Ni Mkatoliki 100% ila hizi ni sababu zangu za kwanini Sihudhurii na Sitohudhuria Jumuiya za kila Jumamosi....

Ni Mkatoliki 100% ila hizi ni sababu zangu za kwanini Sihudhurii na Sitohudhuria Jumuiya za kila Jumamosi....

1. Jumuiya kumekuwa ni sehemu za Majungu.

2. Jumuiya imekuwa ni sehemu za Kuchunguzana Kimaisha.

3. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Masutano.

4. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Wanaume Kutongoza na Wanawake kutafuta wa Kuwachapa Nao ( Kuwabandua )

5. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Kutishana kuwa kama hauhudhurii basi Ukifa ( Ukifariki ) Kanisa Katoliki halitokuombea ukiwa Jenezani Kwako.

6. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya kila Siku kuja na Michango isiyo na Kichwa wala Miguu.

7. Jumuiya imekuwa ni Gulio Kuu la kila aina ya Unafiki unaoujua na usioujua hapa duniani.

Halafu Wewe Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wa Jumuiya yangu hivi mnavyonitishia kuwa kama nisipohudhuria Jumuiya Nikifa hamtoniombea mmeshazungumza na Baba Mungu na akawaambieni kuwa ataanza Kunitanguliza Mimi Kaburini kabla yenu? Wapuuzi wakubwa nyie.

Je, mnavyong'ang'ania Kutoniombea GENTAMYCINE pale Nikifa je, ile Siku ninazaliwa mlikuja Agha Khan Hospital mbele ya Sister Brendah na Sister Aghata waliohakikisha Nazaliwa vyema na salama Kuniombea? Wapuuzi wakubwa nyie.

Na nani aliyewadanganyeni kuwa Imani ya Ukatoliki inapimwa kwa Kuja Kwake ( Kuhudhuria ) katika Jumuiya za Kikatoliki kila Jumamosi kama ya hii leo?

Nilichoamua tu na najua hata Mwenyezi Mungu ananibariki nacho ni kwamba nitajitahidi Kuhudhuria Ibada zote za kila Jumapili ( hasa Misa yangu pendwa ya Kwanza ) na kutoa Sadaka na Michango ya Kikanisa kama tu nitakuwa Nimebarikiwa na Uchumi kwa wakati huo na kama sina najua hata Mola / Maulana nae atajua na hatonichukia au kuwa na Usununu ( Kinyongo ) nami.

Nawatakieni nyote Jumuiya njema!!!!
Binafsi naudhika na matumizi mabaya ya mapato ya kanisa. Mapadre ni vimwana na ulevi mtindo mmoja. Hayo ya kutozikwa yanatekelezwa hata kwa wanao sali. Msiba wa rofa misa ina endeshwa na katekista, wa tajiri mapadri ni wahudumu, askofu anaendesha ibada.
 
Malengo ya jumuia ni mazuri kabisa ila viongozi wake ndo tatizo. Unakuta wengine ni walimu na wengine ni viongozi wa vyama vya siasa, kwa hiyo wanatoa amri kama kwa waumini kama wanafunzi au makada wa vyama.
GENTAMYCIME tafuta mwongozo wa jumuia utaona malengo Vs viongozi wa jumuia.
Nachoka kila Siku tu kuwapeni Ufafanuzi kuwa Mimi siitwi huyu Tapeli wa ID na Mpuuzi GENTAMYCIME aliyeiiga ID yangu ili Kusafiria Nyota yangu Kali ya Kiumaarufu hapa Jamiiforums bali naitwa GENTAMYCINE.

Kwanini huwa hamuelewi tu? Nimejiunga hapa Jamiiforums mwaka 2013 Mwezi July na hili Juha lililoiga ID yangu limejunga mwaka huu huu wa 2022 je, hamwoni hiyo tofauti?
 
Asikutishe mtu! Hakuna mwenye mbingu wala jehanamu ya kukupeleeka!! Neno la Mungu likikuweka huru unakuwa huru kweli kweli!! Kwa sisi wahangaikaji jumamosi ni siku ya uzalishaji!! Fanya kazi zako, shiriki shughuli za kijamii, usimuumize mtu!! Achana na hizo mahakama watu walizoziunda ili kunyanyasa wenzao!!
Amina Mkuu.
 
Afu wanadai eti michango ni ya Mungu? Hawa ni wafanyabishara kama wengine tu! Afadhali Hela yangu ya sadaka nimpe yatima au mlemavu barabarani sio haya mambo ya kanisani....kanisani ilipaswa kusiwe na sadaka kabisa.
Umeandika Kitu cha Kiakili mno ila tegemea Majuha wa Kiimani ndani ya Kanisa / Makanisa kuja Kukupinga kwa hili na hata Kukushambulia pia.

Wenye Akili Kubwa na zilizobarikiwa tumekuelewa vizuri sana tu Mkuu / Kiongozi.
 
1. Jumuiya kumekuwa ni sehemu za Majungu.

2. Jumuiya imekuwa ni sehemu za Kuchunguzana Kimaisha.

3. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Masutano.

4. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Wanaume Kutongoza na Wanawake kutafuta wa Kuwachapa Nao ( Kuwabandua )

5. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Kutishana kuwa kama hauhudhurii basi Ukifa ( Ukifariki ) Kanisa Katoliki halitokuombea ukiwa Jenezani Kwako.

6. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya kila Siku kuja na Michango isiyo na Kichwa wala Miguu.

7. Jumuiya imekuwa ni Gulio Kuu la kila aina ya Unafiki unaoujua na usioujua hapa duniani.

Halafu Wewe Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wa Jumuiya yangu hivi mnavyonitishia kuwa kama nisipohudhuria Jumuiya Nikifa hamtoniombea mmeshazungumza na Baba Mungu na akawaambieni kuwa ataanza Kunitanguliza Mimi Kaburini kabla yenu? Wapuuzi wakubwa nyie.

Je, mnavyong'ang'ania Kutoniombea GENTAMYCINE pale Nikifa je, ile Siku ninazaliwa mlikuja Agha Khan Hospital mbele ya Sister Brendah na Sister Aghata waliohakikisha Nazaliwa vyema na salama Kuniombea? Wapuuzi wakubwa nyie.

Na nani aliyewadanganyeni kuwa Imani ya Ukatoliki inapimwa kwa Kuja Kwake ( Kuhudhuria ) katika Jumuiya za Kikatoliki kila Jumamosi kama ya hii leo?

Nilichoamua tu na najua hata Mwenyezi Mungu ananibariki nacho ni kwamba nitajitahidi Kuhudhuria Ibada zote za kila Jumapili ( hasa Misa yangu pendwa ya Kwanza ) na kutoa Sadaka na Michango ya Kikanisa kama tu nitakuwa Nimebarikiwa na Uchumi kwa wakati huo na kama sina najua hata Mola / Maulana nae atajua na hatonichukia au kuwa na Usununu ( Kinyongo ) nami.

Nawatakieni nyote Jumuiya njema!!!!
Yaani hili POPOMA nimezaliwa nalo hospitali moja, ila popoma leo umeongea point, eti wana mikwara ukifa hawakuombei
 
Tafuta hela ,ukiwa na hela hukosi wa kukuzika watajaa hata wasiokujua ,wapenda kula mtaani watajaa kwenye mahema.Huo ni utaratibu was duniani Mungu hausiki nao
Hakika Mkuu na nimeliona hili mahala.
 
Mimi nasikia nadaiwa viwawa huko hata sielewi. Tena kibabe na kilazima. Katika suala la michango hapana aisee. Too much. Sihudguriagu hata ikiwa inasali kwetu. Wengi naonaga wanafiki tu. Kama mtu siongei nar naenda kusali Mungu si ataniadhibu kwa unafki?
Mimi Binti wa Mwenyekiti wa Jumuiya yangu Nimembandua na alivyojua akaanza Kunichukia cha Kushangaza tena huyo huyo akiniona akiwa na wana Jumuiya ananisalimia Kikatoliki Tumsifu Yesu Kristo na kujifanya ananihimiza nihudhurie Jumuiya hivi huu kama siyo Unafiki Uliotukuka ni nini?
 
sawa,hiyo ni jumuiya yako mkuu. Umechukua hatua gani kusaidia hili ?Tatizo halikimbiwi na inawezekana wewe ndiye wa kusaidia kuirudisha jumuiya kwenye mstari wa unyoofu.
GENTAMYCINE nasomwa mno na Watu Wakubwa na Muhimu ( tena wa Kada mbalimbali ) hivyo nina uhakika Watu Kanisa Katoliki hasa Katibu Mkuu wa TEC Mwalimu wangu wa Media Law na aliyekuwa pia Vice Chancellor wangu SAUT Mwanza 2006 hadi 2009 Genius Fr. Dkt. Charles Kitima.

Pia na Mwalimu wangu Mpendwa aliyeniambukiza Ujiniasi wake Uliotukuka na aliyenifundisha Print Media na Somo lake pendwa la Critical and Logical Thinking ( sasa Askofu Mkuu Jimbo la Kondoa Mkoani Dodoma ) Dk. Bernadine Mfumbusa kwa pamoja watakuwa wameuona huu Uzi wangu Mwanafunzi Wao GENTAMYCINE na watayafanyia Kazi kwa Niaba ya Kanisa langu Takatifu la Katoliki.
 
Nini ni ulevi kama ulevi mwingine
"Nini"
Umeandika kwa kutizama kwa jicho hasi ila umesahau kuwa jumuiya ni msingi wa imani kwani huwaleta wakristu pamoja kama kanisa moja.Hiyo ni moja ya faida pamoja na faida zingine nyingi ikiwemo kusali pamoja. Kama umeona mapungufu nilitegemea kama mkristu makini ungekuwa wa kwanza kurekebisha kasoro hizo ndogo ndogo na kusisitiza watu wahudhurie!
Wale hawarekebishiki atakaloamua kiongozi ndio hilohilo,
 
Kuna ULAZIMA gani na upi kuzikwa na ibada? Ina maana hiyo ibada itasaidia nini? Itafuta dhambi zako? Ibada ni Hofu za kidini na kiimani tu! Ukisha kufa umekufa hakuna anaye jua huko uliko nini kina endelea.
Huwa nafurahi na napenda mno Kusoma Maoni ya Watu Werevu ( Intelligent ) kama Wewe hivi hapa Jamiiforums. Hongera Mkuu.
 
1. Jumuiya kumekuwa ni sehemu za Majungu.

2. Jumuiya imekuwa ni sehemu za Kuchunguzana Kimaisha.

3. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Masutano.

4. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Wanaume Kutongoza na Wanawake kutafuta wa Kuwachapa Nao ( Kuwabandua )

5. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Kutishana kuwa kama hauhudhurii basi Ukifa ( Ukifariki ) Kanisa Katoliki halitokuombea ukiwa Jenezani Kwako.

6. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya kila Siku kuja na Michango isiyo na Kichwa wala Miguu.

7. Jumuiya imekuwa ni Gulio Kuu la kila aina ya Unafiki unaoujua na usioujua hapa duniani.

Halafu Wewe Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wa Jumuiya yangu hivi mnavyonitishia kuwa kama nisipohudhuria Jumuiya Nikifa hamtoniombea mmeshazungumza na Baba Mungu na akawaambieni kuwa ataanza Kunitanguliza Mimi Kaburini kabla yenu? Wapuuzi wakubwa nyie.

Je, mnavyong'ang'ania Kutoniombea GENTAMYCINE pale Nikifa je, ile Siku ninazaliwa mlikuja Agha Khan Hospital mbele ya Sister Brendah na Sister Aghata waliohakikisha Nazaliwa vyema na salama Kuniombea? Wapuuzi wakubwa nyie.

Na nani aliyewadanganyeni kuwa Imani ya Ukatoliki inapimwa kwa Kuja Kwake ( Kuhudhuria ) katika Jumuiya za Kikatoliki kila Jumamosi kama ya hii leo?

Nilichoamua tu na najua hata Mwenyezi Mungu ananibariki nacho ni kwamba nitajitahidi Kuhudhuria Ibada zote za kila Jumapili ( hasa Misa yangu pendwa ya Kwanza ) na kutoa Sadaka na Michango ya Kikanisa kama tu nitakuwa Nimebarikiwa na Uchumi kwa wakati huo na kama sina najua hata Mola / Maulana nae atajua na hatonichukia au kuwa na Usununu ( Kinyongo ) nami.

Nawatakieni nyote Jumuiya njema!!!!
We bwana kitu Kama huwezi waachie wanao weza. Wengine apa tunahudhuria jumuiya kwa burudan kabisa. Au hiyo jumuiya yenu ndio ina shida nahisi. Jaribu kuchunguza
 
Hawa watu bn Padri aligoma kuja kusali kweny mazishi ya baba angu kisa ety alikua ahudhulii hivo vikao vyao vya asubui ety hadi tutoe faini me nkamwambia tu bi mkubwa mine natafuta wasabato waje wamzike mshua angu eeeeh nkatoa taarifa hapo S.D.A haraka haraka wakaja kutuongezea ibada hadi siku ya mazishi
Safi sana huwa napenda Watu 'Defiant' kama Wewe Mkuu. Na najua Walikukoma pia.
 
Kuna wakati nilitafakari kurudi jumuia. Nilimtafuta mwenyekiti nikamweleza nia yangu.

Akaniambia kwa kuwa alishanifuta kwenye register, basi niende akanipe maelekezo.

Maelekezo yenyewe alimuita Katibu ambaye alikuja na karatasi yenye list ya michango ya miaka mitatu. Kila mwaka ni laki na nusu, kwa hiyo, nilipe laki 4 na nusu ili niweze kuendelea na Jumuia.

Nilimwambia sawa. Sikutekeleza na jumuia siendi, maana sikumwelewa kabisa
Mkuu huwezi amini Nimecheka mpaka basi kwa hii post yako na kila nikiikumbuka tu najikuta naangua Kicheko tu. Hakika Jamiiforums ni raha mno na Burudani tosha.
 
Unaweza kuwa na point, ila uko totally wrong kwa kuyaleta huku badala uwapelekee wahusika, (M/Kiti wa Jumuiya ) ama paroko wako kabisa.
Pili, Kanisa Katoliki haliwezi kubadili utaratibu wake eti sababu ya mtu au watu wachache wazembe na wavivu na ma cowards kushindwa kuhudhuria jumuiyani na hivyo kutafuta visababu uchwara ambavyo vinaweza kupatikana popote kwenye kikundi cha watu.
Tatu, wewe ni coward na Popoma mkubwa 🤣☹😊
Sawa Baba Askofu ila najua Sindano yangu ya Leo imewaingieni vyema tu na najua mtayafanyia Kazi haya yote ambayo GENTAMYCINE nimetiririka na kuserereka nayo Kwenu.
 
Kwani Buji na Genta ni ndugu moja?!mbona kama kuna sehemu mmejichanganya hivi .......
Tunajuana kwakuwa huwa tunalewa Kiwanja Kimoja na Kugombania Mabaamedi wa Sinde Pub Mbezi Beach Tangi Bovu.
 
Malalamiko haya yanafumbiwa macho kila kukicha. Kwa nini hakuna suluhisho mpaka hivi sasa?

Mimi ni mu-RC ila kiukweli hizi jumuiya hazijafit objectives ya kuanzishwa kwake.

Nina imani viongozi wetu ni wasomi mtalifanyia kazi hili jambo. MALALAMIKO NI MENGI
Hawawezi kuchukua hatua yeyote, maana wananufaika na mfumo unaopigiwa kelele.
 
Dini aliyotaja mtoa mada ni corporate..core product Imani Ila Kuna bidhaa muambata Kama elimu,afya nk,pia rushwa(ruzuku) toka kwa wanasiasa ili wawaswagie waimini wakati wa uchaguzi,utasikia huyu ni chaguo la mungu
Dini na siasa ni kama mjomba na shangazi, hivi vitu viwili vina undugu kihistoria.
 
Back
Top Bottom