Mtoa mada unadanganya umma kwa uandishi wako tu inaonekana sugu ujaanza msikia mwaka 2000 bali umehadithiwa
Hatuna mpenzi wa huu mziki wa kizazi kipya wa kufoka foka anayeweza kudharau kazi za Mh mbilinyi
Historia ya mziki huu kati ya prof Jay na mbilinyi ni kubwa mno huwezi itaja safari ya sugu kwenda ulaya na kutangaza anaacha mziki pasipo mtaja prof Jay
Huwezi kutaja mashairi mazuri na yenye mvuto ya prof Jay pasipo kumtaja sugu
Kiuhalisia sugu ndio alitangulia kutoka kwenye game ila tungo zake zenye mafunzo na ujumbe mfano mikononi mwa polisi, mambo ya fedha, nimesemama, nk, ni nyimbo zilikuwa na ujumbe kupitia tungo hizo ndio zikawashaeishi wasanii mbali mbali kuja na nyimbo zenye ujumbe
Hali hiyo ikapelekea HBC kuja mwaka 2000 mwanzoni wimbo kama chemsha bongo nk, zikipatikana katika ablam ya funga kazi yao HBC, kundi lilomtambulisha prof Jay na badae kuja kama solo artist na wimbo wake jina langu, badae bongo dsm
Watalamu wa mambo wa nakwambia wimbo wa bongo dar es Salam ndio ulisababisha sugu atangaze kuacha mziki na kuamua kwenda marekani kwani ilionekana wazi kabisa kuwa sugu kapata mpinzani na ana uwezo zaidi yake, mpaka kina dolla so walipagawa ukitaka amini prof aliwaumiza kichwa sikiliza wimbo wa wengi walikuwepo sasa hivi wako wapi ulioibwa na dollar so Kuna mstari anaimba kuwa watu wanasema eti dolla so ni mkali kama Jay hapo ndio ujue prof aliwaumiza vichwa
Stori za mtaani zilisema hivi kipindi prof katoa wimbo wa jina langu aliendaga Tanga akawa anafanya kazi na kampuni ya simu basi ikitokea Siku prof akakutana na sugu prof akawa anaomba ushauri kwa sugu kuwa brother naitaji achia wimbo unaitwa bongo dar es Salam, sasa kwakua sugu alikuwa kaanza pambanisha na prof basi sugu akaja dar fasta akarekodi wimbo kama mnaujua unaitwa dar dsm sema dar es Salam ili prof akitoa wimbo aonekane kaiba wazo la sugu
Bwana wangu prof ni prof tu siku si Siku sugu akasikia prof kachia wimbo bongo dar es Salam akadata sugu jinsi Kijana akivyochambua jiji hap hapo sugu akaomba kuacha mziki na alitamka anaacha mziki
Nimechoka kuandika tushazeeka enzi zetu zimepitishwa inatosha kwa hiki kidogo nilichochangia
Ila ujue pamoja na ukali wote wa prof Jay alikuwa anafichwa na fanani, fanani alikuwa anajua ukitaka amini tafuta ablam ya funga kazi yao HBC sikiliza uandishi wa fanani ndio utajua prof alikuwa hagusi sema ndio hivyo fanani hatuitaji hueshimu mziki hatimae kaishia kwenye uteja