Ni msanii gani wa Kenya anakubalika sana Tanzania?

Eti wakorea [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hiyo point yako haina mashiko,,mbona muziki wa Nigeria unapigwa mpaka kwenye vilabu vya pombe za kienyeji huko Vijijini pamoja na kwamba watu hawaelewi kiingereza?,,mbona nyimbo za injili za wanamuziki wa Kenya zinapigwa sana Bongo

Kwenye hiyo sekta hamna cha kujitetea,,kajipangeni tena mrudi na majibu mazuri
 

Miziki kuchezwa kwenye vilabu sio issue, maana nimecheza sana disco kwenye vilabu vyenu na kawaida DJ huchezesha wimbo wowote na tunaruka tu, lakini nachokisema japo mtabishia hadi kuzimu ila mwenyewe nimejionea kwa macho yangu sitegemei kuambiwa, ni vigumu sana umkute Mtanzania amenunua CD anacheza wimbo usio wa Bongo flava, nyie hamna mtindo mwengine wowote nje ya huo mmoja.

Mara nyingi kwenye laptop yangu nilikua naona kwamba nikiwa na Watanzania halafu niweke nyimbo za kimataifa wanakereka japo kimya kimya, hadi pale nitaweka Bongo akina Diamond ndio unaona kila mtu anachangamka, nchi yenu diversity haipo kabsa, mkiingizwa kwenye zizi moja mnajazana humo, hakuna anayeweza kunyanyua kichwa na kuona chochote kingine nje.
 
Naona unajitahidi kuremba mwandiko.
 

Wewe unandika hisia zako tu.hamna utafiti makini umefanya katika hilo.

Ungejua kwamba wabongo tunapenda mziki mzuri,regad lugha au rangi,tunaruka na kusikiliza tu.though hatunaga shobo za moja kwa moja na wasanii wa nje.na hivi unaona sababu ni wazi music industry ya bongo sasa hivi imekua,ni ngumu sana kupenya humu msanii mpya tokea nje.tunawajua wale ambao tayari walikwishakupata majina kitambo.

Ndio maana humu unasikia wakitajwa watu kama kina nonini,jua kali,nyashiski,jaguar,wahu etc.
 

Sijazungumzia mambo ya lugha, naongea kuhusu mtindo mmoja yaani hata humo Tanzania aibuke msanii aimbe kwa Kiswahili lakini mtindo ambao sio Bongo flava, ataishia kuskliza nyimbo zake mwenyewe na mkewe. Halafu pia kwenu huwa mumegawanyika kwenye timu mbili hata ndani ya hiyo Bongo flava, kuna Mondi na Kiba, wengine wote ni wasindikizaji tu, yaani naifahamu Bongo vizuri sana, hata kwenye michezo hamna diversity, ni mpira tu na wenyewe timu mbili Yanga na Simba, zingine zote zinasindikiza tu.
Ndio athari za ujamaa, huwa unalemaza mtu akili kiasi kwamba hana uwezo wa kutumia akili zake, lazima afuate mkumbo na ndio kipindi fulani hata Kikwete aliwahi kuwaomba muwe mnajiongeza sio kupelekeshwa pelekeshwa, angalia hata kwenye siasa, chama kimoja tangu mzungu awaachie nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…