Ni sahihi fundi kupiga picha kazi aliyopewa aifanye, na kuitumia kujitangaza bila makubaliano na mwenye kazi?

Ni sahihi fundi kupiga picha kazi aliyopewa aifanye, na kuitumia kujitangaza bila makubaliano na mwenye kazi?

Sheillah Sheillah

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2020
Posts
653
Reaction score
1,698
Habari?

Unamtafuta fundi kisha unampa kazi yako na unampa malipo yake kama mlivyokubaliana.

Akimaliza kufanya kazi yako anaipiga picha na kuianika mitandaoni akijitangaza kwamba ni yeye kaifanya.

Hapa mfano mkubwa ni fundi wa ujenzi, deco, kupaua ,rangi nk. Wanafanya kazi kisha wanapiga nyumba yako picha na kuianika mitandaoni.

Wengine ni fundi nguo. Unatafuta mshono wako wa nguo yako ya siku yako muhimu mfano harusi, kisha unampa kazi. Akimaliza anaivalisha kwenye mdoli anaiweka kama matangazo na kuituma mitandaoni.

Je ni sahihi nikulipe pesa ufanye kazi yangu kisha utumie kujitangaza bila makubaliano na mimi?
 
Acha unoko kwani we celebrity hebu mpe riziki maskini

Acha unoko kwani we celebrity hebu mpe riziki maskini mwenzio
Una akili? unajua kusoma na kuelewa?
umeona nimeandika sitaki apige picha mali yangu? Mimi nimeuliza ni sahihi au sio sahihi.
Je kama mimi ni fundi cherehani nimepiga picha nguo ya mtu na sasa ananiletea shida ndio maana nataka kujua ni sahihi au sio sahihi?
 
Una akili? unajua kusoma na kuelewa?
umeona nimeandika sitaki apige picha mali yangu? Mimi nimeuliza ni sahihi au sio sahihi.
Je kama mimi ni fundi cherehani nimepiga picha nguo ya mtu na sasa ananiletea shida ndio maana nataka kujua ni sahihi au sio sahihi?
Matusi ya nn.ok .sio sahihi maana kwanza unaingilia faragha yake pili Ubunifu ni bidhaa kusambaza bila taarifa ni wizi .
 
Matusi ya nn.ok .sio sahihi maana kwanza unaingilia faragha yake pili Ubunifu ni bidhaa kusambaza bila taarifa ni wizi .
Sasa umenijibu vizuri, samahani kwa lugha kali.

Mimi jana nimeenda kusuka. Amenisuka nimependeza na nimemlipa hela yake. Baadaye napita instagram nakuta kumbe mimi bila kujua amenichukua video amepost. Nikamwambia ashushe post au anirudishie hela yangu ili nijue mimi ni modo wake wa matangazo.

Wiki kadhaa nyuma mpiga picha alikuja nikafanya photo shoot za gender reveal za my unborn baby. Na lengo ni niziweke baada ya kujifungua. na kila picha niliilipia.
Sasa na yeye akazipost kwenye page yake. Bila ruhusa yangu.

Sasa ndio ninawaza ni sahihi au sio sahihi? au ni mimi nina matatizo.
 
Mkuu, kwani anapoitangaza anataja na majina ya Mmiliki?

Mfano;
Hii nyumba ni ya Ms Sheillah, ipo mtaa wa Kinondoni B. Paa na urembo wa ndani nimefanya mimi, Fundi Restart. Hebu angalia ilivyopendeza.

Kama hatoi maelezo ya Mmiliki basi sioni shida. Picha hizo ndizo CV yake. Bila shaka hata wewe ulishawishika baada ya kuona kazi zake.

Lakini kama ni kitu ambacho hukitaki, basi mwanzo wa makubaliano yenu mtahadhari kuwa usingependa nyumba yako ipigwe picha.
 
Habari?

Unamtafuta fundi kisha unampa kazi yako na unampa malipo yake kama mlivyokubaliana.

Akimaliza kufanya kazi yako anaipiga picha na kuianika mitandaoni akijitangaza kwamba ni yeye kaifanya.

Hapa mfano mkubwa ni fundi wa ujenzi, deco, kupaua ,rangi nk. Wanafanya kazi kisha wanapiga nyumba yako picha na kuianika mitandaoni.

Wengine ni fundi nguo. Unatafuta mshono wako wa nguo yako ya siku yako muhimu mfano harusi, kisha unampa kazi. Akimaliza anaivalisha kwenye mdoli anaiweka kama matangazo na kuituma mitandaoni.

Je ni sahihi nikulipe pesa ufanye kazi yangu kisha utumie kujitangaza bila makubaliano na mimi?

kama sio kampuni ni sahihi kabisa ispokua kampuni.
Picha halali yako ni kwenye Raman yako ya nyumba na baadae ukikabidhiwa nyumba yako bas picha na video na zako pia
 
Mkuu, kwani anapoitangaza anataja na majina ya Mmiliki?

Mfano;
Hii nyumba ni ya Ms Sheillah, ipo mtaa wa Kinondoni B. Paa na urembo wa ndani nimefanya mimi, Fundi Restart. Hebu angalia ilivyopendeza.

Kama hatoi maelezo ya Mmiliki basi sioni shida. Picha hizo ndizo CV yake. Bila shaka hata wewe ulishawishika baada ya kuona kazi zake.

Lakini kama ni kitu ambacho hukitaki, basi mwanzo wa makubaliano yenu mtahadhari kuwa usingependa nyumba yako ipigwe picha.
Sawa mkuu nimekuelewa.

Ila pia wapo watu ambao hata mimi wamewahi kunifuata kuniomba kazi ya kunyanyua paa la nyumba yangu liwe mtindo wa kisasa.

Waliniambia wao wanafanya hiyo kazi kwa lengo la kujitangaza wapate jina yaani wajulikane. Hivo ningewalipa hela kiasi fulani tu. Kweli niliwapa kazi na kazi ilijitangaza na wenyewe walitangaza. Mtaani kwetu hapa walipata wateja wengi sana maana nyumba nyingi za hapa ni za miaka ya nyuma kidogo.

sasa hawa waliweka wazi lengo ni kujitangaza. nahisi na wwngine walipaswa wazingatie hili pia. Kufa kufaana.
 
Back
Top Bottom