Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Ni wapi Julius Nyerere aliwazidi "ujanja" wazee wa mjini,born town na Watoto wa K'koo? Wazee wake na gwiji wetu wa historia Mohamed Said

Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja DSM tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.

Maelezo mengi ya Wazee yanaonyesha Julius aliaminiwa mapema sana na kupewa madaraka ndani ya chama na hatimaye baadae kuja kuwa Rais wa TAA/TANU na hatimaye nchi.Vijana wenzake waliompokea mjini wakebaki kuwa wao wao watoto wao na wajukuu wao kuwa Julius baada ya Uhuru "aliwasahu"

Wazee wengi wanahisi Julius aliwazidi ujanja na kuwaweka kando baada ya kuchukua nchi.Mitaa ya Kata ya Ng'ambo Tabora,miaka kumi iliyopita nilipata kuwaona wazee wawili,wajanja wa mjini waliompokea Nyerere ktk harakati zake mkoa wa Tabora.Mzee mmoja akiitwa Pacha,akiishi eneo la "filter" pembeni ya kilabu moja maarufu ya pombe mjini Tabora.Mzee mwingine akiitwa Rehani.Huyu kwa heshima kuna mtaa Tabora uliopewa jina lake.Unaitwa mtaa wa Rehani.Kuna Rehani A na Rehani B.

Hawa wote ukikaa nao watakuambia "Julius ni mjanja sana,alituzidi maarifa".Ukija K'koo kuna wazee wengi wapo na malalamiko na wengine wamekufa nayo.Sikumbuki ni Sykes yupi kati ya hao naowasikia.Lkn miaka miwili au mitatu iliyopita...Jijini Nairobi,kwenye Uwanja mdogo wa ndege wa maarufu kama "Wlison Airport" majira ya adhuhuri kuelekea alasiri.Nakutana na Wanawake wawili.Moja Mama wa makamo na mwingine mdada wa umri wa juu kidogo.Huyu Mama bila shaka ni mke wa marehemu na huyu wa pili bintiye.

Hawa wanajiandaa kupakia mwili wa ndugu yao,ni marehemu.Maafisa wa Uhamiaji wanatazama passport zao za kusafiria na kuona ni pass za kidiplomasia. Wanatakiwa kuusafirisha mwili wa ndugu yao kuja Dsm.Wamekodi ndege ndogo aina ya C208. Yenye uwezo wa kubeba watu wanne tu.Lakn wale wanawake wakiwa na ndugu wengine wanakubaliana kubeba maiti na wao kuja DSM.

Ndege ndogo,ktk ubanano na majonzi ya msiba wale wamama wanabanana na maiti ikiwa ndani ya mkeka kuileta Dsm.Ndege ya C206 ni ndogo sana kwa umbali wa Nairobi to Dsm, tena ukiwa na maiti,na hasa kwa wanawake.Kuuliza kwa ndugu waliobaki pale Uwanjani kufanya mpango wa kwenda Jomo Kenyatta ili waje Dsm,wanasema huyo alipata kuwa mpigania uhuru wa Tz,balozi mashuhuri na mwanadiplomasia mbobezi.

Pale pale wanaanza kung'aka kuwa hawa ni wapigania uhuru waliosahaulika na nchi,ndio maana wanabebwa na ndege ndogo aina ya C206 kurudi kwao.Ni malalamiko tu ya "kusahauliwa" muda wote wa maongezi yao.

Akija humu Mzee wangu Mohamed Said, atakutajia kina Mshume Kiyate(?), atataja kina Dosa, mara kina Tewa Said Tewa na wengine wengi kuwa hawa nao hawakufaidi matunda ya Uhuru. Hivi kwani huyu Julius alikuwa na ujanja kiasi gani hawa wote akawaingiza "mjini" wakati wao ndio waliompokea?

Nilitembelea Kilwa,kule kuna Kilwa ya Kivinje na Kilwa Kipatini. Huku Kilwa Kipatini ndio kwao na Kingunge.Huku kuna Kanisa kongwe sana la miaka mingi walijenga Wajerumani. Kanisa hili ndipo alibatizwa Kingunge N. Mwiru. Wengi hudhanj Kingunge hakuwahi kuwa na dini kabisaaa. Kumbe huyu ni mbatizwa ktk Kristo, kabla ya kwenda Usoviet na kuachana na dini.Lkn kwa kubatizwa huyu anaitwa "Ambrose Ngombare Mwiru".

Huku Kivinje kuna watu nao wanasema "Julius alituzidi ujanja". Hivi huu "ujanja" waliozidiwa hawa wote ni kwa sbb ya nini? Ni kwanini walimpokea na kumpa uongozi halafu baadae walalamike?Kwanini wasingemnyima?Je baada ya Uhuru hawa "walalamishi" wote walitaka Julius afanye nini ili walidhike?

Leo ninaomba majibu, nijue, ni wapi Julius, kijana wa Kizanaki aliwazidi "ujanja" hawa vijana wa mjini wa K'koo?
Cc Ngongo UncleBen Barbarosa Ritz
Mzee saidi Mohammed mpaka leo anamlaani Mh nyerere kwa kuwanyima wazee wa kariakoo madaraka wale wazulu wahamiaji kutoka koloni la wareno na kusaidia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964
 
Madai yako ni imaginable ndiyo maana Pro. Haroub alishangazwa na madai yako.
Kwa elimu na wakati alioshi P. Haroub asingelishangazwa na madai yako ikiwa Yalikuwa kwenye ukweli.
Unadanganya hadi unapitiliza na kujishitaki mwenye.
Let..
Hapana sithubutu kuandika uongo katika historia ya uhuru wa Tanganyuika kwa sababu wenyewe waliopigania uhuru huo walikuwa hai.

Ngombale Mwiru alikuwa yu hai yeye aliingizwa TANU na Ally Sykes haya kaeleza mwenyewe.

Prof. Haroub hakuwa anajua ule udugu uliokuwapo kati ya Mwalimu na Abdul.

Prof. Haroub hakuamini hadi alipokwenda kumuuliza Ahmed Rashad yale ambayo yeye hakuyaamini.

Ahmed Rashad na Abdul Sykes walijuana 1936 wakiwa watoto wadogo na wakawa marafiki ndugu hadi Abdul alipofariki 1968.

Ahmed Rashaad alimweleza kila kitu Prof. Haroub kiasi akamwambia ikiwa wewe unashangaa kuambiwa kuwa Abdul Sykes ndiye aliyekuwa nguvu katika kuasisi TANU utashangaa pia nikikuambia kuwa African Association iliasisiwa na baba yake Abdul, Mzee Kleist Sykes mwaka wa 1929?

Mimi ndiye niliyepata mshangao mkubwa zaidi kuwa Prof. Haroub hakuwa anaijua historia ya TANU.

Nitakueleza kitu ujue kuwa Prof. Haroub hakuwa anazijua siasa na historia za watu wa Dar es Salaam.

Prof. Haroub alikuwa mshenga wa kutaka kuposwa bint ya Ahmed Rashaad.

Walipofika nyumbani kwa Ahmed Rashaad na shughuli imeanza Prof. akatoka barua kumpa Ahmed Rashaad na walikuwa wamekaa pamoja bega kwa bega na Abbas Sykes.

Ahmed Rashaad hakupkea barua hiyo akamwambia amkabidhi Abbas Sykes.
Prof. akaja kunieleza kisa hiki na kuniuliza kwa nini aliambiwa posa ile ipokelewe na Abbas Sykes?

Nikampa historia nzima ya Mzee Rashaad na Abdul Sykes na kuwa ule urafiki baada ya kifo cha Abdul ulihamia kwa Abbas.

Ndipo nikajua kuwa Prof. Haroub si mjuzi wa historia yetu.
Ningeandika uongo sasa hivi nishafedheheka.

1679323039523.jpeg

Kulia Sheikh Ahmed Islam, Ahmed Rashad Ali na Prof. Haroub Othman 1997​
 
Mzee saidi Mohammed mpaka leo anamlaani Mh nyerere kwa kuwanyima wazee wa kariakoo madaraka wale wazulu wahamiaji kutoka koloni la wareno na kusaidia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964
Nelson...
Hapana siwezi kumlaani mtu imani yangu inakataza.

Wala sikuandika kitabu cha Abdul Sykes kwa kuwa wazee wangu hawakupewa madaraka katika serikali.

Wala wazee wangu hawakupigania uhuru ili wao waje kukalia viti.

Mimi nimeandika kitabu kusahihisha historia ya TANU ambayo ilijaa makosa mengi sana.

Ukisoma kitabu hutokuta popote nilikotaja kugawana madaraka.
Hayo mengine nimeyakalia kimya kwa kuwa naona si muhimu kuyasemea hapa.

Unajua mchango wa hao akina mama hapo chini katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

1679324742095.png
 
Ni wapi Julius Nyerere aliwazidi "ujanja" wazee wa mjini,born town na Watoto wa K'koo? Wazee wake na gwiji wetu wa historia Mohamed Said

Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja DSM tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.

Maelezo mengi ya Wazee yanaonyesha Julius aliaminiwa mapema sana na kupewa madaraka ndani ya chama na hatimaye baadae kuja kuwa Rais wa TAA/TANU na hatimaye nchi.Vijana wenzake waliompokea mjini wakebaki kuwa wao wao watoto wao na wajukuu wao kuwa Julius baada ya Uhuru "aliwasahu"

Wazee wengi wanahisi Julius aliwazidi ujanja na kuwaweka kando baada ya kuchukua nchi.Mitaa ya Kata ya Ng'ambo Tabora,miaka kumi iliyopita nilipata kuwaona wazee wawili,wajanja wa mjini waliompokea Nyerere ktk harakati zake mkoa wa Tabora.Mzee mmoja akiitwa Pacha,akiishi eneo la "filter" pembeni ya kilabu moja maarufu ya pombe mjini Tabora.Mzee mwingine akiitwa Rehani.Huyu kwa heshima kuna mtaa Tabora uliopewa jina lake.Unaitwa mtaa wa Rehani.Kuna Rehani A na Rehani B.

Hawa wote ukikaa nao watakuambia "Julius ni mjanja sana,alituzidi maarifa".Ukija K'koo kuna wazee wengi wapo na malalamiko na wengine wamekufa nayo.Sikumbuki ni Sykes yupi kati ya hao naowasikia.Lkn miaka miwili au mitatu iliyopita...Jijini Nairobi,kwenye Uwanja mdogo wa ndege wa maarufu kama "Wlison Airport" majira ya adhuhuri kuelekea alasiri.Nakutana na Wanawake wawili.Moja Mama wa makamo na mwingine mdada wa umri wa juu kidogo.Huyu Mama bila shaka ni mke wa marehemu na huyu wa pili bintiye.

Hawa wanajiandaa kupakia mwili wa ndugu yao,ni marehemu.Maafisa wa Uhamiaji wanatazama passport zao za kusafiria na kuona ni pass za kidiplomasia. Wanatakiwa kuusafirisha mwili wa ndugu yao kuja Dsm.Wamekodi ndege ndogo aina ya C208. Yenye uwezo wa kubeba watu wanne tu.Lakn wale wanawake wakiwa na ndugu wengine wanakubaliana kubeba maiti na wao kuja DSM.

Ndege ndogo,ktk ubanano na majonzi ya msiba wale wamama wanabanana na maiti ikiwa ndani ya mkeka kuileta Dsm.Ndege ya C206 ni ndogo sana kwa umbali wa Nairobi to Dsm, tena ukiwa na maiti,na hasa kwa wanawake.Kuuliza kwa ndugu waliobaki pale Uwanjani kufanya mpango wa kwenda Jomo Kenyatta ili waje Dsm,wanasema huyo alipata kuwa mpigania uhuru wa Tz,balozi mashuhuri na mwanadiplomasia mbobezi.

Pale pale wanaanza kung'aka kuwa hawa ni wapigania uhuru waliosahaulika na nchi,ndio maana wanabebwa na ndege ndogo aina ya C206 kurudi kwao.Ni malalamiko tu ya "kusahauliwa" muda wote wa maongezi yao.

Akija humu Mzee wangu Mohamed Said, atakutajia kina Mshume Kiyate(?), atataja kina Dosa, mara kina Tewa Said Tewa na wengine wengi kuwa hawa nao hawakufaidi matunda ya Uhuru. Hivi kwani huyu Julius alikuwa na ujanja kiasi gani hawa wote akawaingiza "mjini" wakati wao ndio waliompokea?

Nilitembelea Kilwa,kule kuna Kilwa ya Kivinje na Kilwa Kipatini. Huku Kilwa Kipatini ndio kwao na Kingunge.Huku kuna Kanisa kongwe sana la miaka mingi walijenga Wajerumani. Kanisa hili ndipo alibatizwa Kingunge N. Mwiru. Wengi hudhanj Kingunge hakuwahi kuwa na dini kabisaaa. Kumbe huyu ni mbatizwa ktk Kristo, kabla ya kwenda Usoviet na kuachana na dini.Lkn kwa kubatizwa huyu anaitwa "Ambrose Ngombare Mwiru".

Huku Kivinje kuna watu nao wanasema "Julius alituzidi ujanja". Hivi huu "ujanja" waliozidiwa hawa wote ni kwa sbb ya nini? Ni kwanini walimpokea na kumpa uongozi halafu baadae walalamike?Kwanini wasingemnyima?Je baada ya Uhuru hawa "walalamishi" wote walitaka Julius afanye nini ili walidhike?

Leo ninaomba majibu, nijue, ni wapi Julius, kijana wa Kizanaki aliwazidi "ujanja" hawa vijana wa mjini wa K'koo?
Cc Ngongo UncleBen Barbarosa Ritz
Watu wanacheza bao,kunywa kahawa cku nzima,wanawaza simba na yanga tu kwa nini wasizidiwe ujanja🤣🤣
 
Watu wanacheza bao,kunywa kahawa cku nzima,wanawaza simba na yanga tu kwa nini wasizidiwe ujanja🤣🤣
Kop...
Mathalan nikikuomba ushahidi kuwa wazee wangu walikuwa wanacheza bao na kunywa kahawa siku nzima na wanawaza Simba na Yanga unaweza kuuweka hapa?

Kahawa na kucheza bao ni katika mila za watu wa Pwani kama wengine wanavyokunywa pombe za kienyeji katika vilabu vya pombe zinazouza dengerua, mbege, kimpumu nk.

Hawa unaowakejeli wewe kuwa ni wanywa kahawa na kucheza bao ndiyo waliounda chama cha TANU na kupiogania uhuru wa Tanganyika.

Soma majina ya ''wanywa kahawa na wacheza bao'' waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo August 1954:

Rajab Diwani, Abdul na Ally Sykes, Dossa Aziz, John Rupia, Julius Nyerere, Mshume Kiyate, Max Mbwana, Jumbe Tambaza, Juma Waziri, Rashid Ali Meli, Clement Mohamed Mtamila, Frederick Njiliwa, Iddi Faiz Mafungo, Schneider Abdillah Plantan, Iddi Tulio, Marsha Bilal na Denis Phombeah aliyekuwa Menaja wa Arnautoglo.

Soma pia hapo chini majina ya wanywa kahawa na wacheza bao walioasisi African Association mwaka wa 1929:

Kleist Abdallah Sykes, Cecil Matola, Mzee bin Sudi, Suleiman Majisu, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Ibrahim Hamisi, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Naomba nami nikuulize wakati hawa ''wanywa kahawa'' wanawatayarisha Watanganyika kupigania uhuru wazee wako wewe wanywa pombe za kienyeji siyo siku nzima bali kwa nyakati maalum walikuwa wanafanya nini?

Mwangalie Julius Nyerere hapo chini na ''wacheza bao kutwa nzima na wanywa kahawa'':

1679334690083.jpeg
 

Attachments

  • 1679334745619.png
    1679334745619.png
    1.8 MB · Views: 4
Watu wanacheza bao,kunywa kahawa cku nzima,wanawaza simba na yanga tu kwa nini wasizidiwe ujanja🤣🤣
Kop...
Mathalan nikikuomba ushahidi kuwa wazee wangu walikuwa wanacheza bao na kunywa kahawa siku nzima na wanawaza Simba na Yanga unaweza kuuweka hapa?

Kahawa na kucheza bao ni katika mila za watu wa Pwani kama wengine wanavyokunywa pombe za kienyeji katika vilabu vya pombe zinazouza dengerua, mbege, kimpumu nk.

Hawa unaowakejeli wewe kuwa ni wanywa kahawa na kucheza bao ndiyo waliounda chama cha TANU na kupiogania uhuru wa Tanganyika.

Soma majina ya ''wanywa kahawa na wacheza bao'' waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo August 1954:

Rajab Diwani, Abdul na Ally Sykes, Dossa Aziz, John Rupia, Julius Nyerere, Mshume Kiyate, Max Mbwana, Jumbe Tambaza, Juma Waziri, Rashid Ali Meli, Clement Mohamed Mtamila, Frederick Njiliwa, Iddi Faiz Mafungo, Schneider Abdillah Plantan, Iddi Tulio, Marsha Bilal na Denis Phombeah aliyekuwa Menaja wa Arnautoglo.

Soma pia hapo chini majina ya wanywa kahawa na wacheza bao walioasisi African Association mwaka wa 1929:

Kleist Abdallah Sykes, Cecil Matola, Mzee bin Sudi, Suleiman Majisu, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Ibrahim Hamisi, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Naomba nami nikuulize wakati hawa ''wanywa kahawa'' wanawatayarisha Watanganyika kupigania uhuru wazee wako wewe wanywa pombe za kienyeji siyo siku nzima bali kwa nyakati maalium walikuwa wanafanya nini?

Mwangalie Julius Nyerere hapo chini na ''wacheza bao kutwa nzima na wanywa kahawa'':

View attachment 2559601
View attachment 2559604
 
Kalamu,
Ahsante.

6MRjcs7kDG5uKWWaMU3qtcOm2v3BC5beuP2SHJPW9GLz09rYA5XuSi6jNSWfTs154FlKgAq30wwJHjAD4mAqRQXsTgvuQkeP8dDjMYkO3owRkDC-MFYCs2F6oxGSHJFS0cbGRFutGUB0nlDSoGwIYErCBrw2kdd7ignOmtEEvuyj_rrEJvcwyMSRn5O1d-gy37XysFuRxicLoezItNOs4_nzFx1Ky0P1xr4Yn6TtX8YB8xHCljcC4am1dRopr5B0ggdqG7QICLKIdSpxjB8bbT87_Z0c2TJetCRNDema6Ecg6YX0jCtFRF89K8AwCkdudE5aG2ou-hf7OAEfOVf5k9aTjbKl5eh8HPDQ0S3QLXzd9yW77ymMOMDN1z9rl2nuLlvowqWer9n--sLfw3VqJhPjKHwKB-KLSOjSp72NJ_hZAPWQ1MnMXlzkfXVWTS9vHeA90wZCbtpVUkMOA9tEBB3gfIQmnsyN2ULGpGY9c0AnGM_FdPodqZkel5UzyJXivv1fqvIWSXgl2dmPof-fbhmIU51qObk9aOp1QVFKJ8sIE6VoXB3tC6V7zFGhCEGt40Ig_eGkN167OgyLW8Vkpwic7j7vxhCmUHNIm71-Z_UCFnMZYDYKf1QSyLwoKxZhmOe_GXb9Pv1VlO0JTwNwbQM89yjZILJMyHQZU-sG8BpB0Yt-uJW365prDaoGWuO__wwjapM2S06Ks-IEZp-f3Op1g_ed1P8-t3YI6iMt0j6DbjdfRbXOXrrE4Jt3LjzmVGTclk7R41YfjtV1ixQaq9uo4k3_8XqgeTgZ5Ufi0DZ1CEhGFTmgeloiR2BmNP0g-1fF7J_hzJjW728Zx6gfrFHznqGtt-jhGV7F4pg7vHgqC5IxJkmuLQxRTNAD6UJtCDrr8TavnP4J8HH6acHOviB1dKkevk8JESXDzXV8flpM4vQu2dO4c_abhfMUMYP72zOZcaBEeefBBbeT6BM=w1017-h650-s-no

Madina 2014​
Picha ninayoiona juu yako ni mtu aliyekaa juu ya mlima wa taka, akichimbua kwenye rundo hilo taka na kuzisambaza kila mara. akitegemea kila anayemsambazia ataona thamani ya hizo taka.
Tena anazisambaza kwa kulazimisha.
 
Picha ninayoiona juu yako ni mtu aliyekaa juu ya mlima wa taka, akichimbua kwenye rundo hilo taka na kuzisambaza kila mara. akitegemea kila anayemsambazia ataona thamani ya hizo taka.
Tena anazisambaza kwa kulazimisha.
Kalamu,
Huwezi.kulazimisha chochote mtandaoni.

Kuna "Block" na "Delete.
Rahisi sana.
8elH9U7k7SuxyeAfdCjMl_52qv2BQHAAkXh4bdyvydtgvnRnAYLqY5PB0M6JBuPiEoMT7pc5Slf5lxCA0u0ERwKbzAHp9DapqICLivLBoNnmANL5x_XqtI9AnMDz_ss0gq0yVlIg0I3oerDYa8eAlYvz1n1QshDjyJOn5nLrubq-AsJpBqfGMjbcnNLTYFgm9hXIJEVv2B8MiOlv5K2I2TfjeeD89Yd5C3DSdaSzMOKoqdsaG4aiBUodsmnfEB6waR0LTXDFfsKQnpxp4jJys0l--VxIVbp-JuQWP6LRGb6VR5teJgW8TP0A9aj6-9ZMvyCLXjXErPSBS_VSHrWL8cwfDUr35sH3xRlDOHUlcwhusOWLehvKxeJRxOhElYCvTSOPC9FXQJX-7nVvNr0S95wIiAEgVUFF2MxqjJezOfQz6uhg8pGIpljFC_xLCZ69uWyKc59Sn0LKYayHcNMaPExu_eVkmkNx4kv1R2YCMxVsygRTEjbFfngv3lz5MtK8dv1jsNGTXBfu4ZLiyWma0q2QNuU1yAA0Q9T2WBNLQvXl2rTT4wm-j9O83dtZnLic7gv4CjEqPXmauYz9mwMr9iJpFv-n2LiixucO0XeFku_SSJMFSBAeAmj_C5sIEG2VnC0yhVzaUNa4rJ22Bd9VDkCEC_mJylGSGD1SEolPmAOehVdDrEkVBkMtiRGT0UUsXZ3l5eztrXqRuBQiNiFEoBvDeCXZgF6Yg5_fdV5dPMezlkW1UvR2kjOMND1Wu10Z6Nq1tRCtu4g3S5woayy9PAbWgyMrIEQeejGwKCecBo5oVMRsfaLL14fiBQURYc7Wk9vHX981OGX0hhe3v-srw839cHrkLZD-hMB_rO-dtFjGpmEP76QNR1FNitfKhzCVtSZ9euVX8oNwhG75-KEoTrWU6mLDEX9KuDkK60B2hWMcqMyyD8Ea9o-WS9rkzPWqYtbHhJdrZkYKMDg7LgY=w867-h650-s-no

Muscat









 
Kalamu,
Huwezi.kulazimisha chochote mtandaoni.

Kuna "Block" na "Delete."
Rahisi sana.
Hapana.
Rahisi ni kutobonyeza kitufe hapo nilipoweka maneno yangu. Usibonyeze hicho kidude, hapo mambo yatakuwa yamekwisha.
Hili nakufundisha kama ulikuwa hujui.
Usibonyeze"Reply". Simple!
 
Back
Top Bottom