Ni sahihi Mwanamke kutimiza miaka 31 hajaolewa? Ukimuoa kuna faida hapo?

Ntachangamkaje sasa, Hata ukiwapata watu nafasi unakuta nao hawana hata mpango[emoji847] au hajakuelewa miaka ndio inaenda ivyo mwisho tunazeeka.
Zama zimebadilika kweli umri wangu huu mama angu ana ndoa ya miaka6[emoji22] na watoto wawili
 
Hapana mkuu
ila imebidi nihoji maana masakamo yamekua mengi hata usipozaa kiafrika jiandae kupambana na changamoto

Nakuelewa sana, uishi vipi maisha yako binadam hauwezi kuwaridhisha wote kwa pamoja. Alimradi hauathiri mtu au kuvunja sheria na wewe uko sawa na amani yako, ishi unavyoona inafaa na kukupendeza.
 
Hapana mkuu
ila imebidi nihoji maana masakamo yamekua mengi hata usipozaa kiafrika jiandae kupambana na changamoto
changamka shauri yako.38 hujazaa wala huna mtoto utapata sana changamoto tena watu wa kwanza kukusema watakuwa wanawake wenzako tena ndugu zako kabisa mfano mama yako,shangazi yako n.k.mimi nina uhakika hata wewe mwenyewe moyoni mwako unaona si sawa kukaa mpaka 38 bila mtoto wala kuolewa.tena huko ulaya ndo bora hata afrika.ulaya na marekani hakuna maadili watu wana wanajiachia tu.mapema tu mabinti wanazaa.huko binti anaruhusiwa kabisa kwenda kulala kwa boyfriend au boyfriend kwenda kwa binti na wazazi hawana noma sio kama huku bongo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fact

Acha kukaa kihasara hasara
 
mwaka juzi nilikuwa bunda mara, nikahudhuria harusi moja pale. walengwa: mwanamke alikuwa na umri wa miaka 45 na hakuwahi kuwa na mtoto na ni mara yake ya kwanza kuolewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…