Ni kweli Mungu hana Upendo? Au sisi tu ndio hatumuelewi!?

Ni kweli Mungu hana Upendo? Au sisi tu ndio hatumuelewi!?

Laana walizopewa Adam na Hawa za kulaaniwa kwa kizazi na kizazi zilitoka kwa nani? Unapaswa kujiuliza sisi vizazi wa Adam ambao leo tunateseka namna hii Tulilaaniwa na nani? Shetani au Mungu,Tafsiri kubwa ya Mungu ni UTAWALA na si UPENDO kama tunavyoambiwa katika imani zetu, ingawa upendo ni tawi lililochanua kutoka kwenye Shina la Utawala wa Mungu....
 
Laana walizopewa Adam na Hawa za kulaaniwa kwa kizazi na kizazi zilitoka kwa nani? Unapaswa kujiuliza sisi vizazi wa Adam ambao leo tunateseka namna hii Tulilaaniwa na nani? Shetani au Mungu,Tafsiri kubwa ya Mungu ni UTAWALA na si UPENDO kama tunavyoambiwa katika imani zetu, ingawa upendo ni tawi lililochanua kutoka kwenye Shina la Utawala wa Mungu....
Matatizo tuliyonayo tumejitakia.wenyewe na.wala hatujalaaniwa na yoyote

Mungu hajatulaani wala Shetani ila.tumejilaani wenyewe!
 
Matatizo tuliyonayo tumejitakia.wenyewe na.wala hatujalaaniwa na yoyote

Mungu hajatulaani wala Shetani ila.tumejilaani wenyewe!

Eiyer nani alikwambia mtoto akifanya kosa nyumbani huwa anajipa adhabu mwenyewe? lazima huwa ni Baba au mama., kama Mungu Avyomuapia mwanamke na Mwanaume kupata shida katika maisha yao yote na Kifo juu?!! Suala la Upendo wa mungu kwa Wanadamu sikatai kama haupo ila unapaswa kujua kuwa hakuna aliye na Hasira kama Mungu sababu hasira yake kwa Adam na hawa kukosea mara moja tu ndiyo inayotupatia shida na taabu mpaka leo!

Tena ukumbuke kuwa makosa hatukukosa sisi ni mababu wa mababu wa mababu, kuhusu upendo wa Mungu tunaamini kama upo kiimani ila haujaonekana dhahiri, ila Hasira yake tunaiona wazi kwa kushudia kwa macho shida, mateso, vifo na Dhiki Duniani.
 
Mleta mada. Mungu aliruhusu taifa lake teule la israel ambalo analipenda, kuangamiza mataifa mengine na Mungu kuwapa israel ardhi zao wamiliki. israel hadi leo hawamjui Mungu. kisa cha mataifa ya kando ya israel kuangamizwa ni kutomjua Mungu wa kweli na wakaabudu masanamu kwa kuwa hawakuwa na mwongozo kama waisrael ambao pamoja na kuwa na miongozo bado waliabudu masanamu ilhali kiongozi wao Musa alikuwa akiwaeleza kuhusu. Mungu wa kweli.

Tuchambulie upendo katika muktadha huu..
 
Eiyer nani alikwambia mtoto akifanya kosa nyumbani huwa anajipa adhabu mwenyewe? lazima huwa ni Baba au mama., kama Mungu Avyomuapia mwanamke na Mwanaume kupata shida katika maisha yao yote na Kifo juu?!! Suala la Upendo wa mungu kwa Wanadamu sikatai kama haupo ila unapaswa kujua kuwa hakuna aliye na Hasira kama Mungu sababu hasira yake kwa Adam na hawa kukosea mara moja tu ndiyo inayotupatia shida na taabu mpaka leo, tena ukumbuke kuwa makosa hatukukosa sisi ni mababu wa mababu wa mababu, kuhusu upendo wa Mungu tunaamini kama upo kiimani ila haujaonekana dhahiri, ila Hasira yake tunaiona wazi kwa kushudia kwa macho shida, mateso, vifo na Dhiki Duniani.
Unakiangalia jambo la adhabu kimakosa sana na hili limesababisha watu washindwe kuelewa mambo mengi

Ninapokosea na kuadhibiwa kimsingi adhabu ile ninakuwa nimeileta mimi yule anaetamka anakuwa anaiwakilisha tu

Unapokwenda kuiba na unajua kabisa kuiba ni kosa halafu ukapelekwa mahalamani hakimu anakueleza adhabu ya kosa lako kwa mujibu wa sheria na sio yeye anaekuhukumu

Sheria imetamka adhabu la kosa lako na unajua,unapoamua kutenda kosa unajiadhibu mwenyewe kwasababu ulitenda bila shuruti
 
mleta mada. Mungu aliruhusu taifa lake teule la israel ambalo analipenda, kuangamiza mataifa mengine na Mungu kuwapa israel ardhi zao wamiliki. israel hadi leo hawamjui Mungu. kisa cha mataifa ya kando ya israel kuangamizwa ni kutomjua Mungu wa kweli na wakaabudu masanamu kwa kuwa hawakuwa na mwongozo kama waisrael ambao pamoja na kuwa na miongozo bado waliabudu masanamu ilhali kiongozi wao musa alikuwa akiwaeleza kuhusu. Mungu wa kweli. tuchambulie upendo katika muktadha huu

Hili umelitoa wapi?
 
Unajua nilishajiuliza maswali mengi sana kuhusu hilo na pia hata kuhusu kwanini tuna dini nyingi na tunatofautiana namna ya kusali mwisho wa siku nilichokielewa kuhusu Mungu ni kwamba Mungu yupo ni mmoja tu ila kwa chini yake kuna miungu wengi ambao hujiita ni yeye lakini hata wao pia ukiwaabudu wanakuja kwake kuomba kulifanikisha unaloliomba kupitia kwao ndio maana akaamua kuturahisishia "usiwe na miungu mingine ila mimi" hapa anamaanisha huko kwingine mtatoa na kutumika kwa gharama kubwa bila faida lakini kwangu ni imani tu.kama unakumbuka kipindi anatoa hizi amri ilikuwa ni kipindi wana wa Israel walipoamua kutengeneza sanamu ya kuchonga kwa kutoa vito vyao.hii ilionyesha upendo wa Mungu kwetu kupitia amri 10 na ambapo anazitoa hizo amri ilikuwa ni kipindi wamemuasi hebu fikiria mtu amekuasi lakini bado unamuonyesha njia sahihi hiyo ndio maana ya upendo.

Kingini nilichokigundua kuhusu Mungu ni imani ukisoma ndani ya Biblia asilimia kubwa kitu tunachohusiwa ni kuwa na imani,imani ni kuwa na hakika ya mambo yanayotarajiwa,Mungu anachotaka kutoka kwetu ni kumuamini anaweza na atatenda hata mafundisho ya Yesu na vitendo vyake vyote ilikuwa ni kuwaonyesha wanadamu sehemu ya kuamini na kwa vile alikuja kwa kutumwa na Mungu ndio maana hakuta awe Miungu mwingine kila alilolifanya alisema ila kwa njia ya Baba hapa anamaanisha aliyeliwezesha ni Mungu Baba ili watu wamuamini Mungu anatenda na anaweza ndio hapo pia zikatoka na dini nyingine lakini zote zinaongelea kuwa na imani na Mungu.hata mababu zetu walimtambua Mungu lakini haikuwa kupitia yeye ilikuwa kupitia Miungu na Mungu anaupendo wa dhati ndio maana hata Miungu ikienda kukuombea muujiza wako anatenda.

Kuna kitu kimoja ambacho wengi tunakikosea kuhusu Mungu wengi tunaweka hisia mungu anatupenda sisi tu tunaomuabudu lakini katika biblia inasema mmoja akiokoka ni sherehe huko mbinguni inamaanisha anajaliwa zaidi yule anaeokoka upya na nadhalia ya Mungu kwa ujumla yeye hutenda kwa yule anaemuamini tu.hata biblia imeandika Mungu kazi na wenye imani isiyokomaa na akatoa na mifano kama watoto wachanga,punje ya haladari na mingine mingi hii yote ni kuonyesha yeye anachohitaji ni imani ya kweli hivyo kama huna imani ya kweli hakuna muujiza.ndio maana wew unalala usiku unasali legelege imani yako haipo kwake ila unasali tu Mungu azilinde kuta nne za nyumba sijui atatuma malaika waje kuzunguka kitanda lakini kuna mwizi alieomba kwa imani Mungu amsaidie aje akuibie na anafanikiwa kukuibia na wewe usiku uliomba unahisi Mungu hana upendo?Mungu anaupendo kazi yake ni kujibu maombi ya wanaomwamini haijalishi ni maombi gani kwa vile ni ya imani asilimia 100 Mungu hutenda humpa yule aaminie.
 
Sasa wewe unawezaje kumzungumzia Mungu bila kuijua biblia? Kiukweli sikwambii imetoka wapi maana nilijua unajua
Inaonekana hujaelewa swali langu lengo lake..

Nimekuuliza hayo uliyoandoka ulipoyatolea,kama ji kwenye Biblia ulipaswa kunijibu na kuniwekea na ushahidi halafu tungeanzai hapo,sijui ni kwanini huwa hamtaki kujibu maswali ....!!
 
Elisha Chuma

Kuna Mungu mmoja tu muweza yote na upande wa pili kuna Shetani,hapa either unamuabudu Mungu au Shetani basi hakuna kingine

Mungu ameweka kanuni ambazo kila mmoja akizifuata atapata matokeo iwe hasi au chanya bila kujali anamjua au hamjui,hivyo unaposema kuna sijui miungu ambayo inakwenda kumuomba huyu mkuu na anafanikisha ni mawazo yako tu!
 
Last edited by a moderator:
Inaonekana hujaelewa swali langu lengo lake..

Nimekuuliza hayo uliyoandoka ulipoyatolea,kama ji kwenye Biblia ulipaswa kunijibu na kuniwekea na ushahidi halafu tungeanzai hapo,sijui ni kwanini huwa hamtaki kujibu maswali ....!!
Mkuu nilifanya makusudi. Kwa namna ulivyoandika mwanzo sikutaka kujipa shida kuweka vifungu kwani nilijua yote haya unayo akilini na moyoni. Kwa wepesi ni kuwa ukisoma Agano la Kale tangu Kutoka hadi Waamuzi ndio utajua mapanzi ya Mungu juu ya Waisraeli na namna alivyowachukia mataifa ya kando kwa kuwa hawakuwa wakimwabudu yeye Mungu wa kweli. Sasa hofu yangu ni kuwa sitapata majibu niliyokuwa natarajia, ila nitakuwekea kifungu specific cha biblia na kwa upeo wako juu ya upendo ujaribu kunijibu swali langu la awali kabisa.

1. Kumb 7: 6-9
2. Kumb 7: 1-4

Soma vyema.

mleta mada. Mungu aliruhusu taifa lake teule la israel ambalo analipenda, kuangamiza mataifa mengine na Mungu kuwapa israel ardhi zao wamiliki. israel hadi leo hawamjui Mungu. kisa cha mataifa ya kando ya israel kuangamizwa ni kutomjua Mungu wa kweli na wakaabudu masanamu kwa kuwa hawakuwa na mwongozo kama waisrael ambao pamoja na kuwa na miongozo bado waliabudu masanamu ilhali kiongozi wao musa alikuwa akiwaeleza kuhusu. Mungu wa kweli. tuchambulie upendo katika muktadha huu
 
Mkuu nilifanya makusudi. Kwa namna ulivyoandika mwanzo sikutaka kujipa shida kuweka vifungu kwani nilijua yote haya unayo akilini na moyoni. Kwa wepesi ni kuwa ukisoma Agano la Kale tangu Kutoka hadi Waamuzi ndio utajua mapanzi ya Mungu juu ya Waisraeli na namna alivyowachukia mataifa ya kando kwa kuwa hawakuwa wakimwabudu yeye Mungu wa kweli. Sasa hofu yangu ni kuwa sitapata majibu niliyokuwa natarajia, ila nitakuwekea kifungu specific cha biblia na kwa upeo wako juu ya upendo ujaribu kunijibu swali langu la awali kabisa.

1. Kumb 7: 6-9
2. Kumb 7: 1-4

Soma vyema.

Sawa nimekuelewa ....

Kwanza Mungu hakuyaangamiza hayo mataifa bali Waisraeli ndio waliofanya hivyo

Pili,sababu ya Waisraeli kupigana vita na hayo mataifa saba sio kwasababu ya hayo mataifa kutomjua Mungu bali ni kwasababu Waisraeli walikuwa wamepewa ardhi ile na Mungu

Sasa kwa mkabala huu swali lako limekosa maana labda ulijenge upya!
 
Sawa nimekuelewa ....

Kwanza Mungu hakuyaangamiza hayo mataifa bali Waisraeli ndio waliofanya hivyo

Pili,sababu ya Waisraeli kupigana vita na hayo mataifa saba sio kwasababu ya hayo mataifa kutomjua Mungu bali ni kwasababu Waisraeli walikuwa wamepewa ardhi ile na Mungu

Sasa kwa mkabala huu swali lako limekosa maana labda ulijenge upya!

huna hoja
 
Unakiangalia jambo la adhabu kimakosa sana na hili limesababisha watu washindwe kuelewa mambo mengi

Ninapokosea na kuadhibiwa kimsingi adhabu ile ninakuwa nimeileta mimi yule anaetamka anakuwa anaiwakilisha tu

Unapokwenda kuiba na unajua kabisa kuiba ni kosa halafu ukapelekwa mahalamani hakimu anakueleza adhabu ya kosa lako kwa mujibu wa sheria na sio yeye anaekuhukumu

Sheria imetamka adhabu la kosa lako na unajua,unapoamua kutenda kosa unajiadhibu mwenyewe kwasababu ulitenda bila shuruti

Kwa hiyo unataka kuniambia mwizi akiiba huwa anajichoma moto mwenyewe? ni wazi kabisa kuwa bado tunaishi kwenye hasira ya Mungu na ametuahidi kwamba atatusamehe ila bado hajatenda hivyo, hapa tulipo tuna imani kuwa kuna siku Mungu, ataitupilia mbali adhabu aliyotupatia, Mungu hafananiki kwa uweza na nguvu, hivyo unapaswa kujua siku yoyote saa yoyote mungu akiamua tu kusema basi inatosha, kila kitu kitakaa sawa na hatutaona shida tena.

Mungu alikuwa na uwezo hata wa kuwasamehe kina adam tangu siku ile ile waliyofanya kosa, ila sababu alipata hasira kali ndo maana mpaka sisi vizazi wa vizazi tunaendelea kuteseka kwenye ile hasira ya Mungu, ila Sio kwamba Mungu akiamua kutumalizia hizi taabu hawezi!, La hasha anaweza sana, ila bado ana hasira na ndo maana anatuahidi kuwa atakuja, tena atakuja mwanae sio yeye kuwahukumu wazima na wafu, maana inaonekana Mungu ana hasira kali mno kwetu..
 
Kwa hiyo unataka kuniambia mwizi akiiba huwa anajichoma moto mwenyewe? ni wazi kabisa kuwa bado tunaishi kwenye hasira ya Mungu na ametuahidi kwamba atatusamehe ila bado hajatenda hivyo, hapa tulipo tuna imani kuwa kuna siku Mungu, ataitupilia mbali adhabu aliyotupatia, Mungu hafananiki kwa uweza na nguvu, hivyo unapaswa kujua siku yoyote saa yoyote mungu akiamua tu kusema badi inatosha, kila kitu kitakaa sawa na hatutaona shida tena, Mungu alikuwa na uwezo hata wa kuwasamehe kina adam tangu siku ile ile waliyofanya kosa, ila sababu alipata hasira kali ndo maana mpaka sisi vizazi wa vizazi tunaendelea kuteseka kwenye ile hasira ya Mungu, ila Sio kwamba Mungu akiamua kutumalizia hizi taabu hawezi!, La hasha anaweza sana, ila bado ana hasira na ndo maana anatuahidi kuwa atakuja, tena atakuja mwanae sio yeye kuwahukumu wazima na wafu, maana inaonekana Mungu ana hasira kali mno kwetu

Kwanza Mungu ana uoendo mkuu na ndio maana alikuja na kufa kwasababu ya makosa yako uliyojitakia mwenyewe

Halafu unapokatazwa kufanya jambo na ukaambiwa adhabu yake ni viboko kumi halafu ukafanya huku unajua kabisa adhabu yake,ukitandikwa utakuwa umejitandika mwenyewe au laa?
 
Back
Top Bottom