Ni muda muafaka sasa TRA mtoke hadharani mtuambie hayo mabango yenye picha ya Rais nchi nzima nani anayalipia na yanaingiza kiasi gani

Ni muda muafaka sasa TRA mtoke hadharani mtuambie hayo mabango yenye picha ya Rais nchi nzima nani anayalipia na yanaingiza kiasi gani

Nilikua nadhani ni kwenye majiji makubwa tu ila tuwe wakweli picha ya rais Samia ipo kwenye mabango karibu nchi nzima tena sehemu karibu zote potential kibiashara

Kuna mahali nilikua na kakibanda tena ndanindani sio hata main road, njia Haina hata lami walikuja TRA wakanipigia hesabu laki 3 kwa mwaka tukashindwana ikabidi nilitoe lile bango, sasa TRA mje mtueleze hayo mabango nchi nzima nani analipia kama ni chama, serikali, au watu binafsi na yanaingiza pesa kiasi Gani?
Samahani, nimeshindwa kuelewa mkuu 'Mr mutuu'!

Ulikuwa na "kakibanda" uchochoroni. Hapa nimeelewa kuwa ulikuwa na kibiashara chako.

"TRA wakakupigia hesabu laki 3 kwa mwaka"- nimeelewa kwamba hiyo laki tatu ilikuwa kodi uliyopaswa kulipia hiyo biashara yako kwa mwaka.

"ikabidi nilitoe lile bango" - hapa ndipo nilipochanganyikiwa hasa. Hilo bango ndilo TRA walilolikadiria laki 3 kwa mwaka?

Mwisho. Nani aliyekuwekea/kupa hilo bango; na ulipoliondoa uliliwasilisha wapi?
 
nadhani yeyote yule yuko huru kuweka mabango popote nchini ikiwa anaona inafaa, na ikiwa atapata idhini ya mamlaka husika kwenye eneo husika....

hakuna bango maalumu popote nchi , lisilolipiwa wala eti halina idhini ya mamlaka husika, labda yale ya waganga wa jadi ya kurudisha mpenz aliepotea 🐒
Kwa hiyo mabango ya rais yanalipiwa, na nani na kwa kiasi gani. Hii pesa inatoka mfuko gani?
 
Samahani, nimeshindwa kuelewa mkuu 'Mr mutuu'!

Ulikuwa na "kakibanda" uchochoroni. Hapa nimeelewa kuwa ulikuwa na kibiashara chako.

"TRA wakakupigia hesabu laki 3 kwa mwaka"- nimeelewa kwamba hiyo laki tatu ilikuwa kodi uliyopaswa kulipia hiyo biashara yako kwa mwaka.

"ikabidi nilitoe lile bango" - hapa ndipo nilipochanganyikiwa hasa. Hilo bango ndilo TRA walilolikadiria laki 3 kwa mwaka?

Mwisho. Nani aliyekuwekea/kupa hilo bango; na ulipoliondoa uliliwasilisha wapi?
Kodi ni ya bango tu, achilia mbali biashara, wanapima size ya bango kwa upana na urefu afu wanakupa makadirio
 
Mabango ya kuzuga tu lakini wamepanga kuiba Kura.
 
Nilikua nadhani ni kwenye majiji makubwa tu ila tuwe wakweli picha ya rais Samia ipo kwenye mabango karibu nchi nzima tena sehemu karibu zote potential kibiashara

Kuna mahali nilikua na kakibanda tena ndanindani sio hata main road, njia Haina hata lami walikuja TRA wakanipigia hesabu laki 3 kwa mwaka tukashindwana ikabidi nilitoe lile bango, sasa TRA mje mtueleze hayo mabango nchi nzima nani analipia kama ni chama, serikali, au watu binafsi na yanaingiza pesa kiasi Gani?
Rostam Azizi kasambaza haya mabango
 
Kodi ni ya bango tu, achilia mbali biashara, wanapima size ya bango kwa upana na urefu afu wanakupa makadirio
Ahsante. Sasa nime elewa.
Ila nina swali, kwa vile sina uzoefu kabisa na maswala ya aina hii.
Unapo pewa bango, na kuliweka hapo mahala pako, unapewa chochote kuhusiana na bango hilo; au ni kama kivutio tu cha biashara yako; au kuunga mkono/shabiki tu wa huyo mwenye bango lake?
Siyo muhimu ujibu hili kama linakupotezea muda. Sehemu muhimu ni hiyo uliyo nipa elimu juu yake hapo juu.
 
Ahsante. Sasa nime elewa.
Ila nina swali, kwa vile sina uzoefu kabisa na maswala ya aina hii.
Unapo pewa bango, na kuliweka hapo mahala pako, unapewa chochote kuhusiana na bango hilo; au ni kama kivutio tu cha biashara yako; au kuunga mkono/shabiki tu wa huyo mwenye bango lake?
Siyo muhimu ujibu hili kama linakupotezea muda. Sehemu muhimu ni hiyo uliyo nipa elimu juu yake hapo juu.
Bango hupewi, unaweka mwenyewe kujulisha watu uwepo wa Hio biashara yako
 
Zaidi watakuambia ni maagizo toka juu.Baadhi ya nchi za Kiafrika na Asia ni Sawa na sehemu za kutolea haja kubwa,kauli hii ya Donald Trump ipo Sawa Sawa kabisa.
 
Watanzania tushakua kama makondoo, mtu nauliza swali basic tu mtu anajibu uchochezi, tumerudi enzi za utumwa sasa huku tukitawaliwa na weusi wenzetu
Baada ya mataifa mengi ya kiafrika kupata uhuru miaka 1960s,Mengi yalijikuta yameingia kwenye utumwa mpya,tena mbaya zaidi kuliko ule wa wakoloni.
 
Nilikua nadhani ni kwenye majiji makubwa tu ila tuwe wakweli picha ya rais Samia ipo kwenye mabango karibu nchi nzima tena sehemu karibu zote potential kibiashara

Kuna mahali nilikua na kakibanda tena ndanindani sio hata main road, njia Haina hata lami walikuja TRA wakanipigia hesabu laki 3 kwa mwaka tukashindwana ikabidi nilitoe lile bango, sasa TRA mje mtueleze hayo mabango nchi nzima nani analipia kama ni chama, serikali, au watu binafsi na yanaingiza pesa kiasi Gani?
Mkuki kwa nguruwe ee. Mbona jpm alisambaza mabango nchi nzima kwama yeye ndo rais aliyetumw na mungu. Unajua tanzania kwa mara ya kwanza tuliishi na shetani bila kujua
 
Mkuki kwa nguruwe ee. Mbona jpm alisambaza mabango nchi nzima kwama yeye ndo rais aliyetumw na mungu. Unajua tanzania kwa mara ya kwanza tuliishi na shetani bila kujua
Jpm nae alipokua anakosea tulihoji vile vile, kwa kua jpm aliharibu basi tumuache na huyu aharibu? Akija mwingine nae vile vile?
 
Kuna jamaa ana bango aliliweka kama week hivi hao wakaja, hesabu waliyompigia alilitoa hapo hapo.
 
Main road huwezi kutoboa, mi kwangu vichochoroni tu nilipigwa laki 3
Ni main road jamaa alisema potelea pote asipouza basi ila hawezi toa hela yote hiyo kulipia bango heri aijazie hadi bidhaa 😃
 
Ni main road jamaa alisema potelea pote asipouza basi ila hawezi toa hela yote hiyo kulipia bango heri aijazie hadi bidhaa 😃
Main road bango likiwa kubwa kidogo tu tunaongelea millions sio malaki tena
 
Back
Top Bottom