Ni kipi chanzo na tiba ya misuli ya jicho kutikisika?

Ni kipi chanzo na tiba ya misuli ya jicho kutikisika?

Kuna jambo ambalo tangu utoto nimekuwa nikilisikia na wengi kuliamini, kuna kitu kinacheza juu au chini ya kope za jicho.

Huko bara wana amini jicho likicheza upande wa juu huwa ni bahati hivyo tarajia kupata taarifa njema, lkn kuna Imani kwamba jicho likicheza upande wa chini ni dariri ya kutoa machozi, hivyo tarajia taarifa mbaya kama misiba, magonjwa au kupoteza pesa na kadhalika.

UZOEFU WANGU:

Nimekuwa nikitokewa na vitu hivyo: 80% baada ya kufuatilia nimejikuta ikitokea hivyo. Mfano upande wa juu wa kope za jicho langu ziliwahi kuwa zinacheza, (yaani kinakuja kitu kama mtetemo), kwa muda wa wiki mbili, baadae nilipigiwa simu kuitwa kwenye interview na nikapata kazi, kuna matukio mengi mengine siyakumbuki lkn nakumbua pia ilinitokea wakati nasubiri matokeo ya mtihiani ambao nilifauru vizuri sana, kwa kifupi ikitokea mara nyingi huwa napata good news ambayo sikutarajia. Lakini pia niliwahi kutokewa upande wa chini wa jicho, niliogopa sana. Nilikaa kimya na baade nilipata taarifa za msiba, kuna wakati nilipata taarifa za magonjwa. Hali hii huwa haitokei mara kwa mara.

Kuna Imani kwamba ikiwa unatokewa na jicho kucheza upande wa juu yaa ni juu ya kope usimwambie mtu kwaani unaweza kufukuza bahati.

Anaefahamu ukweli wa hili jambo atujuze, MSHANA JR tunaomba elimu yako ya kiroho hapa.


Aksante.
 
Uhalisia/ukweli wa jambo lolote huanza na imani. Imani huumba. Kwa vile ushaamini basi kwa upande wako ishakuwa ndio uhalisia.
 
Jamani kwa muda wa siku tatu jicho langu la kulia upande wa chini linacheza nini maana yake?
Afu nikilala naota mara niko shule nafanya mtihani wakati mwingine naota nimepigwa risasi. Wadau hii imekaaje?
Naomben mnisaidie jamani
 
Leo asubuhi hapa ofisini nilipata mteja anahitaji kukata insurance ya Gari..kwenda kuchukua kitabu cha stika nikakikosa nikapanic nikahisi kimeibiwa yaani niketafuta mpaka ikabidi mteja aondoke nikaendelea kukitafuta huku nikepanic na boss wangu alikuwa ameshafika akaanza kuninenea mbovu...Mara Mimi sio mtunzaji maneno kibao, baada ya lisaa nikashangaa Jicho LA kushoto limeanza kucheza automatically nikajikuta nimeenda directly kwenye box store kugusa bahasha nikakikuta huko ndani...kweli nikaamini nguvu ya jicho...sikutegemea yaani...coz nilikuwa nimekwisha jianda kufungwa kwa kweli...mpaka sasa hivi nimeshangaa kwanini jicho lilivyocheza tu ndo nimepata nilichokuwa natafuta.
 
Habari Wadau.
Naombeni msaada wa hilo Jambo la JICHO la kushoto kucheza mara kwa mara(Siku3) Mwenye ufahamu na swala hili. Karibuni Wadau
 
Mimi liliwahi kunicheza kama mwezi mzima hasa nikifumba macho imeisha now hata sikujua nini tatizo.
 
Hata mimi huwa linacheza sana ila kwa sasa nahisi lipo half time, likianza tena nitakustua.
 
Kama una madeni ni vema ukalipa na kuhakikisha hudaiwi, epuka ugomvi wa kutupiana vitu

Utapata dharura nyingi hivyo jiwekee akiba ya fedha
 
Wasalaam,

Naomba kwa mwenye uelewa na suala la ''kucheza kwa jicho'' anisaidie nini sababu na je linahusiana na kundi lipi kati ya hayo hapo juu.

Jambo hili limekuwa likinitokea mara nyingi sana, nyama ya juu au chini, jicho la kulia au la kushoto, ilimradi tu jicho limecheza.

Natanguliza shukurani, Mungu awatunze.

Amen.
 
ts biological, ila ukitaka liwe la kiimani, inawezekana pia, coz what u strongly believe itakuwa, imani ni chochote
 
Ni nini kinatokea,na tafsiri yake ni ipi??
Kiingereza chake ni "eye twitching" husababishwa na kuwa mfadhaiko, "stress", matumizi mengi ya vichocheo kama caffeine, au jicho kuwa kavu n.k.

Lakini kiimani, itategemea na imani za kwenu maana imani zinatofautiana, binafsi huwa siamini hivyo.
 
Ni nini kinatokea,na tafsiri yake ni ipi??
Ni tatizo la kiafya tu pale kunapotokea contraction of eye muscles kusiko kwa kawaida.

Mara nyingi husababishwa na sress,kuchoka,jicho kavu,maumivu ktk jicho,vichocheo kama coffeine,allergy hata kileo pia.

Mambo ya Imani waulize bibi na babu zako wa ukoo watakujuza jicho likicheza maana yake nini
 
Back
Top Bottom