Mkuu tatizo ni fluoride iliyo zidi kwenye maji tangu mtu akiwa tumboni mwa mamake (reffer embryology - teeth formation).kwa sababu ya wingi wa fluoride, itakuwa incorporated badala ya calcium, na kutengeneza fluoroxyapetite ambayo ni brown, badala ya hydroxyapatite ambayo ni nyeupe. Tatizo hilo halikomei kwenye meno tu bali na mifupa itayotengenezwa kipindi unapo kuwa exposed kwenye fluoride, meno na mifupa vilivyo athirika hubadilika rangi na kuwa brown na huwa brittle pia. Tatizo la fluoride iliyo zidi si la wana Arusha tu bali na wale wa singida, tabora/Igunga, shinyanga /kishapu, meatu, Simiyu,Mbeya maeneo ya Mbalizi. Kuzuia tatizo hilo ni kuepuka matumizi ya maji yenye fluoride iliyo zidi tangu mimba ya week 5, kuondoa fluoride iliyo zidi kwenye maji (defluoridatio). Kwa walio athirika tayari kuna huduma za dental bleaching and veneering through dental services. Karibuni kwa maswali zaidi....