Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Status
Not open for further replies.
Neno udini ni silaha kubwa anayoitumia, pamoja na kwamba haujajionyesha kihivyo, hakuna mgawanyiko kihivyo, amekosa silaha za kutumia ili kuwapelekesha watz anasema kulikuwa na udini, nikiangalia kwa undani naona hakuna udini wowote uliokuwa unatumika..sasa nashindwa kumwelewa.
 
Nachojua mimi ikijulikana chama kina mlengo wa kidini inatakiwa kifutwe haraka sana! Bila hata ya kujiuliza na kama kunachama kitafutwa kwa sababu hiyo nitafurahi sana haya maneno mnayosema ni chokochoko mwisho wake mbaya! Mnataka nini sasa! Acheni haya mambo bwana!
 
cuf ya mwambao wa pwani na inayosema haki sawa/ikimaanisha waislam hawajapewa haki, ndo chama cha kidini, kufutwe. pili ,ccm ni ya kidini pia tukienda kiundani.
 
Kama CCM itashindwa kuona na kusikia ukweli huu ya kuwa main actors na successors wao hawataweza shindana na wale waliopo CHADEMA basi watakuwa wanamacho lakini hawaoni na masikio lakini yasiyosikia. Ukiangalia hata tafsiri ya results za uchaguzi inaonyesha kuwa behind CHADEMA kuna nguvu ya waelewa (Literate) ambao kutokana na history ya Siasa za zamani wameshindwa kujionyesha waziwazi so they play indirectly. Na in the front line CHADEMA ina vijana wasomi wenye confidance yakutosha na wenye uwezo wakujenga hoja ambayo itawafanya CCM wajikute mara zote wana resort kwenye kutumia stick measures (Kwasababu ya kuwa proveked) ambayo itasababisha public i sympathize na CHADEMA. Mwisho wa siku CCM itaji identify kama chama chenye kulazimisha mambo na hivyo kukosa public support ya kutosha hivyo kuwa weakened kiasi ambacho....well niishie hapo. Mwenye macho na atazame na mwenye sikio asikie....This is 2010. CCM angalien succession plan yenu!

tujitahidi sana kuwaelimisha wa tz kwani mtaji wa ccm ni 'ujinga wa watanzania' na siku wakielimika ccm watafunga biashara zao. Big up2 CHADEMA
 
Ni jambo la kusikitisha sana kuona kiongozi mkuu wa nchi anaeneza propaganda zisizo na tija kwa taifa. Kutokana na wimbo huu wa udini ambao kikwete amekua akiuimba kila anapopata nafasi ya kuongea mbele ya hadhara watu wengi sasa wameanza kuamini kwamba tanzania kuna udini. Huu ni uchochezi wa hali ya juu tena unaoenezwa mkuu wa nchi. HII NI HATARI KUBWA HAKIKA RAIS ANALIPELEKA TAIFA PABAYA NAWAOMBA VIONGOZI WA DINI WAMKEMEE MARA MOJA!
 
Mimi binafsi nampongeza Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kwa hatua yake ya kukemea udini maana kweli upo.
Kama mnabisha angalieni: Kuna vyama vingine vimejaa watu wa dini moja tu na nafasi za juu zote zimeshikwa na watu wa dini hiyo hiyo tu!
Hata wakiambiwa wateue watu kwenye nafasi fulani basi watateua watu wa dini hiyo tu! Hata kama nafasi ni tatu, wote watakuwa ni wa dini hiyo tu! Kwa hili Watanzania wenzangu udini upo ila mimi ningekuwa na uwezo wa kumwuliza ningetaka kujua mtu hasa anayeendekeza huo udini ili nimjue. Ningemwomba rais wetu ambaye si mdini hata aniambie huo udini anao usema ni nani hasa ameupanda na kuupalilia!!

1. Kwa hoja hiyohiyo, ingetokea wanafunzi wakafaulu mtihani, uchaguzi wako utafuata nini: ushindi wa masomo au madhehebu ya dini wanayotoka ili kusioneshe ni wanafunzi wa dini fulani tu wamechaguliwa.
2. Ukianza kutumia namba kuonesha udini ina maana hutaishia kwa vyama vya siasa tu bali hata maeneo mengine: mfano, sehemu za kazi - je, ili uajiri mtu utaangalia nini: sifa au idadi ya watu kwenye madhehebu ya dini - mfano ukiajri Waislamu 2, lazima pia uajiri wasio amini dini yoyote 2, Wakristo 2, Wahindu 2, kutoka dini za asili 2 nk. Vilevile ukienda Pemba au Zanzibar na ukaamua kuchagua viongozi, utaangalia nini - kama kuna nafasi 20, je utafuata merits au Waislamu 5, Wakristo 5, Wahindu 5, Wasioamini katika dini 5 bila kuangalia sifa maana ukifuata sifa hazitafuata limit ya watu wanaotakiwa? Mfano, unaweza kupata watu wenye sifa nyingi zaidi kutoka dhehebu moja kuliko jingine au wataalamu kwenye dhehebu moja watazidi jingine pia. Hapa najaribu kuonesha jinsi namba sawa zinavyoweza kutupotosha kama hatutangalia vizuri.
 
Acha kuandika porojo na mambo ya kufikirika wewe. Huyo unayerejea kauli yake ndiye mdini namba moja. Suala la udini limejitokeza zaidi chini ya uongozi wake. Kama huna cha kuandika pumzika.
 
Ni jambo la kusikitisha sana kuona kiongozi mkuu wa nchi anaeneza propaganda zisizo na tija kwa taifa. Kutokana na wimbo huu wa udini ambao kikwete amekua akiuimba kila anapopata nafasi ya kuongea mbele ya hadhara watu wengi sasa wameanza kuamini kwamba tanzania kuna udini. Huu ni uchochezi wa hali ya juu tena unaoenezwa mkuu wa nchi. HII NI HATARI KUBWA HAKIKA RAIS ANALIPELEKA TAIFA PABAYA NAWAOMBA VIONGOZI WA DINI WAMKEMEE MARA MOJA!
 
Ndugu Kituko umeongea vizuri sana. Ukweli ni kwamba JK anaiharibu CCM, anataka kuifanya ni ya kidini. CCM kama ilivyo CUF na CHADEMA na vyama vingine si vyama vya kidini. Na kikubwa ni kwamba wananchi wanafahamu hilo. Kipindi cha kampeni niliongea na Bwana mmoja huko mwanza, jimbo la Nyamagana, ambaye ni mwananchi wa kawaida kabisa. Ajira yake ni bodaboda, i.e kuendesha pikipiki kama chombo cha usafiri. Nilimuuliza kuhusu uchaguzi na mambo yanavyokwenda hapo Nyamagana, aliliongelewa swala la Udini.
Alisema hivi: "CCM wanasema CHADEMA ni wa dini. Wanadai CHADEMA ni ya wakristo. Baadhi ya mashehe wamefikia hatua ya kuongea hiki kitu msikitini. Lakini sisi hatukubali, chaguzi zilizopita CCM walisema CUF ni ya waislam, leo wanasema CHADEMA ni ya wakristu, shida yao kutugawa"
Haya ni maneno aliyosema mwananchi wa kawaida kabisa. Ambaye ni muislamu. Nikagundua kwamba silaha moja wapo ya CCM ya kuwagawa wananchi katika misingi ya udini imeshagundulika, na wala haitafanya kazi kwa watanzania wengi katika uchaguzi huu.
Ndo tuseme kwamba CCM haiitakii mema nchi hii kwa kila wakati kupandikiza chuki ya UDINI. Wameishiwa Sera wanataka kugawa wananchi, JK aanzishe udini halafu awaambie waandishi wa habari wamsaidie kuponya majera ya udini. Kama nchi itafikia udini wa kulaumiwa ni CCM. Mie ningewazhauri wadau tuing'oe CCM kabla hatujafikia huko.
 
Kwa nini huyu asibanwe aeleze huo udini ukoje? Tumemchoka na 'rhetorics' zake kuhusu udini. Kwa mtazamo wangu yeye ndiye anayeamsha hisia za udini. Tanzania yetu haina ujinga wa udini kwa sababu utakuta watu wa familia moja wengine wakristo na wengine waislamu na hakuna tatizo maisha yanaenda. Huyu anawaaga ndugu zake kuwa anaenda msikitini, na mwingine anaaga anakwenda kanisani na hakuna tatizo lolote. Huu udini anaousema Kikwete u wapi? Anaudhi sana.
 
Ni jambo la kusikitisha sana kuona kiongozi mkuu wa nchi anaeneza propaganda zisizo na tija kwa taifa. Kutokana na wimbo huu wa udini ambao kikwete amekua akiuimba kila anapopata nafasi ya kuongea mbele ya hadhara watu wengi sasa wameanza kuamini kwamba tanzania kuna udini. Huu ni uchochezi wa hali ya juu tena unaoenezwa mkuu wa nchi. HII NI HATARI KUBWA HAKIKA RAIS ANALIPELEKA TAIFA PABAYA NAWAOMBA VIONGOZI WA DINI WAMKEMEE MARA MOJA!
 
Unajua watanzania either wanapotoshwa kuhusu maana ya udini, au hawajui maana ya udini.
Mfano mtoa mada anaonekana hajui maana ya udini.
Udini sio chama flani kuwa na viongozi wengi wa dini moja bali ni kupeana uongozi kwa kuzingatia dini ya mtu na sio sifa ya mtu.
Sasa kama kipo chama kilichotoa nafasi kwa kuzingatia dini ya mtu na sio sifa zake basi kiwekwe hadharani na mifano hai itolewe.
Na sio kukariri tu chama flani kina udini.
 
Kikwete na kikundi chake ndani ya CCM wameamua kutumia udini kama tatizo ili kufunika mambo muhimu yenye utata katika nchi kwa sasa. Nchi ina matatizo ya kifisadi, utendaji mbovu wa serikali, maisha magumu kwa wananchi na mengine muhumu. Udini sio tatizo Tanzania, unatumika kugeuza upepo.

alikosa la kuongea bungeni tatizo jubwa hapa nchini ni utofauti mkubwa ya kimaisha kati ya wakuma+wafanyakazi(wenyenchi) na mafisadi(wakiwemo watendaji wake) ila yeye halioni hilo kwakua macho yake tayari yanamatongo tongo na ujungu wa ccm.Hawezi kuliona hili na kwakweli mtu huyu si msaada kwa nchi hii. Heli israeli ampumzishe
 
Mimi ninacho kiona nikwamba watu wengi wanajua nini nisiasa nakila aliye na nafasi yakuongea kwenye jamii akiongelea siasa wakati yupo kanisani ccm wanasema niudini!mfano ni askofu kakobe aliongea kanisani na akatoa mistari inayoelekeza watu wakamchague kiongozi lakini ccm waliibebea bango!!wakasahau misikitini nini kilichokuwa kikisemwa kila siku kwenye miadhara hadi kwenye sala za ijumaa!!

KakaKiiza, Kakobe hakusema chochote kuhusiana na uislam au Ukristo. Na JK sidhani kama anasema juu ya yale yaliyokuwa yanasemwa makanisani kwa kuwa hayakutaja lolote juu ya tofauti za dini. Hapa JK anachokiongelea ni yale yaliyoandikwa kwenye magazeti ambayo yaliweka wazi kabisa, msimamo wa waislam dhidi ya Slaa, na kumtukuza JK na Lipumba kama viongozi safi. Nafikiri ndiyo maana JK alivikemea vyombo vya habari. Na magazeti yaliyolikalia bango jambo hili ni Uhuru, Mtanzania, Al huuda na Al Nuur. Na ushahidi upo.
 
Jamani ndugu zangu kuna udini shauri yenu!! Ila ningeweza kumwuliza, ningemwulia nani mwazilishi wa hayo mambo mabaya?
 
Wanausalama wanapokaa kimya hata km Mkuu anapoteleza, au nao wamegawanyika?
 
Wanausalama wanapokaa kimya hata km Mkuu anapoteleza, au nao wamegawanyika?

Wamegawanyika kwa sana tu. Kama hawajagawanyika Dk Slaa anatoa wapi nyeti za Ikulu? Jibu ni rahisi hupewa na usalama.
 
Abraham Lincolin The father of Democracy alipata misukosuko ya hapa na pale ili kupata Democracy ya kweli, sio kazi rahisi kupata uhuru wa kweli, siku moja utafahamu ni nini kinaongelewa hapa, ni mapambano kuelekea Democracy ya kweli sio chenga chenga tunazoziona sasahivi,
nafikiri tunapaswa kuishi karne ya 21 na siyo kurudi nyuma tena. i thought you'll be the one to support! mapambazuko ndiyo hayo, endelea kufuatilia yanayotokea.

wajemeni mwee. Toka lini Lincoln akawa baba wa demokracia? Lincoln alikuwa Federalist na democracia aliikuta tayari.
 
Kwa nini huyu asibanwe aeleze huo udini ukoje? Tumemchoka na 'rhetorics' zake kuhusu udini. Kwa mtazamo wangu yeye ndiye anayeamsha hisia za udini. Tanzania yetu haina ujinga wa udini kwa sababu utakuta watu wa familia moja wengine wakristo na wengine waislamu na hakuna tatizo maisha yanaenda. Huyu anawaaga ndugu zake kuwa anaenda msikitini, na mwingine anaaga anakwenda kanisani na hakuna tatizo lolote. Huu udini anaousema Kikwete u wapi? Anaudhi sana.



Ni kweli kabisa JK abanwe aeleze udini anaousema uko wapi? ili watu wapime ni kweli au si kweli vinginevyo anapandikiza chuki kati ya waislamu na wakristo. Tanzania hatujawahi kuwa na tabia ya kuchagua viongozi kwa kufuata dini zao. Yeye aseme kuwa ameshindwa kuwa na jambo jipya hivyo kaamua kuhamishia kwenye dini,mfano mzuri uspika baada ya kuona mtazomo wa wananchi wengi ni kuunga mkono sita kama mpambanaji wa ufisadi wakaamua kumuengua kwa kisingizio cha mwaka wa wanawake. Huu ni unafiki mkubwa sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom