Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Mkoa wa Songwe..... ukiwa unamaliza kupanda mlima wa Senjele unataka kushoto kuna sehemu inaitwa Iyula.....huko kuna kijiji kinaitwa Idiwili.......yaani kule nimeshangaa watu wamefata nini kule........watu mpaka saa nne hakuna aliyeamka baridi kali....watu wanalala huku wameacha milango wazi ili kuku watoke pakikucha......mitaani kumezagaa nguruwe tu na vitoto vya nguruwe.....
 
kibondo kigoma yani, ilikua mwaka 2015 , kwanza kufika uko ni barrier za maana tulikutana nazo barabarani adi nikajiuliza ivi uku ni Tanzania au nchi nyingine.

kwanza kipindi icho uko kibondo ukienda kijiji kimoja ukitaka kwenda kingine ni hakuna njia ya shortcut ni lazima urudi barabara kuu ndio uanze moja, alafu kuna mito ina mamba, na nyumba kule ni za nyasi yaani unaambiwa ukiezeka bati tu umekwishaaaaa ni wanakuloga
 
Dodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,watoto wamebabuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
Wewe unisurika kuchomwa moto na gari lenu. Kimsingi wanawaona kama wanyonya damu za watu
 
Habari za muda huu wana JF,

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji cha Baranga kata ya Sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndio kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu, jua kali ndio kwao, vurugu Sasa ndio chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafiki na timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa na mgogoro wa mpaka wa shamba kati ya ukoo na ukoo huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu nini?
Ni wapi huko, hao ndio waandamanaji wanaotakiwa Tz.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
kijiji cha tanganyika,kata ya masagati tarafa mlimba wilaya ya kilombero .nikipangiwa kule kituo cha kazi mwaka 1999 nikarudi kumshukuru DED kwa kazi.nikarudi zang Dar .aise Kule watu alikuwa wanaishi kama mazombie hakuna huduma ylza jamii hata moja hadi uende mlimba 150km Dahhh ila nasikia mambo siku hizi yamebadilika Luna kula kitu japo afadhari.
Dah umenikumbusha mbali, tanganyika masagati, iduhi ndembo na utengule.
 
Kuna sehemu Mkoa wa mbeya inaitwa Lupa tingatinga then unaingia ndani ndani huko kunaitwa Nkunungu aisee nliona watoto wa shule ya msingi shati Lina rangi ya udongo hata ufulie jiq haliwezi takata! Umasikini ni mkubwa sana vijijini, Bado watu hutumia mitishamba kwa kiasi kikubwa! Nlikuwa nna project ya research kule sasa pencils nlikuwa nazo kwenye vibox ikabidi nizikatekate nigawe kwa watoto karibia darasa la pili wote walikuwa hawana mtoto anakipenseli kama ukucha! Kila nikikumbuka huwa nawaza wale watu ni lini watakuja kuondokana na Hali ile
 
Kuna sehemu Mkoa wa mbeya inaitwa Lupa tingatinga then unaingia ndani ndani huko kunaitwa Nkunungu aisee nliona watoto wa shule ya msingi shati Lina rangi ya udongo hata ufulie jiq haliwezi takata! Umasikini ni mkubwa sana vijijini, Bado watu hutumia mitishamba kwa kiasi kikubwa! Nlikuwa nna project ya research kule sasa pencils nlikuwa nazo kwenye vibox ikabidi nizikatekate nigawe kwa watoto karibia darasa la pili wote walikuwa hawana mtoto anakipenseli kama ukucha! Kila nikikumbuka huwa nawaza wale watu ni lini watakuja kuondokana na Hali ile
Unawawaza halafu wao wanaona kawaida
 
Mimi nilifika sehemu moja panaitwa salawe shinyanga v/jijini kuna mnada mkubwa wa ng'ombe jumamos siku moja ulitokea upepo mkali kuna upepo flan huwa unakuja kama mnara mrefu huwa unazunguka kwa kujinyonga kama kamba unasepeed san huwa unatumiwa na wachawi ule upepo ulikufika ulianza kuondoka na vitu kam pesa za matajiri zilizokuwa mkononi na mifugo kupotea tu maana lazima ufumbe macho vumbi kali mno cha ajabu ulienda kupita kwenye gari la tajiri mmoja maarufu mnunuzi wa ng'ombe ukasepa na jacket lilikuwa ndani ya gari na pesa nyingi sana tuliishia kuliona juu tu linazid kupaa na hatukuona liliposhukia huku upepo unazid kusepa,, hiyo sehemu kuna uchawi balaa.
 
Dodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,watoto wamebabuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
God must be crazy kumbe bado inaishi
 
Back
Top Bottom