Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Isaya 41:10-13
Screenshot_20231006_174022_Swahili Bible Offline.jpg
 
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
Isaya 41:10
[10]usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
 
Ayubu 2:10
[10]Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Na Muhubiri 3
1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;

3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Imeshiba sana hii na imekaa vizuri,shukrani kwa neno zuri!
 
Toleo gani hili linabadili neno tofauti na lilivyo kwenye matoleo mengine?
Muhimu sana kama wewe ni Mkristo ujue kwamba lengo la Biblia kuwepo kwa toleo la lugha tofauti tofauti ni ili kila atakaeisoma aielewe kiurahisi kwa lugha anayoielewa na kutafakari kitu akiwa amekielewa Biblia siyo kitabu cha siri au cha uganga kwamba isomwe huku msomaji akifungua codes

Na tujue huwa hakipungui kitu neno na maana inabaki vile vile muhimu ni mimi ninaesoma naelewa?mfano huo mstari uliopandishwa hapo kuna eneo ukisomwa wasikilizaji wanabaki njia panda same to unaoujua wewe ukisomwa watu hawauelewi.
 
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
Bwana ni mchungaji wamaisha yangu sitapungukiwa na kitu
 
Mithali 3:1 Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.

Mithali 3:2 Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.

Mithali 3:3 Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

Mithali 3:4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu

Mithali 3:5 Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe..

Mithali 3:6 Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.
 
Back
Top Bottom