Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Vipi hapa imekaaje wakuu?

View attachment 2470699
screenshot_20230106-072248-jpg.2470699

Naomba niulize hizi paa ambazo zimechongoka namna hii yaani ni karibia vertical zinatokana na nini? Ni fashion ya sasa hivi au kuna jingine? Hizi roof zingefaa sehemu zenye snow ili snow itereze isigandamize nyumba!
 
Fundi wa Wiring alitokota. Heater za Maji moto zote zimeungua, AC imeungua, circuit breaker inasumbua na kujiswitch off kila mara kwenye kipindi hiki cha mvua. Radi ikipiga au kumulika Mbeya Mjini mimi huku Rungwe kanajiswitch off. Very interesting.
 
Nilivyouziwa sikua nagari, nikajenga nikamaliza na njia ya kuingilia na kutokea ilikuwepo kwasababu wakati wa ujenzi gari ya vifaa ilikuwa inaingia Hadi site.

Sasa nimehamia nikakaa miezi 6 nikanunua gari Alieniuzia tukaanza mgogoro mara apande miti sehemu ninayo pita mara aanzishe biashara ya tofari sehemu ninayo pita kiasi cha kubakisha kichochoro cha wapita kwa miguu.

Nikampeleka kwa mjumbe akaambiwa angoe miti yake akingoa siku chache ana panda tena, nikaona Bora niuze nikajenga sehemU salama yenye majirani wanaojielewa sio yule chawivu anaetamani kila mtu atembee kwamguu.
Pole sana
 
screenshot_20230106-072248-jpg.2470699

Naomba niulize hizi paa ambazo zimechongoka namna hii yaani ni karibia vertical zinatokana na nini? Ni fashion ya sasa hivi au kuna jingine? Hizi roof zingefaa sehemu zenye snow ili snow itereze isigandamize nyumba!
Pia bati hazivuji au kuoza
 
Kwa tunaoanza kujenga kwa mara ya kwanza...anza kwa kujenga kakibanda chako ishi humo then unaanza kujenga kile unachotaka (nyumba ya ndoto yako) polepole unakuwa umetuliza akili.
Ndicho nilichokifanya ,, i wish watu wangesoma hii comment kisha wakaifanyia kazi ,sina stress ya uhifadhi wa vifaa wala kuibiwa hovyo wala uharibifu mwingi ,, nyongeza nimezungusha fensi
 
Pia vyumba nilivyojenga vya uani baadae kimoja ni stoo, kingine ni jiko la nje (familia zetu jiko la ndani pekee ujiandae kwa uchafu mwingi na kuziba makaro na wadudu kama mende) na laundry room (hii room itakuwa na sehemu ya mashine ya kufulia , kupasi ,kuweka nguo chafu , kuweka nguzo zisizovaliwa tena (give away) nk

Epuka kujenga karo la kuoshea vyombo nje refu nimeona wengi sana wamekosea hili
 
Pia vyumba nilivyojenga vya uani baadae kimoja ni stoo, kingine ni jiko la nje (familia zetu jiko la ndani pekee ujiandae kwa uchafu mwingi na kuziba makaro na wadudu kama mende) na laundry room (hii room itakuwa na sehemu ya mashine ya kufulia , kupasi ,kuweka nguo chafu , kuweka nguzo zisizovaliwa tena (give away) nk

Epuka kujenga karo la kuoshea vyombo nje refu nimeona wengi sana wamekosea hili
Urefu kiasi gani usiohitajika
 
Nilitoka Ulaya nakiwa nime-save bilioni moja nikitaka nijengewe nyumba yenye ubora sawa na Ulaya. Mafundi wa Dar es Salaam ambar walikuwa wanafisiwa na watu wengi walinifanyia kazi ya hovyo kiasi kwamba maji ya moto yalikuwa hayatoki, nyumba inavuja, rangi haijapakwa vizuri. Tulikaa mwaka mmoja, tukaamua kuhama. Kwa kuwa kiwanja kilikuwa ni prime plot na ilinichukua miaka mingi kukusanya pesa za kukinunua. Sikutaka kuishi kwenye nyumba ambayo sikuwa na furaha. Nikaamua kuibomoa nyumba yote, nikakopa benki halafu nimkatafuta architect kutoka Afrika ya Kusini, nikachora ramani mpya. Nikatafuta kampuni ya ujenzi kutoka Cape Town (Wana uzoefu wa kujenga nyumba za kwenye fukwe au mija yenye joto). Nyumba mpya imenipa furaha kubwa. Somo: Mafundi na wachoraji wa ramani wetu (with all due respect) wanakosa exposure lakini wanaamini wanajua kila kitu. Tanzania tumejifungia Saną; tunahitaji kujifunza kutoka nchi nyingine. Tunahitaji kuwatia moyo watt wasafiri kwenda Afrika ya Kusini, Kenya na kwingine kote tukiwa tumefungua moyo na akili wa kutaka kujifunza. Kama unataka prime property/high end house, nakushauri uangalie njee ya mipaka ya Tanzania.
Naweza kukubaliana na wewe. TZ tuna changamoto ya mafundi. Yes wanajua kujenga. Lakini exposure ni tatizo. wazuri wapo Lakini ni wa kutafuta kwa tochi.

kuna mmoja nilikuta kafanya kazi kwa jamaa yangu nikampa kazi. Lakini Huwezi amini tulipelekana mpaka Polisi. Ukimpa pesa humuoni for the next five days.

kiukweli bongo ujanja ujanja siyo kwenye siasa tuu. Ni kila fani. Ingawa ujenzi ni zaidi.

quality bado sana. Ndo maana ukiangalia kwa umakini, finishing za maana ni kule kule wanakokaa wadosi…..
 
Wasichokielewa wengi ni kwamba hao wataalamu mnaowasema hawana utaalamu wowote kuwazidi mafundi wapo mafundi wameenda shule wamepoteza miaka 5 au 3 utamuambia nini na yuko practical zaidi mainjinia wengi hawawezi na hawajui kazi ni makaratasi tu injinia mwenyewe anamtegemea fundi kufanya hesabu na ujenzi kiufupi ni amubane fundi yeye afanikiwe

Msiwadharau mafundi ila Mara nyng maboss ndio wanaosababisha nyumba kujengwa chini ya kiwango kumminya fundi unatoa hela ya material labda million 14 halafu hela ya ufundi laki 8 au million upaua nyumba kwa bati la kigae/versatile halafu hela kiduchu kwa ushauri wa paa nitafute inbox kukufanyia kazi ni ngumu kwani nabanwa Sana na muajiri Wang muda sipati na sipendi kuacha mafundi saiti wakaharibu kazi ya mteja
Mkuu hakuna anayemdharau fundi hapa. Huhitaji kuongea mengi. Wacha kazi ya mikono yako iongee.
 
Back
Top Bottom