Ni kwa asilimia ngapi ukizaliwa familia ya kifukara unaweza kutoboa?

Ni kwa asilimia ngapi ukizaliwa familia ya kifukara unaweza kutoboa?

Tatizo una akili ambazo unafikiri Kwa kutumia masabuli!!
Mm nimezaliwa Familia maskini kabisa!!
Tena Baba allinikataa! na Mama aliolewa na mwanaume mwingine. Hivyo Mimi nilelewa na Bibi Mungu amlaze mahali pema Bibi yangu!!
Niliishia Elimu ya msingi. Lakini nilisoma QT mjini Moro Kwa Rikado maria,( peku peku) niliishi Moro takribani miaka 19

Nikijidhughulisha na shughuli mbali mbali. Ikiwepo kufuga kuku, na nilipata tenda ya kupeleka nyama ya ngo'mbe kwenye chuo kikuu kimoja hapo mjini Moro.

Lakini alikuja COVID-19 ilinirudisha nyuma Kwa kiasi kikubwa!! Sikukata tamaa!! Nikarudisha mpira Kwa kipa. Nikarudi Singida. Singida tuna neema ya mabwawa mengi!! nikajiingiza kwenye shughuli za uvuvi. Kwa kifupi mpaka Sasa namiliki million 50 nipo Tabora Loya..
Acha kukariri dogo! Mungu ni mwema Kwa Kila mtu!!
Kuhusu kupeleka tenda kumetoa watu, sema hapo kucheza na watu wa manunuzi kumtoa kiaina , mi mzee wangu alikuwa mtu wa kuwapa watu tenda kwenye chuo x wamenyanyuka kweli Hawa matajiri wa Moro, si tulikuwa wadogo hatukujitambui mpaka kastafu Sasa.
 
Kutoboa ni namna wewe utakavyoamua kufanya mambo ambayo wengine hawafanyi, either kwa kuogopa au kwa mazoea tu!
 
Kuhusu kupeleka tenda kumetoa watu, sema hapo kucheza na watu wa manunuzi kumtoa kiaina , mi mzee wangu alikuwa mtu wa kuwapa watu tenda kwenye chuo x wamenyanyuka kweli Hawa matajiri wa Moro, si tulikuwa wadogo hatukujitambui mpaka kastafu Sasa.
Mi covid 19 ndiyo iliyoniharibia!! Nilishawashika watu wa stoo, jikoni na manunuzi. Wacha nijipange niatachukua tu tena tenda hio!!
 
Kutoboa kupo inategemea na akili zako ukitumia kigezo cha umaskini wenu kama kikwazo cha mafanikio yako wallah hutoboi
 
Back
Top Bottom