Ni nyimbo zipi za Sugu zenye Ujumbe na zilizohit sana kuliko za Professor J?

Dei waka dei waka yeahhhhh dei waka dei waka yeahhhh x 4

Nionjesheni kidogo mashairi ya huu wimbo

Na kuna ule wimbo anasema yupo kwenye mziki kabla ya redio za FM , sijui waitwajeee
Sugu 'moto chini'...
 
Dei waka dei waka yeahhhhh dei waka dei waka yeahhhh x 4

Nionjesheni kidogo mashairi ya huu wimbo

Na kuna ule wimbo anasema yupo kwenye mziki kabla ya redio za FM , sijui waitwajeee
Sugu 'moto chini'....
 
Sugu na prof bhana prof ana nyimbo nyingi kali sana sugu za kutafta kwa tochi heshma yake kubwa ni uasisi wa music tz
Prof hawezi kuwa kama SUGU, MTU kaimba mpaka miduara halafu mmfananishe na SUGU kweli?
 
SUGU NI NOMA, HAO WATOTO WA JANA HAWAWEZI JUA NJISI GANI SUGU NYIMBO ZAKE ZILIVYOKUWA ZINAGUSA VIJANA KIPINDI KILE, PROFES YUPO VIZUR BT SUGU NI KIBOKO, SIKILIZA KAKA TULIOSIKILIZA NYIMBO ZA SUGU MIAKA NA 90s NA KUSIKILIZA PRO J MIAKA YA 2000s TUNAKWAMBIA SUGU MWISHO
 
Mtoa mada unadanganya umma kwa uandishi wako tu inaonekana sugu ujaanza msikia mwaka 2000 bali umehadithiwa

Hatuna mpenzi wa huu mziki wa kizazi kipya wa kufoka foka anayeweza kudharau kazi za Mh mbilinyi

Historia ya mziki huu kati ya prof Jay na mbilinyi ni kubwa mno huwezi itaja safari ya sugu kwenda ulaya na kutangaza anaacha mziki pasipo mtaja prof Jay

Huwezi kutaja mashairi mazuri na yenye mvuto ya prof Jay pasipo kumtaja sugu

Kiuhalisia sugu ndio alitangulia kutoka kwenye game ila tungo zake zenye mafunzo na ujumbe mfano mikononi mwa polisi, mambo ya fedha, nimesemama, nk, ni nyimbo zilikuwa na ujumbe kupitia tungo hizo ndio zikawashaeishi wasanii mbali mbali kuja na nyimbo zenye ujumbe

Hali hiyo ikapelekea HBC kuja mwaka 2000 mwanzoni wimbo kama chemsha bongo nk, zikipatikana katika ablam ya funga kazi yao HBC, kundi lilomtambulisha prof Jay na badae kuja kama solo artist na wimbo wake jina langu, badae bongo dsm

Watalamu wa mambo wa nakwambia wimbo wa bongo dar es Salam ndio ulisababisha sugu atangaze kuacha mziki na kuamua kwenda marekani kwani ilionekana wazi kabisa kuwa sugu kapata mpinzani na ana uwezo zaidi yake, mpaka kina dolla so walipagawa ukitaka amini prof aliwaumiza kichwa sikiliza wimbo wa wengi walikuwepo sasa hivi wako wapi ulioibwa na dollar so Kuna mstari anaimba kuwa watu wanasema eti dolla so ni mkali kama Jay hapo ndio ujue prof aliwaumiza vichwa


Stori za mtaani zilisema hivi kipindi prof katoa wimbo wa jina langu aliendaga Tanga akawa anafanya kazi na kampuni ya simu basi ikitokea Siku prof akakutana na sugu prof akawa anaomba ushauri kwa sugu kuwa brother naitaji achia wimbo unaitwa bongo dar es Salam, sasa kwakua sugu alikuwa kaanza pambanisha na prof basi sugu akaja dar fasta akarekodi wimbo kama mnaujua unaitwa dar dsm sema dar es Salam ili prof akitoa wimbo aonekane kaiba wazo la sugu

Bwana wangu prof ni prof tu siku si Siku sugu akasikia prof kachia wimbo bongo dar es Salam akadata sugu jinsi Kijana akivyochambua jiji hap hapo sugu akaomba kuacha mziki na alitamka anaacha mziki

Nimechoka kuandika tushazeeka enzi zetu zimepitishwa inatosha kwa hiki kidogo nilichochangia


Ila ujue pamoja na ukali wote wa prof Jay alikuwa anafichwa na fanani, fanani alikuwa anajua ukitaka amini tafuta ablam ya funga kazi yao HBC sikiliza uandishi wa fanani ndio utajua prof alikuwa hagusi sema ndio hivyo fanani hatuitaji hueshimu mziki hatimae kaishia kwenye uteja
 
Mkuu kwa hiyo Nyerere alipong'atua hiyo mwaka 1996 ndio Bwana Sugu alipoachia hiyo ngoma yake?!
 
Sehemu ktk mistari ya wimbo huo inasema hivi ...wakati wa rumba kali saa moja shuka utosini na kujifanya unawaza mambo mengi ya ofisini, sikiliza kichapo chake pale m'bongo anapozipata, ni mwendo wa viti virefu jirani na nyama choma, na toto mbili tatu za geti au za kona, hii husema tunapoteza mawazo ila mara nyingi hutokea wakati wanazo!
Pitia pitia night kali mitaa ya kinondoni...
Kinadada poa nusu uchi na fegi mdomoni, na kama unagari watajazana madirishani wee.. Na wote wanataka hisani...



Hatukatai Sugu alianzia ila Prf.J ni zaidi ya Sugu.
 
Mkuu kwa hiyo Nyerere alipong'atua hiyo mwaka 1996 ndio Bwana Sugu alipoachia hiyo ngoma yake?!
ndugu huu ukata wa leo unaweza mlaumu Magufuli kweli,hapa wa kulaumu kikwete kampa mwenzie kazi ya kurekebisha by then mkapa kaingia kaanza kurekebisha matatizo ya nyerere yaliyomshinda mwinyi hata baada ya kuapply structural adjustment policy iliyosisitiza ukusanyaji mapato ndo maana matajiri wengi 1995 walifilisiwa kwa makadilio makubwa ya VAT utakumbuka wengi walikimbia mikoani wakaenda DAR ,Kariakoo na hata TRA ilianzishwa 1996.been there
 
TRA imeanzishwa na mwinyi,imeanza kazi kipindi cha mkapa
 
na unapokua na kitu,bongo ni kama new york,kila siku ni sikukuu,utakula kuku na chochote utachopenda,mpaka denda,kila dem atakuita handsome-sugu mwaka 1996
 
Tatizo wengi wanao mponda sugu ni watoto wa juzi tu na wameanza kusikiliza mziki /bongo flavor miaka ya 2000 wakati radio za fm zimeanza kusambaa kwa kasi nchi nzima. Sugu alikua anafanya mziki wakati prof Jay yuko shule tena form 1 huko lutengano tukuyu. Prof Jay na hard blasters wanatoa album ya kwanza sugu ana album 4 sokoni na wakati huo bongo flavor haipigwi redioni. Mr 2 aliubeba mziki toka shimoni single handedly ndipo wakina prof Jay wakaanza kula matunda.
 
TRA imeanzishwa na mwinyi,imeanza kazi kipindi cha mkapa
Dahh unahitaji nikuweke chini nikujuze hapa hatutamaliza mdogo wangu.TRA haikuanzishwa kwa uweledi au mapenzi wa mwinyi bali kama mojawapo ya masharti magumu ya kitu ilikuwa inaitwa STRUCTURAL ADJUSTMENT POLICY hii ndo iliyomfanya nyerere ang'atuke hivyo awamu za mwinyi na mkapa zilikuwa zinatibu balaa ya kuanguka urusi (tumaini letu) nyerere akaogopa kumeza matapishi yake ...its a damn long story
 
structural adjustment policy 1&2 haikuwa na masharti ya kuanzisha tra,acha kunifanya mi mtoto na shule sikwenda
 
structural adjustment policy 1&2 haikuwa na masharti ya kuanzisha tra,acha kunifanya mi mtoto na shule sikwenda
Long-term adjustment policies usually include:[1][8]

tizama penye nyekundu ,wazungu walikuwa wanataka tuwa na sound financial institution ndo wamwage mikopo ,usizani mkapa alipenda ilikuwa ni hiyo condition ya pili
SOURCE: wikiepaedia
 
Yote hayo ni sawa mkuu ila anachojaribu kukieleza mleta uzi kulinganisha uwezo binafsi wa kila mmoja ktk kutunga na kuwasilisha fanani ktk hadhira,
Yaani ile perfomance ya Sugu na Prf. J.
Na sio nani wa kwanza kabla ya nani, wote ni wazuri na kila mmoja kafanya makubwa.
Lakn je uwezo binafsi ktk kutunga na kuimba nani ni nani??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…