Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Nilivyouziwa sikua nagari, nikajenga nikamaliza na njia ya kuingilia na kutokea ilikuwepo kwasababu wakati wa ujenzi gari ya vifaa ilikuwa inaingia Hadi site.

Sasa nimehamia nikakaa miezi 6 nikanunua gari Alieniuzia tukaanza mgogoro mara apande miti sehemu ninayo pita mara aanzishe biashara ya tofari sehemu ninayo pita kiasi cha kubakisha kichochoro cha wapita kwa miguu.

Nikampeleka kwa mjumbe akaambiwa angoe miti yake akingoa siku chache ana panda tena, nikaona Bora niuze nikajenga sehemU salama yenye majirani wanaojielewa sio yule chawivu anaetamani kila mtu atembee kwamguu.
🤣🤣
 
Kuna ndugu yangu alikuwa anajenga kwa simu.. Kila akiambiwa tuma hela anatumaaa ilaa anaandika.. nyumba ya vyumba viwili na sebule kuja kupiga tu idadiya tofali alizonunua ni 5000 sasa picha la cement na mabati ndo utaliaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nilitoka Ulaya nakiwa nime-save bilioni moja nikitaka nijengewe nyumba yenye ubora sawa na Ulaya. Mafundi wa Dar es Salaam ambar walikuwa wanafisiwa na watu wengi walinifanyia kazi ya hovyo kiasi kwamba maji ya moto yalikuwa hayatoki, nyumba inavuja, rangi haijapakwa vizuri. Tulikaa mwaka mmoja, tukaamua kuhama. Kwa kuwa kiwanja kilikuwa ni prime plot na ilinichukua miaka mingi kukusanya pesa za kukinunua. Sikutaka kuishi kwenye nyumba ambayo sikuwa na furaha. Nikaamua kuibomoa nyumba yote, nikakopa benki halafu nimkatafuta architect kutoka Afrika ya Kusini, nikachora ramani mpya. Nikatafuta kampuni ya ujenzi kutoka Cape Town (Wana uzoefu wa kujenga nyumba za kwenye fukwe au mija yenye joto). Nyumba mpya imenipa furaha kubwa. Somo: Mafundi na wachoraji wa ramani wetu (with all due respect) wanakosa exposure lakini wanaamini wanajua kila kitu. Tanzania tumejifungia Saną; tunahitaji kujifunza kutoka nchi nyingine. Tunahitaji kuwatia moyo watt wasafiri kwenda Afrika ya Kusini, Kenya na kwingine kote tukiwa tumefungua moyo na akili wa kutaka kujifunza. Kama unataka prime property/high end house, nakushauri uangalie njee ya mipaka ya Tanzania.
Hapa waswahili wenzangu wakiona umeandika nyumba ya billion moja wanaogopa. wengi watasema hii ni chai. YET KIUHALISIA kwa mtu anayekaa Europe au North America, hiyo ni pesa inayofikika kabisa kiutafutaji. Hapa bongo hizo nyumba zipo nyingi tuu ila zinajengwa na watu ambao (wengi wao) ni wezi wa pesa za serikali.

Bottomline, watanzania wengi tumejifungia sana. Hata ukienda hapo Nairobi au Cape Town, utajifunza mengi.
 
nishapambana vya kutosha na naamini sijapigwa sana kwenye ujenzi....sasa niko kwenye hatua ya kuweka tiles, wajuzi naomba kujua tiles gani ni bora kwa livingi room, dining room, na bed room, ikiwapendeza chooni pia na zile za jikoni....
 
Back
Top Bottom