Ni kipi kifanyike ili kuondoa wizi maofisini na katika mashirika ya Kiserikali?

Ni kipi kifanyike ili kuondoa wizi maofisini na katika mashirika ya Kiserikali?

Kuna MTU mmoja aliwahi kusema kama kuna wanaume wenye miujiza basi ni wabongo MTU ana familia mke na watoto watatu plus mchepuko na jioni anakaa viti virefu bar,michango ya harusi watoto English medium.mshahara lk 3 au 4 huo sio muujiza ni nn? Wataacha kuiba kwa hali hiyo?au nasema uongo Ndugu zangu?
Huu kweli muujiza
 
Piga RISASI tumalizane na hoja hizo, tumechoka kusikia mambo hayo masikioni. Kutumbuliwa kama jipu haijatosha. Mama jitoe, tundika watu kwenye mti, twanga RISASI hadharani uone kama kuna mtu ataiba tena pesa ya umma. CHINA wamefanya hivyo na wamefaulu.
 
Toa maoni yako hapa,

Jambo gani lifanyike ili kudhibiti wizi wa Mali na fedha za serikali?

Je, mishahara ni kidogo?
Marupurupu yaongezwe?

Unadhani ni kipi kiboreshwe ili kukomesha hali hiyo?
Pawepo na Sheria ngumu dhidi ya Mwizi
Sheria hiyo iwe wazi na adhabu ziwe wazi bila kificho
Kama mtu kukatwa Kichwa,Basi bila kificho,na kama ni kukaa ndan,akae ndani miaka isiyopungua 15 ikiambatana na adhabu kali

Mwisho
Iondolewe Kinga ya Rais kutoshtakiwa
 
Toa maoni yako hapa,

Jambo gani lifanyike ili kudhibiti wizi wa Mali na fedha za serikali?

Je, mishahara ni kidogo?
Marupurupu yaongezwe?

Unadhani ni kipi kiboreshwe ili kukomesha hali hiyo?
Hakuna cha kufanya wacha yaende hivohivo

Sent from my Moto E (4) using JamiiForums mobile app
 
Hakuna cha kufanya wacha yaende hivohivo

Sent from my Moto E (4) using JamiiForums mobile app
Mkuu, kama Taifa, tunaona kabisa juhudi za watu kutaka kulikwamua Taifa letu, lakini kuna Baadhi ya Watanzania vilevile wanaoturudisha nyuma Kwa uwizi

Tunataka angalau tufahamu ni kipi tufanye kama Taifa kudhibiti huu uwizi wa Mali zetu
 
Tatizo wafanyakazi wameshagundua wanasiasa wanafaidi zaidi keki ya Taifa. Hivyo wanapo pata nafasi na wenyewe wanajimegea.

Haiwezekani Mbunge anayejua tu kusoma na kuandika, anakaa miaka mitano tu Bungeni! lakini mafao yako ni zaidi milioni 200! Halafu mfanyakazi anayefanya kazi miaka 30-40, analipwa mafao ya milioni 60!

Nalo neno
 
Hakuna la maana kama utawala wa Sheria kuchukua Mkondo wake

Ni Kama nilivyosema mwanzo
Sheria ngumu na adhabu,ni moja ya kuendea mafanikio.
Tubadili mfumo wa Sheria zilizopo.na tuangalie Sheria faidishi kwa Wote
 
Hakuna la maana kama utawala wa Sheria kuchukua Mkondo wake

Ni Kama nilivyosema mwanzo
Sheria ngumu na adhabu,ni moja ya kuendea mafanikio.
Tubadili mfumo wa Sheria zilizopo.na tuangalie Sheria faidishi kwa Wote
Nimekuelewa chief!!
 
Toa maoni yako hapa,

Jambo gani lifanyike ili kudhibiti wizi wa Mali na fedha za serikali?

Je, mishahara ni kidogo?
Marupurupu yaongezwe?

Unadhani ni kipi kiboreshwe ili kukomesha hali hiyo?

Mkuu Pslmp habari. Tabia ya wizi inaweza kupungua pale takwa la "Uadilifu" katika kazi linapokuwa kigezo muhimu cha kumpatia mtu uongozi bila kusahau hata hivyo Elimu ya Mtu na uwezo wake wa kazi. Kwa muono wangu somo la Uadilifu & Uzalendo lingeanza kufundishwa mashuleni hata kabla ya kuanza kufundisha somo la Historia. Juhudi za kupanda mbegu ya uadilifu katika jamii zinatakia ziwe endelelevu (Mazoea Hujenga Tabia) kuanzia kwa watoto wadogo. Hebu angalia tabia za ndugu zetu wa Zanzibar, kiukweli maakuzi yao yanawafanya watu kule "Automatically" kuwa waadilifu.

Nadhani Mama yetu (Rais wa JMT) Mh. Samia Suluhu Hasani aliweke hili jambo liwe mojawapo ya vipaumbele vyake hadi pale kosa la wizi wa mali ya umma lionekane kuwa kosa la aibu kama mtu kujulikana ana magonjwa ya zinaa.

Ahsante
 
Back
Top Bottom