Ni mambo gani mepesi kufanyika ambayo huwezi kuyafanya?

Ni mambo gani mepesi kufanyika ambayo huwezi kuyafanya?

1. Kukata chips Kama wanavokata wakaanga chips wanamenya kiazi wwnapiga mistari yao sijui ndo ya diagonal chap vipande vinatokea Mimi nahangaika nitaanza kukata kwenye circle Kwanza ndo circle moja nitoe vipande.

2. Kupiga mlunzi aisee nimeshindwaga

3. Kucheza mziki ni rahisi Ila nishapishana nao naonaga hata Soo kwenye watu wengi kucheza kimasai aisee labda ningekuwaga kwenye team ya dance nikaririshwe zile move Ila me na style yangu moja tu ama mbili za mziki hizohizo naishi nazo sitaki shida.

4. Kufungua kizibo Cha chupa ya bia kwa chupa nyingine..hii kitu imenishinda Nisha jaribu mshikaji wangu yeye akikaa kwenye meza haitaji opener anashika chupa mbili anaziumanisha kwaa moja inaachia sijui huu ujuzi unakuja Kama kipaji ama laa.

5. Kuongea na simu bila kuweka loudspeaker hii Sasa ni tabia imejengeka mpaka naona kuongea bila loudspeaker sikuelewi vizuri labda iwe ishu ya Siri Sana Ila mazungumzo yoyote ya kawaida lazima nikuweke loud
1. Kutoa au kupokea rushwa
2. Kuendelea kuwa Mtanzania kama watapitisha sheria ya kinga mwa maafisa wa usalama,
 
1. Kupiga mluzi, kuna dada mmoja tangu ajue siwezi kupiga mluzi basi kila akiniona anakuja nikuringishia kwa kunipigia mluzi masikioni.

2. Kula taratibu. Yaani kila nikikaa na watu kula pamoja, lazima niwe wa kwanza kumaliza.

3. Kupiga kura, yaani mimi ninyanyuke kwenda kituoni kupiga kura? Lata nikirogwa siendi...

4. Kubargain bei wakati wa kununua kitu. Mimi huwa natoka na bei yangu nyumbani. Ukifika sawa, usipofika natembea mbele...
 
Kuvuta sigara ........ Nishashindwa kabisa ! Sijui wanawezaje kuvuta ,Nilijaribu nikawa na nunua hadi pakiti ,ila najikuta nasahau kuvuta na najikuta nazifulia kwenye nguo

siku moja nikashushuliwa eti sina sura ya uvutaji sigara na pisi kali moja hivi .

Soo nishaamua kuachana nayo tu.
 
Back
Top Bottom