua muda wa kuondoka jukwaani.
Hiyo nchi ya kupewa chadema ni nchi gani kweli?
Hawa mkiwapa nchi wanabadili katiba ya nchi mara moja ili rais toka kwao awe madarakani kama mwenyekiti wao.
Uenyekiti wa chama wameugeuza kuwa ufalme!
 
Back
Top Bottom