Ni nani huyu Waziri Rajab Salum, Katibu binafsi wa Rais Samia?

Ni nani huyu Waziri Rajab Salum, Katibu binafsi wa Rais Samia?

Kama ilivyokuwa kwa Nguza Samike katibu binafsi wa Rais Magufuli na sasa tuna Waziri Rajab Salum katibu binafsi wa Rais Samia.

Huyu ndiye mtendaji wa shughuli zote binafsi za Rais Samia katika masuala ya utawala na serikali.

Huyu ndiye mwandishi wa hotuba za Rais, hivyo Rais siku akipatia credit ziende kwa huyu mwamba na akiskosea pia ni hivyohivyo.

Kwasasa viongozi wengi hasa wabunge wamekuwa wakimpost huyu jamaa kupitia mitandao yao ya kijamii ili tu kuweka mazingira yao ya kisiasa vizuri.

Mwenye CV anaweza kuleta ili tunjue kwa undani.View attachment 2909032View attachment 2909033View attachment 2909034
Unataka msaidizi apate sifa za Rais? Ni wasaidizi wangapi wanafanya vizuri chini ya maboss wao na sifa anachukua boss? That is an administrative and leadership order. Short of that will just be chaos die to lack of order and disruption of the chain of command. Mwenye mamlaka ndio mwenye kuchukua credits na ndio mchukua lawama pia. Kuna wasaidizi kibao tunavurunda huku chini lkn lawama zote kwa Rais na wenzake katika Baraza la mawaziri.
 
Naambiwa ni jamaa Makini sana huyu . Ni jamaa anayeshirikiana na kila mtu hata wasio na umaarufu , tofauti na ilivyokuwa kipindi kile January Makamba akiwa muandishi wa JK.

Kwa sifa alizo nazo atakuwa ni wa kitengo tu huyu.

Kama unapitia hizi post basi endelea kuwa mtu wa watu bila kubagua maana Maisha ya kesho ni fumbo kubwa sana .
 
Anahusika

Kama ilivyokuwa kwa Nguza Samike katibu binafsi wa Rais Magufuli na sasa tuna Waziri Rajab Salum katibu binafsi wa Rais Samia.

Huyu ndiye mtendaji wa shughuli zote binafsi za Rais Samia katika masuala ya utawala na serikali.

Huyu ndiye mwandishi wa hotuba za Rais, hivyo Rais siku akipatia credit ziende kwa huyu mwamba na akiskosea pia ni hivyohivyo.

Kwasasa viongozi wengi hasa wabunge wamekuwa wakimpost huyu jamaa kupitia mitandao yao ya kijamii ili tu kuweka mazingira yao ya kisiasa vizuri.

Mwenye CV anaweza kuleta ili tunjue kwa undani.View attachment 2909032View attachment 2909033View attachment 2909034
Kuna tofauti Kati ya Katibu binafsi wa Rais na Katibu wa Rais Ikulu
Dah! Yeye anahusika na yapi Mh.
Huyo ni Katibu binafsi wa Rais, appointment za Rais ndo anapanga yeye, hauhusaini na hotuba wala kumpangia safari Rais... Nachelea kusema kuwa huyo sio Mtumishi wa Umma maana sio lazima awe Mtumishi wa umma , maana anaweza kumtoa popote, Chamani, Vyuoni, inategemea na Rais mwenyewe japo mara nyingi akishakuwa hapo ikulu lazime aajiriwe. QqHuyo ndo huwa anasoma meseji zetu humu na kumwambia Ma Samia yanayoendelea, huyo ndo huwa anamwambia mama Kuna mtu ameomba cherehani mpatie , huyo ndo huwa anamwambia mama tukifika hospital beba mtoto au Mpe pole Mzee flani , wananchi wanapenda kusikia ukisema hivi au vile ..Kwa machache nayoyajua
Wajuzi wapo humu watakuambia
 
Huyo ni Katibu binafsi wa Rais haihusiki kumpangia Safari.
Inawezekana kwenye protocol za kiserikali, but huyu jamaa is the most powerful person hapa TZ ukiachana na Rais mwenyewe. Acha mchezo na mtu anayeaminiwa na Rais.

Google mtu mmoja anaitwa Farouk Kibet, ndio PA wa Ruto. Huyo jamaa akisema "Hautamuona Ruto", ni uhakika Hautamuona.
 
Ni mtu ambaye hajikwezi .. ukikutana naye kwa mara ya kwanza huwezi muona kama ni mtu mwenye cheo kikubwa labda utambulishwe ukikaa naye kuzungumza naye utapata madini sana ..

Tofauti na aina nyingine ya binadamu akiwa kapata access ya kuwa na cheo kama chake mtajua hamjui..
 
Naona huyo Lucas Mwamshamba hajamjua akimjuuua tu tumekwisha ,atakua anamuandikia uzi kila akinywa maji
Mwashamba kwa sasa kaajirawa na makonda ili kumsifia muda wote ktk mitandao!
Mchana na usiku ni kumsifia makonda hadi kubadilisha ID ili tu ionekane watu wengi wanamsifia makonda kumbe ni yeye anafanya yote! Njaa kitu mbaya sana! 🤣 🤣
 
Tanzania imelaaniwa, hapo amevaa kofia yenye picha ya Rais na kuonyesha anamkubali kumbe kafuata pesa
Na ukiona kiongozi mkuu anatapeliwa kwa style hii (kama ilivyokuwa kwa Mobutu) ujue hakuna kitu hapo!
Yaani hao wanakufanyia hivyo kwa vile tayari wanakudharau nawe unachekelea kudhani uko level moja na Mungu.
Haya ndio yale ya JK alivyoishia kufedheheshwa msibani Monduli akajikuta kajikunyata kama kuku mwenye kideri

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Na ukiona kiongozi mkuu anatapeliwa kwa style hii (kama ilivyokuwa kwa Mobutu) ujue hakuna kitu hapo!
Yaani hao wanakufanyia hivyo kwa vile tayari wanakudharau nawe unachekelea kudhani uko level moja na Mungu.
Haya ndio yale ya JK alivyoishia kufedheheshwa msibani Monduli akajikuta kajikunyata kama kuku mwenye kideri

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Tangu aondoke Mkapa nchi haijapata kiongozi wa maana
 
Back
Top Bottom