Ni nini sababu na suluhisho kwa wachagga kuwa na meno yenye rangi ya manjano/kahawia?

Ni nini sababu na suluhisho kwa wachagga kuwa na meno yenye rangi ya manjano/kahawia?

Sababu kubwa ni uchafu.

Wachanga ni wachafu sana.

Huwa hawapigi mswaki.
Duh, hii kali sana wasio wachaka na wanaishi maeneo hayo na meno ni brown pia wachafu? Wooote wanaoishi maeneo mengine na meno siyo brown ni wasafi wooote?
 
Mkuu tatizo ni fluoride iliyo zidi kwenye maji tangu mtu akiwa tumboni mwa mamake (reffer embryology - teeth formation).kwa sababu ya wingi wa fluoride, itakuwa incorporated badala ya calcium, na kutengeneza fluoroxyapetite ambayo ni brown, badala ya hydroxyapatite ambayo ni nyeupe. Tatizo hilo halikomei kwenye meno tu bali na mifupa itayotengenezwa kipindi unapo kuwa exposed kwenye fluoride, meno na mifupa vilivyo athirika hubadilika rangi na huwa brittle. Tatizo la fluoride iliyo zidi si la wana Arusha tu bali na wale wa singida, tabora/Igunga, shinyanga /kishapu, meatu, Simiyu,Mbeya maeneo ya Mbalizi. Kuzuia tatizo hilo ni kuepuka matumizi ya maji yenye fluoride iliyo zidi tangu mimba ya week 5, kuondoa fluoride iliyo zidi kwenye maji (defluoridatio). Kwa walio athirika tayari kuna huduma za dental bleaching and veneering through dental services. Karibuni kwa maswali zaidi....
Nakushukuru kwa kujielekeza vilivyo Kwenye mada,
Je , Huduma ya kubrashiwa meno inapatikana wapi na kwa gharama gani?
 
Naungana na NN wengi wao ni wachafu balaa, nilikutana na demu wa chuo lkn ni majanga sijui kwa nini.

NB: sina conglicting interest juu ya hili ni exoerience niliyokutana nayo, na si wote
 
Nakushukuru kwa kujielekeza vilivyo Kwenye mada,
Je , Huduma ya kubrashiwa meno inapatikana wapi na kwa gharama gani?
Mkuu kwa hapa dar, bei zina range kuanzia elfu 30000-50000/=
 
Kuna harusi nilihudhuria mdada meno meupe anacheka na kutabasamu.
Nilipokuja kukutana nae siku ya nne, kidogo nikimbie, meno ka Lily wine.
Naomba kujua ni dawa gani alitumia siku ya harusi.
Unatuuliza sisi kwani tulikua nae siku ya harusi? Ungemuuliza siku ya nne uliokutana nae angekupa majibu
 
Si wachaga tu, hili tatizo nimeliona sana A town (rangi flani ya njano). Mwenyewe ni mwathirika kwa kiasi fulani. Machalii wengi waliokulia Kaloleni, Makao mapya, Sakina, Kijenge, Sanawari, tuna hili tatizo. Si uchafu, and it doesn't take away anything.

Binafsi, I get around pretty cool with my 'golden grills'. Not smiley perfect, but my smile score me excess.
Chalii angu hii thread imekaa ki-daslam sana

Mi pia ni muathirika kwa mbaaali but proudly
 
Mkuu tatizo ni fluoride iliyo zidi kwenye maji tangu mtu akiwa tumboni mwa mamake (reffer embryology - teeth formation).kwa sababu ya wingi wa fluoride, itakuwa incorporated badala ya calcium, na kutengeneza fluoroxyapetite ambayo ni brown, badala ya hydroxyapatite ambayo ni nyeupe. Tatizo hilo halikomei kwenye meno tu bali na mifupa itayotengenezwa kipindi unapo kuwa exposed kwenye fluoride, meno na mifupa vilivyo athirika hubadilika rangi na kuwa brown na huwa brittle pia. Tatizo la fluoride iliyo zidi si la wana Arusha tu bali na wale wa singida, tabora/Igunga, shinyanga /kishapu, meatu, Simiyu,Mbeya maeneo ya Mbalizi. Kuzuia tatizo hilo ni kuepuka matumizi ya maji yenye fluoride iliyo zidi tangu mimba ya week 5, kuondoa fluoride iliyo zidi kwenye maji (defluoridatio). Kwa walio athirika tayari kuna huduma za dental bleaching and veneering through dental services. Karibuni kwa maswali zaidi....
Shukran sana kwa clarification.
 
Naungana na NN wengi wao ni wachafu balaa, nilikutana na demu wa chuo lkn ni majanga sijui kwa nini.

NB: sina conglicting interest juu ya hili ni exoerience niliyokutana nayo, na si wote

Kumbe na wewe unajua eeh?

Safi sana kamanda.

Lazima tuwaambie hao watu.

Wamezidi kuwa wachafu.
 
sio wachaga wala sio moshi tu ni ukanda mzma wa kaskazini kuanzia Tanga hadi Manyara wote wana meno ya aina hiyo n kutokana na maji yana floride kuwa nyng kwenye maji na ww ukikaa kwa mda wa miaka mi5 utapatwa na hilo tatzo
Ni wilaya gani Tanga?
 
Habarini Wadau,

Nimewahi kufika na kukaa kwa muda katika maeneo ya kibosho na huru kilimanjaro kwasababu za kikazi,nimeona asilimia kubwa ya wenyeji wa huko wana meno yenye rangi yaani isiyokuwa myeupe pee,na wengine meno yao yana utando mweusi.

Nimesikia mara kwa mara kuwa sababu ni wingi wa flouride katika maji wanayotumia,ila hata kuwa na utando mweusi ni sababu ya flouride au kuna sababu nyingine?

Pia ni nini suluhisho kwao waliokuwa tayari wana meno ya hivyo ukubwani?

Nawasilisha.
Suluhisho wanahitaji kupigia mswaki na Baking soda itasaidia kuondoa calcium na ugwasu wa meno.
 
Back
Top Bottom