Ni ipi siri ya mafanikio ya kudumu kwenye ndoa za Wazee wetu?

Ni ipi siri ya mafanikio ya kudumu kwenye ndoa za Wazee wetu?

Siri kuu ni kujifanya mpumbavu ndani ya ndoa, wanandoa wanatakiwa kujua muda sahihi wa kubadilishana kijiti cha upumbavu, tatizo kwa wanandoa wa siku hizi kila mtu anajifanya mwerevu, ndoa nyingi siku zinavunjika kwa sababu za kijingajinga sababu kila mtu ni mwerevu, ndoa nyingi ambazo zimedumu ujue wanandoa hao wamejua muda sahihi wa kubadilishana kijiti cha upumbavu.
 
binafsi naweza kusema kwa kiasi kikubwa utandawazi umebadili mtindo wetu wa maisha ambao ulikuwepo hapo awali. ndoa za kipindi hiki cha utandawazi zimekua na changamoto nyingi ukilinganisha na zamani kulingana na uwepo wa mambo kadhaa.

mitandao ya kijamii. kwamfano shemeji yako kaweka status whatsapp kuhusu hisia zake either akiwa mwenye huzuni, au furaha au akiwa kwenye tukio fulani ni rahisi kuanzisha mazungumzo juu ya status yake na kuongeza ukaribu mpaka kujikuta katika hali ya kutamaniana. zamani kumuona tu mtu au kufahamu hisia zake ilikua ngumu sababu hatukua na hizi simu za kisasa tulizonazo sasahivi.

Tamaa.hasa kwa wakinadada unakuta hali ya maisha nyumbani kwake ni ya kipato cha kawaida au cha chini ila akiwatizama marafiki zake wanamiliki vitu vya gharama hivyo inapelekea kujiona mpweke na kutamani vitu visivyoendana na kipato chake hivyo inakua rahisi kushawishika na watu wenye kipato cha juu na kuamua kuisaliti ndoa yake.

changamoto za kiafya. hapa ipo mifano hai kabisa. mpo kwenye ndoa wote mkiwa na afya nzuri ila ikatokea mmoja wapo akatetereka kiafya mwenza anakosa uvumilivu na kuamua kumsaliti mwenzake.

malezi. aina ya malezi pia kwa namna fulani inachangia ndoa nyingi kutodumu ukilinganisha na miaka ya nyuma. kwa hivi karibuni tumekua na changamoto za kima adili pamoja na malezi. watu hawazingatii tena miiko na maadili pindi unapokua kwenye ndoa ndo kama tulivyosikia baadhi ya semina za wanawake kwamba sio lazima kumuaga mume pindi unapotaka kutoka.

usawa wa kininsia. ukweli hili suala la usawa wa kinjinsia limekua ni changamoto kubwa sana katika ndoa zetu. unakuta mwanamke hatimizi mambo ya kifamilia kwasababu ya ubize wa kazi za kazini. hali ya kujiona mko sawa wote na kupelekea ubishani na hata kuwa tayari kutengana pindi mnaposhindwa kuelewana.

miaka ya nyuma sana aina fulani ya mtindo wa maisha ulisaidia sana kudumisha ndoa pamoja na maadili kwa wanandoa pamoja na jamii kwa ujumla. ila hatuwezi kupingana na utandawazi ila tusiache asili na tamaduni zetu kwani zilituongoza katika njia sahihi na bora.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Mpaka akili zitakapowarudi vijana na kukubali kwamba "mwanamke aliumbwa kwa ajili ya kuwazalia watoto na kukaa nyumbani wakiwatunza huku wao wakienda kutafuta mkate wa familia na siyo wasaidizi wao wa kuwatafutia hela ya ada au ujenzi" ndiyo watapata utulivu walioupata babu zao,leo kijana kichwani anawaza kutafuta mke wasaidiane maisha msaidiane maisha na mwanamke kwenye uchumi hii mliisikia wapi?watu mmekua mkiwaona mama zenu nyumbani kila siku wanawaogesha na kuwapikia huku baba zenu wakitoka kila siku na kurudi usiku leo mnataka ninyi na wake zenu mtoke wote alfajiri mrudi usiku eti ndiyo maisha yanavyotaka huku mwanaume unayejiita msomi ukiiacha damu yako ilelewe na mtu ambaye hata unasaba nae wa kabila huna kisa eti mimi na mke wangu tunawatafutia watoto wetu maisha baadae wasipate shida,ndiyo hao leo wanageuka mashoga nani ataendeleza uzao wako?

Kwamba kwa sababu mna visomo vichwani basi wazee wenu kuacha mama zenu nyumbani wawatunze wao walikuwa outdated nyie ndiyo mpo smart zaidi!na siyo ndoa tu,leo angalia hata watoto wengi waliozaliwa baada ya Beijing conference hawa wamekuwa changamoto kwenye malezi baada ya kuwa mama anataka akatafute hela yake baba nae aende akatafute so wamelelewa na ma-house maids ambao hata mtoto akifanya kosa kubwa kiasi gani la kimaadili hazingatii maana mtoto akiharibika siyo wake.

Tupo leo na kizazi cha vijana kukataa ndoa mabinti nao kuvua vua chupi hovyo,kama binti kipindi akiwa mtoto alishuhudia dada yake (house girl wao) akipigwa mpini sebuleni na muuza genge (maana hawa ndiyo wabaya kwa wafanyakazi wa ndani huko mitaani) leo ataona ajabu gani kuvua nguo hovyo afanye ngono?na huko kugongwa kuna mawili apate mimba awe singo mama au ukimwi,hii yote sababu wakati alipokuwa anahitaji msingi wa malezi ya mama yake huyu mama alikuwa ameenda kutafuta pesa.

NB;oweni std 7,form 4&6 hawa hawana mambo mengi ya sijui nataka nikafanyie kazi ujuzi wangu niliosomea muhimu mke ajue kusahihisha homework za watoto the rest fanyeni wenyewe.
 
Hakuna kama mtu unamuoa ukimpiga au mkiwa mnagombana anakwambia acha niende kwetu sijau hapo kuna uvumilivu?
Hii tabia husababishwa na wazazi na baadhi kaka zao wenye akili za kiwendawazimu.

Siku moja nilihudhuria send off ya binti mmoja,ktk process za kukamilisha taratibu za kukabidhiana mke akaitwa kaka mtu ile mbuzi ikasema inamwambia mshenga wa jamaa "sisi dada yetu tumewakabidhi akiwa hana hata kovu moja tunataka akiwa anakuja nyumbani kutusalimia awe hivi hivi,dada ukiona huko maisha magumu nyumbani kwako kupo rudi"

Mzee wao alipopewa nafasi alisema pale pale clearly kabisa kwamba "wewe (jina) umeamua kuanzisha maisha na (jina) hakuna aliyekulazimisha hivyo tukitoka hapa kile chumba chako kitapangishwa au kufanywa store pale usirudi ishi kwako na mumeo kama mama yako alivyokaa hajawahi kurudi kwao"

watu kama hawa leo hawapo au wapo lakini kwa makusudi wanaamua kwenda nje ya rules za maisha.
 
Hii tabia husababishwa na wazazi na baadhi kaka zao wenye akili za kiwendawazimu.

Siku moja nilihudhuria send off ya binti mmoja,ktk process za kukamilisha taratibu za kukabidhiana mke akaitwa kaka mtu ile mbuzi ikasema inamwambia mshenga wa jamaa "sisi dada yetu tumewakabidhi akiwa hana hata kovu moja tunataka akiwa anakuja nyumbani kutusalimia awe hivi hivi,dada ukiona huko maisha magumu nyumbani kwako kupo rudi"

Mzee wao alipopewa nafasi alisema pale pale clearly kabisa kwamba "wewe (jina) umeamua kuanzisha maisha na (jina) hakuna aliyekulazimisha hivyo tukitoka hapa kile chumba chako kitapangishwa au kufanywa store pale usirudi ishi kwako na mumeo kama mama yako alivyokaa hajawahi kurudi kwao"

watu kama hawa leo hawapo au wapo lakini kwa makusudi wanaamua kwenda nje ya rules za maisha.
Haya ndio unataka ndoa za leo zidumu
 
Zamani wanawake walikuwa submissive chochote atakachotaka mume au kusema mume kilikuwa kinatekelezwa vizuri.Sasa hapo mume atawezaje kumwacha mwanamke na huo utii na heshima ukawafanya wanaume wawapende wake zao waliowaoa na kudumu nao.
 
Promotion of women empowerment and rights (POWER)
 
Kuamini kuwa lazima anamchepuko ambao ni afya ya ndoa.
Mtoto akizaliwa kwenye malango yako ni wako period.
Wanawake walijishughulisha mno kwenye kazi za mikono na kulisha familia.
Ugomvi ulikuwa ukiamuliwa kwa staha.. umekosea unarudishwa nyumbani kwenu. Wazee watapelka ujumbe na namna ya kumaliza.
 
Mmoja wao kujifanya mjinga wakati unamsikiliza mpumpavu.
 
Mpaka akili zitakapowarudi vijana na kukubali kwamba "mwanamke aliumbwa kwa ajili ya kuwazalia watoto na kukaa nyumbani wakiwatunza huku wao wakienda kutafuta mkate wa familia na siyo wasaidizi wao wa kuwatafutia hela ya ada au ujenzi" ndiyo watapata utulivu walioupata babu zao,leo kijana kichwani anawaza kutafuta mke wasaidiane maisha msaidiane maisha na mwanamke kwenye uchumi hii mliisikia wapi?

Siyo ndoa tu,leo angalia hata watoto wengi waliozaliwa baada ya Beijing conference hawa wamekuwa changamoto kwenye malezi baada ya kuwa mama anataka akatafute hela yake baba nae aende akatafute so wamelelewa na ma-house maids ambao hata mtoto akifanya kosa kubwa kiasi gani la kimaadili hazingatii maana mtoto akiharibika siyo wake.

Tupo leo na kizazi cha vijana kukataa ndoa mabinti nao kuvua vua chupi hovyo,kama binti kipindi akiwa mtoto alishuhudia dada yake (house girl wao) akipigwa mpini sebuleni na muuza genge (maana hawa ndiyo wabaya kwa wafanyakazi wa ndani huko mitaani) leo ataona ajabu gani kuvua nguo hovyo afanye ngono?na huko kugongwa kuna mawili apate mimba awe singo mama au ukimwi,hii yote sababu wakati alipokuwa anahitaji msingi wa malezi ya mama yake huyu mama alikuwa ameenda kutafuta pesa.

NB;oweni std 7,form 4&6 muhimu mke ajue kusahihisha homework za watoto the rest fanyeni wenyewe.
Cc Zemanda [emoji846]
 
Mpaka akili zitakapowarudi vijana na kukubali kwamba "mwanamke aliumbwa kwa ajili ya kuwazalia watoto na kukaa nyumbani wakiwatunza huku wao wakienda kutafuta mkate wa familia na siyo wasaidizi wao wa kuwatafutia hela ya ada au ujenzi" ndiyo watapata utulivu walioupata babu zao,leo kijana kichwani anawaza kutafuta mke wasaidiane maisha msaidiane maisha na mwanamke kwenye uchumi hii mliisikia wapi?watu mmekua mkiwaona mama zenu nyumbani kila siku wanawaogesha na kuwapikia huku baba zenu wakitoka kila siku na kurudi usiku leo mnataka ninyi na wake zenu mtoke wote alfajiri mrudi usiku eti ndiyo maisha yanavyotaka huku mwanaume unayejiita msomi ukiiacha damu yako ilelewe na mtu ambaye hata unasaba nae wa kabila huna kisa eti mimi na mke wangu tunawatafutia watoto wetu maisha baadae wasipate shida,ndiyo hao leo wanageuka mashoga nani ataendeleza uzao wako?

Kwamba kwa sababu mna visomo vichwani basi wazee wenu kuacha mama zenu nyumbani wawatunze wao walikuwa outdated nyie ndiyo mpo smart zaidi!na siyo ndoa tu,leo angalia hata watoto wengi waliozaliwa baada ya Beijing conference hawa wamekuwa changamoto kwenye malezi baada ya kuwa mama anataka akatafute hela yake baba nae aende akatafute so wamelelewa na ma-house maids ambao hata mtoto akifanya kosa kubwa kiasi gani la kimaadili hazingatii maana mtoto akiharibika siyo wake.

Tupo leo na kizazi cha vijana kukataa ndoa mabinti nao kuvua vua chupi hovyo,kama binti kipindi akiwa mtoto alishuhudia dada yake (house girl wao) akipigwa mpini sebuleni na muuza genge (maana hawa ndiyo wabaya kwa wafanyakazi wa ndani huko mitaani) leo ataona ajabu gani kuvua nguo hovyo afanye ngono?na huko kugongwa kuna mawili apate mimba awe singo mama au ukimwi,hii yote sababu wakati alipokuwa anahitaji msingi wa malezi ya mama yake huyu mama alikuwa ameenda kutafuta pesa.

NB;oweni std 7,form 4&6 hawa hawana mambo mengi ya sijui nataka nikafanyie kazi ujuzi wangu niliosomea muhimu mke ajue kusahihisha homework za watoto the rest fanyeni wenyewe.
Mkuu Sina la ziada yote niliyotaka kuongea umeyasema kiufupi umeongea ukweli mtupu .Kiufupi mwanamke kiasili ni housewife wa kulea mume na watoto na kufanya kazi za nyumbani hayo mengine ni kwenda against nature.

Ndiyo maana hata akipata hizo pesa Bado zinamsaidia yeye na wazazi wake na kumfanyia mambo yake mwenyewe sababu nature haijawatune wanawake kuwa watafutaji wahudumie watoto wanafosi tu.
 
Back
Top Bottom