▪ ?Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, mke wa Kaini alitoka wapi?? Ingawa mara nyingi wachambuzi wa Biblia huuliza swali hilo ili tu kuwavuruga watu, Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa.
Katika tunapata habari zifuatazo: (1) Hawa alikuwa ?mama ya kila mtu anayeishi.? (2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu. (3) Baada ya kufukuzwa na kuwa ?mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,? Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ?mtu yeyote akakutana naye? na kujaribu kumuua. (4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. (5) ?Baadaye? Kaini alilala na mke wake ?katika nchi ya Ukimbizi.?? .
Kutokana na habari hizo, tunaweza kusema kwamba mke wa Kaini, ambaye haijulikani alizaliwa wakati gani, alikuwa mzao wa Hawa. Andiko la linasema kwamba katika miaka 930 ambayo Adamu aliishi, ?alizaa wana na mabinti.? Bila shaka, Biblia haisemi waziwazi kwamba mke wa Kaini alikuwa binti ya Hawa. Hata hivyo, kwa kuwa mke wa Kaini anatajwa baada ya Kaini kufukuzwa, jambo hilo linaonyesha kwamba wakati wa kutosha ulikuwa umepita na angeweza kuwa mmoja wa wajukuu wa Adamu na Hawa. Kwa hiyo, tafsiri ya Biblia The Amplified Old Testament inasema tu kwamba mke wa Kaini alikuwa ?mmoja wa watoto wa Adamu.?