Ni nini hatma ya Pesa zetu zilizotafunwa na zinazotafunwa na Hawa wabunge 19? Watanzania tumefanywa wajinga kiasi hiki?

Sawa
 
CHADEMA utawalaumu bure. Walijitahidi kuondoa hao akina Mzee Halima tangu mwanzo, Ndugai akawakingia kifua. Sasa Tulia anaendeleza!

Tatizo ni kuwa nchi imegeuzwa shamba la bibi', hakuna mlinzi, wanavuna tuu!

Mwigulu Nchemba njoo usaidie kujibu kwa nini fedha za walipa Kodi maskini zinatafunwa kimasihara huku mmekodoa tu macho?!!
 
Usiilaumu CHADEMA.... Imefanya kinachostahili kufanyika na haina mawaa tena kwenye hilo na IMESHAMALIZANA NAO
Cha muhimu jiandae tu kisaikolojia kwakuwa hao watakuwa wabunge wa mbeleko mpaka 2025 kama mahakama nayo itatumika kisiasa

Kamati kuu ya Chadema ilifanya maamuzi 2020,
Kisha Baraza kuu limekuja kubariki 2022

Na hapo Baraza kuu lilikaa baada ya Mbowe kumalizana na Serikali ktk kesi yake, vingnevyo kama kesi ingeendelea kusomwa basi maamuzi ya hiki chama juu ya hawa wabunge yasingefanyika

Ndio maana baadhi ya watu wanasema hiki chama kinategemea mtu mmoja tu,,, MBOWE

Na mtoa hoja anailaumu chadema kwa delays
 
Reactions: RNA
Katiba ya CHADEMA tu hamuiwez kuifuata mtaiweza ya nchi mkishika dola?😁

Kama CHADEMA iliweza kubadili kipengele cha ukomo wa uongozi ktk katiba yake kitashindwa kubadili ktk katiba ya nchi kikishika dola?😁
Unajua nini wewe sister?
 
Hahaha Mwigulu ashawahi kuwa na majibu ya Kueleweka
 
Shida yako nini? Unaamini tukiwatoa kodi hazitakatwa? Mungepeleka mnaowataka tusingekatwa kodi au ndo zingeenda hela kihalali? Acha wapiganie nchi wamama hawa, waliwaongezea umaarufu CHADEMA bila malipo yoyote acha wajilipe kupitia umaarufu waliowaleteeni. 😀 hujui tu, kadri mnavyoifuatlia hii kesi ndo mnajiongezea umaarufu so msikate tamaa kujitangaza kupitia covid 19.
 
Wanakopakopa , na kukata tozo hovyo hovyo watanzania ili kulipa Mambo ya kipumbavu Kama haya. Nchi ina madeni makubwa, hali ya kuangaika lakini wapo watu wazima mliowapa dhamana na heshima wanafanya hovyo wakiona watanzania huwa wajinga ma leziafea. Mnafurahia kusifiwa,kupigiwa MAKOFI ya kinafiki
 
Kutawala Taifa lisilo na uchungu na mali zake za umma, lisilofikiri hata kufanya demonstrations kupinga lolote linalofanyika ndivyo sivyo ni rahisi mno, you rule the way you want, hata ukipindisha sheria na katiba wananchi wanasema "Hewalaa bwana mkubwaa.."

Viva Tanzaniaaa !!

Waacheni hao 19 wale pesa maana si za kwenu za mfukoni.
 
Shida ni kutolipwa kihalali
 
Je wanaweza kuwa wametafuna bilioni ngapi mpka sasa??
 
Tatizo wanaccm wanafikiri kuwang'ang'ania covid19 ni kuikomoa chadema, wanasahau kuwa chadema wameshamaliza sehemu yao. Tunaokomolewa ni sisi walipa kodi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…