Ni matumaini yangu Uongozi wa Simba SC utaandaa Uongo wa kutuambia kwanini Bernard Morrison hatoenda South Africa tarehe 24 April, 2022

Ni matumaini yangu Uongozi wa Simba SC utaandaa Uongo wa kutuambia kwanini Bernard Morrison hatoenda South Africa tarehe 24 April, 2022

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Na GENTAMYCINE najua ili 'Kutuzuga' zaidi na Wawahadae Majuha (Mazuzu) wengi huyu Mchezaji ataambiwa ama ajifanye Kaumia Mechi yetu ya Kwanza na Orlando Pirates FC tarehe 17 April, 2022 au acheze Faulo apate Kadi Nyekundu ili sababu ya Yeye kutoenda Afrika Kusini katika Mechi ya marudiano na Orlando Pirates FC tarehe 24 April, 2022 ipatikane.

GENTAMYCINE niliwahi hapa hapa JamiiForums kuandika kuwa Mchezaji Bernard Morrison ana BAN ya Kutoingia nchini Afrika Kusini kutokana na Vitendo vyake vya Utovu wa Nidhamu kama kawaida ya Mazuzu ( Majuha ) hapa wakaanza Kunitukana, Kunidhihaki na Kunibishia juu ya hili.

Sasa Mimi huyu huyu GENTAMYCINE leo tena kwa Kujiamini kabisa nawaambieni kuwa Mchezaji Bernard Morrison ana BAN ya kuingia South Africa na tafadhali Uongozi wa Simba SC uwaambieni huu Ukweli na siyo Kuficha halafu wakaondoka nae kisha Wakamficha Zimbabwe au Lesotho na Kumlazimisha apige Picha akiwa na Watu katika Treni za Umeme kama alivyofanya Simba SC ilipoenda mwaka Jana Afrika Kusini kucheza na Kaizer Chiefs FC na Kuzitupia Mitandaoni ambapo Waswahili wenye Akili fupi wakaamini kuwa nae aliingia nchini Afrika Kusini.

Endeleeni tu Kunichukia GENTAMYCINE ila Kazi yangu kubwa hapa JamiiForums ni kuwapeni Ukweli, Kuwakosoa, Kuwaelimisha wale Majuha ( Mazuzu ) na Kusifia / Kupongeza pale tu nionapo kuna la maana / tija limepatikana.

Naipenda mno Simba SC yangu ( hata Mwenyezi Mungu anajua ), ila sipendi Unafiki au Kuficha madhaifu ambayo nayaona eti ili tu GENTAMYCINE niwafurahishe 'Followers' wangu hapa JamiiForums na wale Watu ambao Wananipenda na hunisoma sana hapa.

Mwisho namalizia kwa wale wana Simba SC Mazuzu ( Majuha ) mliopo hapa na ambao Kutwa mnanishambulia GENTAMYCINE kwa kusema Ukweli na kutokuwa Mnafiki kwa kuwaambia kuwa kama ambavyo mlikuwa mkishangilia nikiwa Nawananga (Nawasema) wana Yanga SC hapa JamiiForums na wakawa Wanatulia, basi nanyi pia safari hii tulieni hivyo hivyo nikiwa 'nimewachenjia: na sasa 'Nawakandia' ili mjitathmini na ikiwezekana mbadilike na muache Upuuzi na Uswahili wenu mlioubobea.
 
Kutokana na kesi zake za wizi wa magari na wale wanaigeria wawili aliokua nao hapa last year. Ni kweli hatokwenda
Nashukuru kwa Kunielewa, nawe Kulisemea tena Kiufafanuzi zaidi kwani kuna Majuha (Mazuzu) ndani ya Simba SC (hasa Mashabiki) walidhani naongopa, nimekosea na Kukurupuka pia wakiwa Wamesahau kuwa moja ya Sifa Kuu ya GENTAMYCINE ni Kufuatilia Jambo.

Kulichimba, Kulidadisi, kutafuta Maarifa zaidi, Kujichanganya na Watu mbalimbali, kuwa na Vyanzo vingi na aminika vya Taarifa ( Habari ) za Ndani na Ngumu, Kushauri na kutoa Suluhisho lenye Kujenga zaidi katika Jamii au Taasisi husika.
 
Morisson hawez kwenda south africa kwa sabab za kiserikali

Kama msimu uliopita alivyokosa mechi na kaizer chief ile ya 4 -0 south africa ndivyo atakavyokosa tena msimu huu na orlando pirates
Kuna Majuha (Mazuzu) walishajiandaa kuanza kutaka Kunibishia / Kunikatalia hili Mkuu ila wanesahau na pia hawajui kuwa GENTAMYCINE niko mbele yao katika Kudadisi na Kusaka Taarifa Ngumu na zilizojificha ambazo zingine ni Hatari hata kwa Maisha yako ukizifuatilia.
 
Ila pamoja na kujua hivyo bado tu 24/7 ukiwa hapa Jamiiforums ni lazima tu utapitia Mada zangu na Kuzichangia vile vile Kudadadeki.

Mimi ndiyo GENTAMYCINE sina Mfano.
Mimi sina ubaguzi, nawajali hata wale ambao najua akili zao zinahamahama. Nasoma mada maana nakua sijui wakati gani akili yako inakuwa imerudi kwenye ubongo.
 
Kuna Majuha ( Mazuzu ) walishajiandaa kuanza kutaka Kunibishia / Kunikatalia hili Mkuu ila wanesahau na pia hawajui kuwa GENTAMYCINE niko mbele yao katika Kudadisi na Kusaka Taarifa Ngumu na zilizojificha ambazo zingine ni Hatari hata kwa Maisha yako ukizifuatilia.
Kwahiyo unataka tufanye mini?
 
Nashukuru kwa Kunielewa, nawe Kulisemea tena Kiufafanuzi zaidi kwani kuna Majuha ( Mazuzu ) ndani ya Simba SC ( hasa Mashabiki ) walidhani naongopa, nimekosea na Kukurupuka pia wakiwa Wamesahau kuwa moja ya Sifa Kuu ya GENTAMYCINE ni Kufuatilia Jambo, Kulichimba, Kulidadisi, kutafuta Maarifa zaidi, Kujichanganya na Watu mbalimbali, kuwa na Vyanzo vingi na aminika vya Taarifa ( Habari ) za Ndani na Ngumu, Kushauri na kutoa Suluhisho lenye Kujenga zaidi katika Jamii au Taasisi husika.
Una Hip Hop kali sana
 
Back
Top Bottom