Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Eccles 9:11

Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Romans 8:28
And we know that all things work together for good to those who love God.......
 
Mithali 3:1 Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.

Mithali 3:2 Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.

Mithali 3:3 Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

Mithali 3:4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu

Mithali 3:5 Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe..

Mithali 3:6 Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.

Amina.
 
Muhimu sana kama wewe ni Mkristo ujue kwamba lengo la Biblia kuwepo kwa toleo la lugha tofauti tofauti ni ili kila atakaeisoma aielewe kiurahisi kwa lugha anayoielewa na kutafakari kitu akiwa amekielewa Biblia siyo kitabu cha siri au cha uganga kwamba isomwe huku msomaji akifungua codes

Na tujue huwa hakipungui kitu neno na maana inabaki vile vile muhimu ni mimi ninaesoma naelewa?mfano huo mstari uliopandishwa hapo kuna eneo ukisomwa wasikilizaji wanabaki njia panda same to unaoujua wewe ukisomwa watu hawauelewi.
UJumbe wowote wa maneno huwa unabadilika maana pale ambapo maneno halisi yakabadilishwa kwa namna moja au nyengine na kutiwa mengine .

Sasa kuna haja gani ya kubadikisha maana ya maneno kutoka kwenye uhalisia wake? Au haujui lugha huwa zinazidiana maneno na matamshi? Kitu ambacho kinapelekea neno kuzidi kuhama zaidi mwisho wa siku tunabaki na kitu ambacho ni tofauti na cha mwanzo .

Kuelewa namaanisha nini hebu jaribu kupitia mfano wa "THE SHIP OF THESEUS".

Na umesema biblia si kitabu cha siri au cha uganga kwamba hakiitaji kusoma huku tunafungua codes. sasa kwanini inahitajika kuwa na roho mtakatifu ili kulielewa neno?
 
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
Ufunuo 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

halafu namalizia na;

Luka 10:19 Tazama, nimewapa Mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

nikitumia kwa moyo na Imani, mashetani, majini, na shida huwa zinayeyuka.
 
Back
Top Bottom