Ni muda sasa sijawahi kumbuka ndoto yoyote niliyoota

Vyema sana mkuu, nitajitahidi nisiamke kwa mawenge, yani nitulie kwanza kabla ya kukurupuka. Hii hali ni ya muda mrefu sana, pia ni kweli sio ndoto zote zina maana ila ni muhimu kukumbuka japo kidogo tu
 
Tenga mda wa kufanya meditation kila siku angalau mara mbili, kwa mda usiopungua dakika 30 utakumbuka kila kitu .
Mediation niliwahi jaribu mkuu, tatzo eneo ninapo ishi kuna distraction kibao. Labda nitafute maeneo mengine yenye utulivu
 
Mediation niliwahi jaribu mkuu, tatzo eneo ninapo ishi kuna distraction kibao. Labda nitafute maeneo mengine yenye utulivu
Meditation ni maisha yako ya kila sku na kwa kila kitu unachokifanya ila ukiweza tenga mda utapata utulivu wa kufanya meditation kama maisha ya kila siku ,hautakiwi kujaribu fanya.
 
Ndoto ni za muhimu sana, ndio kioo chako cha kutazama mambo kwa upana. Ni RADA.

Ukiona hukumbuki ndoto zako ujue kuna tatizo dhahiri.

Lazima ukumbuke ndoto ili uone yanayojiri, vinginevyo utaumia.

Ni ama kuna "watu" wanafuta kumbukumbu za ndoto zako, au wanaufunga mwili wako.

Na hasa ukianza kuona "yasiyotakiwa", lazima WAFUTE kila kitu.
 
Mie naota halafu zinakua na maana kabisa, yani nnayoyaota yanatokea....

Nilishajifunza kitambo huwa sipuuzii ndoto zangu kabisa. Kuna siku niliota ugomvi yani kila nilichokiota kesho yake kilikua kama nilivoona ndotoni.

Ni kweli kuna watu mna vipawa navyo, kwetu mama huwa akiota aina flani ya ndoto lazma atuambie kuwa kuna msiba au kuna issue mbaya inakuja,

Mfano, mara zote sehemu aliyoiota watu wanakula na kunywa lazma msiba utokee. Hiki kitu kiilikuwa kinanishtua sana ila siku hizi nimeshazoea
 
Kuna ndoto zinazotokana na mambo yako ya kila siku na kuna ndoto zimebeba ujumbe au maono kwa ajili ya maisha yako.

Kutokukumbuka ndoto ni tatizo mkuu!
Kweli ni tatizo, najihisi kama nakosa kitu muhimu sana ambacho ni wajibu wa mwanadamu kukipata
 
Reactions: I M
Meditation ni maisha yako ya kila sku na kwa kila kitu unachokifanya ila ukiweza tenga mda utapata utulivu wa kufanya meditation kama maisha ya kila siku ,hautakiwi kujaribu fanya.
Sawa mkuu, nitajitahidi kufanya kadri ya uwezo wangu
 
Kuna pastor aliniambia, ukiona huoti au hukumbuki ndoto yoyote bhasi umeanza kufa kiroho. Kwa hiyo rudi kwenye sala na sadaka.
 
Aisee, sasa mbona mimi sina tatzo na mtu yeyote, sina ugomvi na mtu, sina maadui wa shari ninao wafahamu, nashindwa kuelewa kabisa yan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…