huu ni mtazamo wako kama mwingine tu naye anayeweza kuja na mtazamo wake juu ya kila awamu....
Kila awamu iliongoza nchi kadili ilivyoona nchi ilipofika..japo wote walifail kwa kushindwa kuyajua kiuhalisia matatizo ya Tanzania na solution, wote walishindwa kujenga mifumo imara ikayoishi karne na karne na kuwa muongozo wa Taifa letu milele.. Wote walishindwa kujenga kizazi cha watanzania chenye uelewa na touch itakayokuwa kama alama ya utanzania...
Awamu ya kwanza tunaisamehe maana jukumu lake kubwa ilikuwa kututoa kwenye ukoloni, baada ya kufanikiwa kwenye hili ikashindwa kuweka muendelezo na kujenga misingi na mizizi imara kwa jamii ya kitanzania ambayo ingeishi mpaka leo baadala yake ikaacha issues dhaifu dhaifu ambazo zimekufa au kuuliwa kirahisi, Failure ya Taifa hili ndio ilianza hapa kwa Mzee Nyerere kwa kushindwa kuweka misingi imara itakayoishi na ingekuwa kama muongozo mpaka leo...
Awamu ya pili yenyewe ilikuja na mtazamo tofauti based na maisha iliyowakuta nayo watanzania, umasikini uliotukuka na mkwamo mkubwa wa kila mahala, nchi ikiwa imejifunga na hakuna kinachoendelea, wanannchi wakivaa matambala na kupanga foleni kwenye maduka ya ujamaa, nchi ilikuwa haina mipango yeyote ya kuendeleza Taifa vs population increase na kuendana sawa na kasi ya uchumi wa dunia..
Awamu iliamua kuleta sera au solo huria na kuifungua nchi iliyokwama na hapa watanzania kwa kiasi fulani wakapata mwamko na kuanza kuijua dunia na uelekeao wake japo elimu duni na wasomi wachache + ushamba wa watu kama moja ya athari ya awamu ya kwanza ukasababusha wahindi na waarabu kutuzidi akili kwa kuziwahi fursa na kutengeneza utajiri uliopindukia....Awamu hii ya pili iliamua kuwatoa watanzania tongotongo na kuifungulia milango na dunia kiasi cha maendeleo ya watu kuanza kushika kasi..
itaendelea..