Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 182,097
- 1,099,383
Ana semina ya siku tano inaendelea Kawe na anamaliza kesho. Nimehudhuria siku zote tangu ianze.[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mwakasege hakukosea kujiita mwalimu, ni mtu anaweza sikilizwa na dini/dhehebu lolote na ukatoka na kitu kikubwa.
Itoshe tu kusema kwamba Mwakasege kweli ni Mwalimu na Neno la Mungu Analijua. Na napenda alivyo simple. Ni neno tu basi hakuna makorokocho mengine wala maigizo.
Somo analofundisha katika semina hii (Maombi ya Kimkakati) ni gumu kidogo lakini anakwenda polepole na anahakikisha kuwa kila mtu anaelewa kwa kadri ya uwezo wake. Ni Neno kwa Neno, Mifano kwa Mifano...
Mungu Azidi kumtunza mtumishi huyu.
Na katika miaka hii minne inayokuja anasisitiza sana tuiombee Tanzania maana itapita katika misukosuko mingi. Ndiyo lengo hasa la semina hii. Kupata makuhani watakaosimama katika zamu zao ili kuiombea nchi yetu kwa maombi ya kimkakati hasa katika miaka hii minne inayokuja...