Ni msanii gani wa Kenya anakubalika sana Tanzania?

Ni msanii gani wa Kenya anakubalika sana Tanzania?

Wewe una matatizo kichwani,sio bure.

Sasa hao wasanii wenu hata nyinyi wenyewe mmewazira unataka nani ajishughulishe nao??msanii anatoa video miezi sita ina views 30k!!!sisi huku tunasikiliza wasouth,wanigeria,wakongo,mpaka wakorea wanapata umaarufu sana katika movie bongo.Bongo imebadikika siku hizi hutoboi bila kuwa serious.

Sasa wakenya wenu hao nikiwatizama sioni cha maana wanafanya.
Eti wakorea [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nazungumza kuhusu ninachokijua, ni ngumu sana kumkuta Mtanzania anaskliza wimbo wowote nje ya Bongo flava, hili nimeliona sana kwenu na hiyo nchi yenu nimeitembea zaidi ya wengi wenu humu, nimekatiza mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya hivyo napafahamu vizuri sana.
Yaan ukute Mtanzania amekaa anaskliza wimbo usio Bongo flava, utatembea sana, ni wachache labda waliobahatika kutoka na kuishi nje ya nchi na kurudi, ila wengine wote mumefungiwa ndani ya zizi moja, athari za ujamaa hizo, inalemaza mtu kiakili kwamba hauwezi kuwaza nje ya ulichoelekezwa.
Leo hii Bongo flava imeanza kubadilika na kuiga mitindo ya Kinijeria na ndio maana unakuta wengine wenu mumeanza kuwakubali hao Wanaijeria.
Hiyo point yako haina mashiko,,mbona muziki wa Nigeria unapigwa mpaka kwenye vilabu vya pombe za kienyeji huko Vijijini pamoja na kwamba watu hawaelewi kiingereza?,,mbona nyimbo za injili za wanamuziki wa Kenya zinapigwa sana Bongo

Kwenye hiyo sekta hamna cha kujitetea,,kajipangeni tena mrudi na majibu mazuri
 
Hiyo point yako haina mashiko,,mbona muziki wa Nigeria unapigwa mpaka kwenye vilabu vya pombe za kienyeji huko Vijijini pamoja na kwamba watu hawaelewi kiingereza?,,mbona nyimbo za injili za wanamuziki wa Kenya zinapigwa sana Bongo

Kwenye hiyo sekta hamna cha kujitetea,,kajipangeni tena mrudi na majibu mazuri

Miziki kuchezwa kwenye vilabu sio issue, maana nimecheza sana disco kwenye vilabu vyenu na kawaida DJ huchezesha wimbo wowote na tunaruka tu, lakini nachokisema japo mtabishia hadi kuzimu ila mwenyewe nimejionea kwa macho yangu sitegemei kuambiwa, ni vigumu sana umkute Mtanzania amenunua CD anacheza wimbo usio wa Bongo flava, nyie hamna mtindo mwengine wowote nje ya huo mmoja.

Mara nyingi kwenye laptop yangu nilikua naona kwamba nikiwa na Watanzania halafu niweke nyimbo za kimataifa wanakereka japo kimya kimya, hadi pale nitaweka Bongo akina Diamond ndio unaona kila mtu anachangamka, nchi yenu diversity haipo kabsa, mkiingizwa kwenye zizi moja mnajazana humo, hakuna anayeweza kunyanyua kichwa na kuona chochote kingine nje.
 
Shida ni hela pia kusema ukweli Tanzania pande ya hela wapo chini sana kuweza kuwahost wasanii wa Kenya lakini inakuwa ni kinyume na hapa Kenya Jinsi wabongo wengi wamenufaika kwa uwepo wa hela kwa wanakenya. As a matter of fact for any Tanzanian Musician to make it ama akubalike duniani lazima aingie Kenya aweze kupitishiwa kwa moto kama vile dhahabu hupitishiwa hadi ikakubalika.
Naona unajitahidi kuremba mwandiko.
 
Miziki kuchezwa kwenye vilabu sio issue, maana nimecheza sana disco kwenye vilabu vyenu na kawaida DJ huchezesha wimbo wowote na tunaruka tu, lakini nachokisema japo mtabishia hadi kuzimu ila mwenyewe nimejionea kwa macho yangu sitegemei kuambiwa, ni vigumu sana umkute Mtanzania amenunua CD anacheza wimbo usio wa Bongo flava, nyie hamna mtindo mwengine wowote nje ya huo mmoja.

Mara nyingi kwenye laptop yangu nilikua naona kwamba nikiwa na Watanzania halafu niweke nyimbo za kimataifa wanakereka japo kimya kimya, hadi pale nitaweka Bongo akina Diamond ndio unaona kila mtu anachangamka, nchi yenu diversity haipo kabsa, mkiingizwa kwenye zizi moja mnajazana humo, hakuna anayeweza kunyanyua kichwa na kuona chochote kingine nje.

Wewe unandika hisia zako tu.hamna utafiti makini umefanya katika hilo.

Ungejua kwamba wabongo tunapenda mziki mzuri,regad lugha au rangi,tunaruka na kusikiliza tu.though hatunaga shobo za moja kwa moja na wasanii wa nje.na hivi unaona sababu ni wazi music industry ya bongo sasa hivi imekua,ni ngumu sana kupenya humu msanii mpya tokea nje.tunawajua wale ambao tayari walikwishakupata majina kitambo.

Ndio maana humu unasikia wakitajwa watu kama kina nonini,jua kali,nyashiski,jaguar,wahu etc.
 
Wewe unandika hisia zako tu.hamna utafiti makini umefanya katika hilo.

Ungejua kwamba wabongo tunapenda mziki mzuri,regad lugha au rangi,tunaruka na kusikiliza tu.though hatunaga shobo za moja kwa moja na wasanii wa nje.na hivi unaona sababu ni wazi music industry ya bongo sasa hivi imekua,ni ngumu sana kupenya humu msanii mpya tokea nje.tunawajua wale ambao tayari walikwishakupata majina kitambo.

Ndio maana humu unasikia wakitajwa watu kama kina nonini,jua kali,nyashiski,jaguar,wahu etc.

Sijazungumzia mambo ya lugha, naongea kuhusu mtindo mmoja yaani hata humo Tanzania aibuke msanii aimbe kwa Kiswahili lakini mtindo ambao sio Bongo flava, ataishia kuskliza nyimbo zake mwenyewe na mkewe. Halafu pia kwenu huwa mumegawanyika kwenye timu mbili hata ndani ya hiyo Bongo flava, kuna Mondi na Kiba, wengine wote ni wasindikizaji tu, yaani naifahamu Bongo vizuri sana, hata kwenye michezo hamna diversity, ni mpira tu na wenyewe timu mbili Yanga na Simba, zingine zote zinasindikiza tu.
Ndio athari za ujamaa, huwa unalemaza mtu akili kiasi kwamba hana uwezo wa kutumia akili zake, lazima afuate mkumbo na ndio kipindi fulani hata Kikwete aliwahi kuwaomba muwe mnajiongeza sio kupelekeshwa pelekeshwa, angalia hata kwenye siasa, chama kimoja tangu mzungu awaachie nchi.
 
Back
Top Bottom