Ni mfumo wetu wa elimu mbovu au wanafunzi uelewa upo chini? Nchi nyingi duniani vijana waliosoma ICT ndio matajiri ila kwetu wanazunguka na bahasha

Ustadh tongwe

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2020
Posts
717
Reaction score
1,903
Kama kichwa cha habari kinavyosema hebu tutoe maoni kwanini vijana wa sayansi especially ICT wanahangaika sana wakati Kwa elimu yao wangekuwa na uwezo wa kubuni apps ambazo zingewakwamua kiuchumi badala yake wanahangaika na bahasha kama wahitimu wa procurement & supply.

Mfano wa kijana wa kitanzania aliesoma nje na akabuni apps yake ni Benjamin Fernandez ila waliosoma DIT, UDSM wahitimu wakimaliza wanahangaika sana na bahasha, je tatizo mitaala yetu? Au uelewa ndio tatizo kukariri kupata GPA.
 
Haya mambo yanahitaji zaidi ya elimu.

Mfano.

1. Mitaji.
2. Support ya Serikali.
3. Uchumi mzuri wa nchi.
4. Track record.
5. Elimu kuwa juu kwa watu wengi.
6. Mifumo mizuri ya kodi.
7. High tolerance for failure.
8. Ease of doing business
9. Kujua lugha za kimataifa.
10. Utamaduni unaoruhusu kubadilika haraka.

Haya kumi yote ni matatizo makubwa Tanzania.
 
Wengi watakaofata watarudia haya uliyosema ndugu.
 
wengi watakaofata watarudia haya uliyosema ndugu.
Mimi nimeanzisha Uzi nimeshamuelewa Hila kwenye mtaji tu nadhani ndio tatizo kuu hila support ya serikali nadhani ukienda tume ya sayansi na technology ukienda na ideal yako wanaweza kukusaidia zaidi.
 
Mimi nimeanzisha Uzi nimeshamuelewa Hila kwenye mtaji tu nadhani ndio tatizo kuu hila support ya serikali nadhani ukienda tume ya sayansi na technology ukienda na ideal yako wanaweza kukusaidia zaidi.
Ukienda kwenye tume wakakusaidia zaidi kwa mipango isiyotimizika kwa sababu serikali ina kodi kubwa na kuanzisha biashara kuna vipingamizi vingi, hapo bado hujapata support ya serikali.

Nchi ambayo serikali inazima mitandao haiwezi kutajwa kuwa ni nchi yenye serikali inayo support technical innovation.
 
kuna shida sana kwenye mfumo wetu wa elimu toka primary hadi chuo.
Wanafunzi wanakariri na copy and paste hakuna ubunifu hakuna jitihada binafsi.

Niliwahi kuwashirikisha wanafunzi wanaosifiwa sana chuo cha computer hapa Tanzania kwenye program zangu isee ni shida hakuna developer bongo isee na kama wapo ni wa copy and paste hakuna ubunifu yet they demanding a lot of money wajati hawana ubunifu kiivyoo.
 
Hakuna eco system ya tech bongo ndo tatizo kubwa zaidi hiyo inahusu list yote aliyoorodhesha hapo juu.

Pia hata huko majuu ambapo unafikiri ni mbinguni wanahangaika sana kupata ajira kipindi hiki, soko la tech limeshuka sana nenda sehemu yoyote wanapokutana wahitimu utaona malalamiko inibidi uaply kazi 200-300 kupata hata interview.
 
Kabisa mkuu
 
Inawezekana nchi Haina dira yoyote au kama ipo basi ni kwenye makaratasi tu na si Kwa vitendo, katika suala zima la ujasiriamala mazingira si rafiki kabisa TZ, utasikia serikali imeweka mazingira mazuri lakini ukija ground Hali ni tofauti kabisa, ni kama Kuna nchi au jamhuri mbili, ya kwanza ni nchi au jamhuri ya jukwaani na nyingine ni ya mtaani (field Kwa watekeleza sera).

Kama una roho ndogo, mpenda haki na ni muoga kamwe biashara kubwa hutoiweza TZ, ni ujanja ujanja tu.
 
Hata hapa kwetu wapo watu wa ICT wapo vizuri. Usiangalie tu Chini angalia juu pia kuna watu wengi wametoboa na hii sekta.

Marehemu Ali Mufuruki utajiri wake ni Voda na yeye ndio ana mchango mkubwa kwenye Fiber nchi hii kwa kutuletea Zuku.

Pia kila mtu wa ICT hawi mgunduzi wengi na wao wa natafuta ajira, na usishangae app na program nyingi zinamilikiwa na wajasiriamali na wafanyabiashara mbalimbali na sio watu wa ICT, ngumu sana kukuta mtu kama Bill gate ana skillset zote za IT na ujasiriamali.
 
ICT wa Microsoft office na kupiga window utafanana na wenzetu wanaumiza kichwa na ma AI ndiyo maana mtoto wangu nimesukumizia akasomee KILIMO NA UFUGAJI SUA ili turudi kwenye uzalishaji wa chakula maana technology na ubongo wa muAFRICA ni maji na mafuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…