Ni kweli Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulishinikizwa na mabeberu?

Ni kweli Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulishinikizwa na mabeberu?

Muungano ulipangwa hata kabla ya mapinduzi, Moja ya malengo ya hayo mapinduzi ilikua ni huo Muungano
Wakati anapewa nchi alipewa maagizo kuhusu Zanzibar ,Kwanza ni Sultan Jamshid bin Abdullah bin Busaid na pili ni wakomunist walikuwa Zanzibar kina Babu,Hanga,Sultan nk.Maslahi ya Muingereza ,Rumi na Anglikana.
 
Ahaa, kwa hiyo hizi tetesi za mabeberu kuhusika halina ukweli wowote sio..
Mijadala ilianzia Anatouglo na kukamilukia Lancaster house.Kulikuwa na pande tatu,TANU Kwa upande mmoja upande wa pili Rumi na Anglikan na upande wa tatu Beberu.
 
Hao mabeberu ndio waliokua master planer, Unafikiri Zenj bila ya baraka ya Mabeberu kungelifanyika mapinduzi? Mbona Bara mapinduzi yalishindikana licha ya kua Nyerere alikua kashivishwa Hijabu na kukimbia.
Wakaagiza kabisa,akishapinduliwa wee mpokee halafu ataomba Kuja huku nasi tutampokea,na ataishi hapa bila kukusumbua.
 
Sasa ni kwa Nini waliwapa Uhuru Ile serikali ya waliyoiacha, Kisha baada ya miezi michache wapange tena kuipindua?

Si wangeacha kuipa Zanzibar Uhuru chini ya Waarabu?
Muda wa ukoloni ule ulikuwa umeisha hivyo ilibidi waikabidhi Zanzibar kwenye Mikono salama.Sultan hawakutaka kumtoa kwa Mikono yao ndo maana wakamtafuta mtu wao ili amalizie kazi.
 
Kwa Zaire naweza nikaelewa, Lumumba alikuwa communist, na serikali za kikomunisti zilikuwa zikipinduliwa kipindi kile
Ila Zanzibar serikali ya Waarabu haikuwa na itikadi za kikomunisti. Sababu ilikuwa ni nini
Ukomunist ulikuwa mkali Zanzibar,Kuna wasomi wengi walikuwa wamesoma Urusi ya Zamani,Cuba ,China na Misri.Akina Kassim Hanga,Mohamed Abdul Rahman Babu na wengine.Mwandishi Shafi Adam Shafi akamtungia kitabu bwana Denge akiyetuhumiwa na serikali ya kikoloni kwa ukomunist kinaitwa Vuta N'kuvute.
 
Kusema kwamba tumewahonga ili tuendee kuwatafuna..sema nini mahaba ya zenji matamu..bahari yote ipo Tanganyika.

#MaendeleoHayanaChama
Asikudanganye mtu Zanzibar inatawaliwa na Tanganyika.Angalia TPDF,Police,Waziri mkuu,Uchaguzi ndani ya CCM,mikataba na mataifa ya nje,biashara ya nje,fedha ,bank kuu nk.
 
Hata kama, lakini kungekuwa na namna hata Serikali ingejaribu kuyazima hata Kama ingeshindwa, lakini inaonyesha Kama walikuwa usingizini Hadi mlugaluga kama Okello akaweza ku organize mapinduzi nchini mwao

Na hata Kama wasingekuwa na uwezo basi wangeomba mataifa rafiki wangewapa msaada Kama wangegundua hiyo hatari mapema
Okelo alitumika tu kuficha ukweli,michezo ikipangwa magogoni.
 
Wakati anapewa nchi alipewa maagizo kuhusu Zanzibar ,Kwanza ni Sultan Jamshid bin Abdullah bin Busaid na pili ni wakomunist walikuwa Zanzibar kina Babu,Hanga,Sultan nk.Maslahi ya Muingereza ,Rumi na Anglikana.

MKuu Hizbu ilikua ndio tatizo kubwa kwa Mabeberu Zanzibar kuliko wote hao
 
Hizbu ndio watu gani?..nifahamishe mana hili neno nalisikia sana.

#MaendeleoHayanaChama

MKuu hizbu kilikua ni chama cha siasa kipindi cha kupigania uhuru ambacho ndio walikua mahasimu ASP ambacho kikiitwa ZNP hilo jina la Hizbu ni umaarufu wao. Hao ndio walioshinda uchaguzi wa uhuru na Nchi ilipata Uhuru chini yao, ASP kwa kupitia msaada wa TANU walfanya mapinduzi 1964 na ndio haya yanayolindwa na CCM mpaka hii leo.
CUF Ya Maalim Seif imekua ndio mbadala wao tokea 1992 Baada ya Vyama Vingi kuruhusiwa tena kwa mara nyengine Nchini.
 
MKuu hizbu kilikua ni chama cha siasa kipindi cha kupigania uhuru ambacho ndio walikua mahasimu ASP ambacho kikiitwa ZNP hilo jina la Hizbu ni umaarufu wao. Hao ndio walioshinda uchaguzi wa uhuru na Nchi ilipata Uhuru chini yao, ASP kwa kupitia msaada wa TANU walfanya mapinduzi 1964 na ndio haya yanayolindwa na CCM mpaka hii leo.
CUF Ya Maalim Seif imekua ndio mbadala wao tokea 1992 Baada ya Vyama Vingi kuruhusiwa tena kwa mara nyengine Nchini.
Katika chaguzi zilizoganyika lati ya 1960-1963 ZNP ilikuwa kwenye calition na ZPPP cha Mohamed Shamte na huo muungano ndo ilishinda majimbo Mengi ila kura ya mtu mmojammoja ukiIhesabu,ASP ilikuwa na idadi kubwa.Vyama vyote vikimtambua Sultan ka ndiye sovereign wa Zanzibar,baada ya Mapinduzi,Sultan akaitwa jina bovu hata ilipozaliwa wakasema CUF itrejesha Sultan,Zanzibar
 
MKuu hizbu kilikua ni chama cha siasa kipindi cha kupigania uhuru ambacho ndio walikua mahasimu ASP ambacho kikiitwa ZNP hilo jina la Hizbu ni umaarufu wao. Hao ndio walioshinda uchaguzi wa uhuru na Nchi ilipata Uhuru chini yao, ASP kwa kupitia msaada wa TANU walfanya mapinduzi 1964 na ndio haya yanayolindwa na CCM mpaka hii leo.
CUF Ya Maalim Seif imekua ndio mbadala wao tokea 1992 Baada ya Vyama Vingi kuruhusiwa tena kwa mara nyengine Nchini.
Hizbu maana yake chama/kundi,ni jina mbadala la kiarabu
 
Katika chaguzi zilizoganyika lati ya 1960-1963 ZNP ilikuwa kwenye calition na ZPPP cha Mohamed Shamte na huo muungano ndo ilishinda majimbo Mengi ila kura ya mtu mmojammoja ukiIhesabu,ASP ilikuwa na idadi kubwa.Vyama vyote vikimtambua Sultan ka ndiye sovereign wa Zanzibar,baada ya Mapinduzi,Sultan akaitwa jina bovu hata ilipozaliwa wakasema CUF itrejesha Sultan,Zanzibar

Ni propaganda uchwara za CCM tu, ASP kuwa na idadi ya kura nyingi haikuwa Point ya msingi kabisa mana sheria za nchi hazikua zikizingatia hilo jambo. Hata Trump alikua Rais wa U.S bila ya kuwa na kura nyingi kuliko mshindani wake.

CCM wamekua na porpaganda za kipuuzi kabisa. Kwa bahati mbaya nchi yetu bado imejaa wajinga na ndio mana wapo watu wamekua wakiwaamini.
 
Dawa hapa ni kuwa na Serikali moja na Zanzibar iwe kanda kama zilivyo kanda za huku bara. Kama ilivyo kanda ya kati, Ziwa, Kusini na nyinginezo na huko kuwe na kanda ya Zanzibar na mikoa yake.
 
Hivi unafikiri hao Zanzibar watakubali kufutiwa Serekali yao?
'Rhetorical question' ulilouliza ndilo sahihi kuanzia wakati wa kujadili Muungano wetu. Serikali ya Tanganyika ilikufa. Vipi serikali ya Zanzibar isife tukawa na serikali moja tu? Hatusemi Zanzibar imezwe na Bara (kwa kuwa hakuna Tanganyika); au Bara imezwe na Zanzibar. Hoja ni kuwe na nchi moja inayoendeshwa na serikali moja. La sivyo, tuwe na serikali tatu: ya Visiwani, ya Bara, na ya Muungano. Hivi sasa Rais na mawaziri wa Muungano wanaweza kutoka Zanzibar, kwa kuwa nchi ni moja. Lakini hakuna mtu wa Bara anayeweza kuwa Rais, au waziri au hata Mbunge tu wa Zanzibar!
Hivi karibuni Zanzibar ilitangaza masharti ya kununua ardhi nchini Zanzibar kwa wageni; ikafafanua kwamba masharti hayo yanawahusu Raia wa Bara pia. Pamoja na yote hayo, bado kuna Wazanzibari wanaolalamika kwamba Bara inainyonya Zanzibar! Jee, kuna ukweli hapo?
 
Kama mambo yangekua ni mepesi kihivo mbona wangelikua wameshafanya zamani, Ndoto ya Nyerere ya mda mrefu sana ilikua ni kuifuta serekali ya Zanzibar na kuwa na Serekali Moja.
Hayo mambo Hayapo mepesi kihivo
Si kweli kwamba Nyerere alikuwa na mawazo ya Serikali moja tu! Serikali mbili (ukifuta ya Tanganyika) ndiyo yalikuwa mawazo yake. Hoja yake ilikuwa kwamba nchi mbili zinaungana; bila kujali ukubwa au idadi ya watu wa kila upande. Hadhi tu ya kwamba kila upande ni nchi, ndiyo ilikuwa kanuni ya muungano. Sasa, kama ni hivyo, kwa nini alikubali serikali ya Zanzibar ibaki na ya Tanganyika ife? Hilo ndilo swali gumu linalohitaji uchunguzi yakinifu.
 
'Rhetorical question' ulilouliza ndilo sahihi kuanzia wakati wa kujadili Muungano wetu. Serikali ya Tanganyika ilikufa. Vipi serikali ya Zanzibar isife tukawa na serikali moja tu? Hatusemi Zanzibar imezwe na Bara (kwa kuwa hakuna Tanganyika); au Bara imezwe na Zanzibar. Hoja ni kuwe na nchi moja inayoendeshwa na serikali moja. La sivyo, tuwe na serikali tatu: ya Visiwani, ya Bara, na ya Muungano. Hivi sasa Rais na mawaziri wa Muungano wanaweza kutoka Zanzibar, kwa kuwa nchi ni moja. Lakini hakuna mtu wa Bara anayeweza kuwa Rais, au waziri au hata Mbunge tu wa Zanzibar!
Hivi karibuni Zanzibar ilitangaza masharti ya kununua ardhi nchini Zanzibar kwa wageni; ikafafanua kwamba masharti hayo yanawahusu Raia wa Bara pia. Pamoja na yote hayo, bado kuna Wazanzibari wanaolalamika kwamba Bara inainyonya Zanzibar! Jee, kuna ukweli hapo?

Hoja ya Serekali moja ni kitu ambacho kwa wazanzibari haiwez kukubalika, Kwa Tanganyika munaona ni jambo jepesi mana nyinyi ndio mutakaokwenda kunufaika nayo. Je mutakua tayri kuwe na serekali moja ambayo makao mkuu yake yawe Unguja, Raisi wa JMT atoke Unguja, Wakuu wa Idara zote kuanzia TISS, JWTZ, TANPOL na nyengine nazo watoke Unguja, Je watanganyika mutakua tayari nahilo?
 
Back
Top Bottom