Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Kuna kijiji kipo katikati ya Kidete wilaya ya Kilosa na Mpwapwa magenge 30 kinaitwa Nana, kwa Mara ya kwanza nilikaa hapo wiki moja bila kuoga, dumu la maji ya mtoni ni buku mnatumia kupikia na kunywa, anayewauzia hayo maji akitoka alfajili kufuata maji na punda anarudi SAA 10 jioni.

Nilipoanza kutafiti maisha yao siku moja Mwenyeji akanipeleka kwa mama mmoja ndio ana club ya pombe za kienyeji ila Mimi nilikwenda kununuwa mihogo asubuhi tuchemshe kunywea chai kambini.

Sasa nikashangaa kila mlevi anayekuja pale amebeba kibegi cha sports mgongoni nikamuuliza mbona hii style siielewi? Akaniambia huku watu hawana pesa ukitaka kunywa pombe unakuja na maindi kwenye kibegi yanapimwa mama muuza anakupa pombe yeye anachukuwa mahindi, aisee Yale maisha ni Bonge la adventure kwangu.

Sehemu zenye madini zina asili ya kutokuwa na maji, madini na maji havikai pamoja, serikali iwahurumie watu hawa kuwapelekea maji maana hata ukichimba visima Mirefu huwezi kupata maji sehemu yenye madini.
Dodoma kuna madini gani?
 
kijiji cha tanganyika,kata ya masagati tarafa mlimba wilaya ya kilombero .nikipangiwa kule kituo cha kazi mwaka 1999 nikarudi kumshukuru DED kwa kazi.nikarudi zang Dar .aise Kule watu alikuwa wanaishi kama mazombie hakuna huduma ylza jamii hata moja hadi uende mlimba 150km Dahhh ila nasikia mambo siku hizi yamebadilika Luna kula kitu japo afadhari.
Tanganyika ni kijiji ambacho unakwenda ukifika hapo ndo mwisho wa barabara hakuna kuendelea....siku niliyofika kwenye kile kijiji nilijiuliza maswali mengi sana khs wale watu wanavyoishi kule.
 
Bora hata mpanda, kuna mahali panaitwa MAJIMOTO aisee huko nilipoenda nilijiuliza qatu wamefuata nini, na wengi wao ni wasukuma kule...Ajabu ni kwamba they are making money ile hatari. Ni matajiri wa kutupwa kutokana na kilimo ufugaji na madini.
Yes majimoto nishawahi kufika, hilo jina linatokana na Chem Chem ya majimoto iliyopo hapo kijijini
 
Kuna Kijiji kinaitwa mapangali kipo Iringa.

Unashukia ilula alafu unachukua bodaboda na ni mwendo wa saa 1 nauli kwasasa inaweza kuwa 25000 maana mara ya mwisho ilikua 20000 na hakuna gari la abiria kwenda kule .
Uwe na uvumilivu haswa maana utapanda milima mpaka utahisi bodaboda inapinduka.
Nilivofika kule nikajiuliza hivi watu wanaishije huku japo pesa ipo.
 
Niliwahi kufika kule mwaka 2002 mpaka mimea inaungua kutokana na baridi nilifika kandete, kyejo mpaka isange kupitia kiwanda Cha majani ya chai Katumba au Tandale Tukuyu Mjini.
Nimezunguka sana maeneo hayo, na njia yao ile ya mawe mawe ukitoka katumba kuanza kuitafuta mwakaleli, ila baridi ipo ifupa aisee ,hiyo ni ndugu yake na makete, yani mchana wa saa nane watu wanaota moto
 
Wewe kilimanjaro una maanisha Moshi, njoo same na mwanga ndiyo utajua hujui. Watu huku wamekauka unaweza kuwapasua kuni na ukapikia maharage yakaiva haraka kuliko stima
Wilaya ya mwanga iko vizuri Sababu watu wengi wanaishi miliman mfano usangi na ugweno kunafikika kwa lami

wilaya ya same ndo changamoto Kuna vijiji kama chome unajiuliza watu wanaishije kwanza ni mliman sana
 
Umeishawahi kufika mamba kwa nabii eliya? Guantanamo ni mbinguni
Wilaya ya same jiographia yake ni ngumu sio mimba hata chome hapafikiki kirahisi ndomaana wapare wa same hawapendi kwenda kwao sababu hapafikiki ni tofauti na wapare wa same kwao kuna lami yaan kunafikika
 
Back
Top Bottom