Ni muda muafaka kwa sasa kufunga mipaka janga la njaa linakuja kwa kasi

Ni muda muafaka kwa sasa kufunga mipaka janga la njaa linakuja kwa kasi

Kama kweli nyie niwazalendo kwann msinunue kwabei nzuri kuliko wakenya ili mazao yabaki hapapa tanzania.
Bado tunazungumzia suala lile lile mana nikishindana na mkenya nami nitanunua kwa Bei ya juu nikiuza kwenye soko la ndani bado nitauza kwa bei ya juu na kuwaumiza wengine.
 
Watu wakila wakashiba amani inakuwepo. Ila ukiruhusu taifa lako liwe na njaa amani hutoweka kila mahali na ikizidi taifa huangamia. Bora mfumuko wa bei uwepo mana ni janga la dunia ila njaa njaaa sijui.
Baada ya kushauri tuongeze uzalishaji ja kilimo Cha umwagiliaji pamoja na mazao mbadala kama mihogo wewe unashauri tufunge mipaka ili mkulima apate hasara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi silimi ila nanunua mazao, wakulima wanauza mazao kwa fujo na wakenya wamekuja kulangua mazao ya chakula tani kwa tani kwa dau la kutamanisha tofauti na nyuma, kweli wamepata hela Ila wanauza hadi wanasahau kuwa kuna kesho na hali ya hewa haitabiriki.
Bora umeliona hilo kiongozi. Huku nilipo, wakenya wanakuja mpaka mashambani kununua mpunga. Hii ni hatari sana. Kwanza wanaua ajira za vijana waliojiajiri kama wanunuzi wa kati yaani antoa mpunga shambani, anakoboa na kupeleka mchele sokoni. Pili wanaua viwanda vyetu. Tatu, hiyo pesa wanayonunulia huku ni ndogo sana kulinganisha na faida wanayoenda kupata huko kwao. Nne, wanabeba hadi pumba ambazo huku kwetu tunalishia mifugo na pia tunachomea tofali. Kwa kifupi, bila kufunga mipaka taifa litapigwa technical KO.
 
Nasikia njaa imehamia kaskazini-mashariki ya Uganda,,, sasa ni Kenya,Somalia,Ethiopia na Uganda,,,Mungu atulin

Nasikia njaa imehamia kaskazini-mashariki ya Uganda,,, sasa ni Kenya,Somalia,Ethiopia na Uganda,,,Mungu atulinde!
Ni kweli, Mungu atuepushie tu janga hili na viongozi wawe na busara.
 
Mimi silimi ila nanunua mazao, wakulima wanauza mazao kwa fujo na wakenya wamekuja kulangua mazao ya chakula tani kwa tani kwa dau la kutamanisha tofauti na nyuma, kweli wamepata hela Ila wanauza hadi wanasahau kuwa kuna kesho na hali ya hewa haitabiriki.
Akipata njaa ndo ataikumbuka kesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya kushauri tuongeze uzalishaji ja kilimo Cha umwagiliaji pamoja na mazao mbadala kama mihogo wewe unashauri tufunge mipaka ili mkulima apate hasara

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaaa irrigation scheme hizo za kulisha nchi nzima ziko wapi? Hiyo ni sera ya muda mrefu tuangalie kwanza hali tuliyonayo kwa Sasa ili tujinasue. Utaipanda miogo kiangazi hiki?
 
Bora umeliona hilo kiongozi. Huku nilipo, wakenya wanakuja mpaka mashambani kununua mpunga. Hii ni hatari sana. Kwanza wanaua ajira za vijana waliojiajiri kama wanunuzi wa kati yaani antoa mpunga shambani, anakoboa na kupeleka mchele sokoni. Pili wanaua viwanda vyetu. Tatu, hiyo pesa wanayonunulia huku ni ndogo sana kulinganisha na faida wanayoenda kupata huko kwao. Nne, wanabeba hadi pumba ambazo huku kwetu tunalishia mifugo na pia tunachomea tofali. Kwa kifupi, bila kufunga mipaka taifa litapigwa technical KO.
Sijui nani anaruhusu upuuzi huu, inakuwaje wakenya wanaruhusiwa kwenda kununua mazao mashambani badala ya kusubiri yaletwe kwenye minada? nchi ina watu wa hovyo sana. Yakitokea ya Sri lanka wao wanawahi usafiri wa ndege.
 
Kama kweli nyie niwazalendo kwann msinunue kwabei nzuri kuliko wakenya ili mazao yabaki hapapa tanzania.

Bora umeliona hilo kiongozi. Huku nilipo, wakenya wanakuja mpaka mashambani kununua mpunga. Hii ni hatari sana. Kwanza wanaua ajira za vijana waliojiajiri kama wanunuzi wa kati yaani antoa mpunga shambani, anakoboa na kupeleka mchele sokoni. Pili wanaua viwanda vyetu. Tatu, hiyo pesa wanayonunulia huku ni ndogo sana kulinganisha na faida wanayoenda kupata huko kwao. Nne, wanabeba hadi pumba ambazo huku kwetu tunalishia mifugo na pia tunachomea tofali. Kwa kifupi, bila kufunga mipaka taifa litapigwa technical KO.


Hapana hapana

Haiwezekani nafuu iwepo kwa gharama ya jasho la mkulima
 
Sijui nani anaruhusu upuuzi huu, inakuwaje wakenya wanaruhusiwa kwenda kununua mazao mashambani badala ya kusubiri yaletwe kwenye minada? nchi ina watu wa hovyo sana. Yakitokea ya Sri lanka wao wanawahi usafiri wa ndege.
Waswahili wana msemo wao usemao damu ni nzito kuliko maji. Hata Yusufu aliwaokoa ndugu zake kwa namna hiyo hiyo.
 
Watu wakila wakashiba amani inakuwepo. Ila ukiruhusu taifa lako liwe na njaa amani hutoweka kila mahali na ikizidi taifa huangamia. Bora mfumuko wa bei uwepo mana ni janga la dunia ila njaa njaaa sijui.
Yaani mtu alime halafu umpangie bei na sehemu ya kuuza?! Wewe mbona hukukima ili uepukane na njaa?
 
Yaani mtu alime halafu umpangie bei na sehemu ya kuuza?! Wewe mbona hukukima ili uepukane na njaa?
Ulishaona nchi gani ambayo kila mtu ni mkulima, lazima serikali iweke control kwenye kila eneo vinginevyo katafute nchi yako utakayojifanyia mambo unavyotaka.
 
Gunia la mahindi litanunuliwa 200K ikiwa huyu mama (slow learner) hatapata mtu wa kumsanua.

Yani hii ni july wakati wa mavuno ila vyakula bado ni bei ghali, gunia la mahindi kwasasa ni 120K.
Kwa hiyo unataka wakulima wauze mahindi elfu 20 kwa gunia? Acheni upumbavu na kuwa na akili mgando. Kama unaona wakulima wanafaidika na wewe nenda kalime. Acha wivu wa kishoga. Shoga mwenzako anagongwa chumba cha pili na ww unajamba.
 
Kuna mahala nilikuwa naongea na jamaa anasema sembe kilo 5 imefika elfu tisa kwa hapa Dar, na hii ni July kipindi cha mavuno. Majuzi hapa niliona sabuni ya kuogea ya Protex ambayo nilikuwa nainunua kwa 2500 baadaye 2800 imeshafika 3500. Hii kasi ya kupanda kwa vitu muhimu kwa matumizi ya watu linaenda kuwa janga kubwa sana.
Sio linaenda limeshaenda.........hio huitwa "Inflation"....Jana kwa U.S imefika hadi 9.1%,which is 40 years high,....sembuse kwa TZ tunaimport bidhaa zaidi ya 90%.
Mfano kwa U.S,foods commodities inflation ni 12.5%,wakati kwenye energy na fuel ni 100%.
Hii kwa nchi kama Tanzania lazima ilete impact kubwa sana,sababu miundombinu ni hafifu mno,hii ikamaanisha energy consume ya fuel ni kubwa zaidi,lakini matokeo inayotatoa ni hafifu
 
Vichwa Maji wa Lumumba hawawezi kukuelewa.

Njaa inayokuja, tutatafutana sana ,waacha waendelee kufungua nchi .
 
Huku ni kwa wakulima lakini mahindi debe nanunua 16000.

Wakati nilikua nanunua 5000 na ikifika 7000 unaona bei kubwa sana lakini sasa imepanda ×3.
Gunia la mahindi litanunuliwa 200K ikiwa huyu mama (slow learner) hatapata mtu wa kumsanua.

Yani hii ni july wakati wa mavuno ila vyakula bado ni bei ghali, gunia la mahindi kwasasa ni 120K.
 
bora wewe umeliona hili

huku kanda ya kaskazini pamejaa magari ya wa kenya,, yanavusha mahindi nq maharage si mchezo

hlf kilo ya unga ndo tunanunua 1700..

Mungu mwenyewe ndo anajua tunapopelekwa
 
Ulishaona nchi gani ambayo kila mtu ni mkulima, lazima serikali iweke control kwenye kila eneo vinginevyo katafute nchi yako utakayojifanyia mambo unavyotaka.
Sawa, ila ni kwanini na wewe hukua miongoni mwa waliolima
Ili uepukane na njaa? Yaani wenzako wapigike na jua kali mashambani, wewe ukae mjini unajipodoa na kupuliza pafyumu halafu naada ya mavuno ndio uanze kulia njaa?
 
Mimi silimi ila nanunua mazao, wakulima wanauza mazao kwa fujo na wakenya wamekuja kulangua mazao ya chakula tani kwa tani kwa dau la kutamanisha tofauti na nyuma, kweli wamepata hela Ila wanauza hadi wanasahau kuwa kuna kesho na hali ya hewa haitabiriki.
Kumbe hapa ishu ni kuongea na wananchi wetu kutunza chakula.Binafsi Mimi ni mkulima wa mpunga.mwaka Jana tulivuna Kwa combining harvester ef 80,000 Kwa Heka ila mwaka huu ni 120,000 natarajia kuvuna next week hivyo ntauza nusu ya mavuno yanisaidie gharama za uvunaji
 
Watu wakila wakashiba amani inakuwepo. Ila ukiruhusu taifa lako liwe na njaa amani hutoweka kila mahali na ikizidi taifa huangamia. Bora mfumuko wa bei uwepo mana ni janga la dunia ila njaa njaaa sijui.
Daah! Mkuu kumbe na wewe unafikiria kama mimi
 
Back
Top Bottom