Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Tanzania sio kubwa acha chai
Mzee Baba kama hujatembea ila linchi likubwa japo naona unataka fananisha na Russia. Nchi kubwa sana hii na ina mapori Mengi sana. Mara ya Kwanza natoka Nyumbani Arusha naenda Katavi pitia Tabora ndio niliona linchi lilivyo kikubwa. Kuna kipindi nilitoka Kagera kwenda Kugoma via Nyakanazi. Sio kwa Misitu ile.
 
Sehemu nyingine ipo wilaya ya Mbalali mkoa ni Mbeya kule Blonde la Mpunga la Usangu. Kule kuna vijiji vingi Sana. Kuna Kijiji nilikaa pale Miezi nilishangaa Sana.

1. Sikuwahi kusikia Kuna kituo cha police au police . Kule bangi inavutwa kama sigara.

2. Kwa wale wala kitimoto kule inauzwa kama Dagaa.

3. Kwasababu kitimoto ni nyingi Sana na hawaoimi Kwa kilo wanaweka Kwa mafungo kama nyanya. Kitimoto ya 4,000 ukimaliza wewe ni shujaa.

4. Sikuwahi kuona limao, kitunguu , Ndizi za kuiva wala nyanya.

5. Hiyo kitimoto inapikwa Ila bila hivyo vitu hapo juu.


6. Usiku kuisikia Sauti ya wanyama wakali kama Simba na tembo ni kawaida.


7. Kuna Baridi usiku kama uko Yemen au Kwenye Vilima Vya magaidi wa Taliban kule Afghanistan.

8. Sikuwahi kuona kiwanja cha mpira hata kupiga danadana.


9. Kule mchele na wali unaweza Kula Hadi ufe hakuna Kijiji nimetembea tanzania nikakuta kina mchele kama kile.
Kinaitwaje mkuu?
 
Tangeni bila shaka[emoji16] siku ya jumapili wanashuka milimani kuja kugonga kitimoto
Mkuu Tangeni hapo jirani na Mzumbe University? Hiyo labda itakuwa Bunduki au kule Juu kabisa ya Kijiji kinaitwa Nyandira..
 
Tanzania sio kubwa acha chai
Ukubwa wa Tanzania ni 945,087 km²... Yaani ukiunganisha Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda labda ndiyo itakaribia... Kwa ukubwa wa hii nchi ili kila eneo lipate maendeleo ya haraka ilikuwa ni vema kuwa na mfumo wa majimbo, yaani mfano Kigoma, Katavi na Rukwa jimbo moja hilo ambalo linapewa mamlaka ya kutumia sehemu ya asilimia from their resources kwa maendeleo yake...
 
Nenda Morogoro shuka msamvu, chukua bodaboda akupeleke hadi shule ya msingi kikundi, nauli 1500.
Ukifika pale angalia mlimani kule watu wamejenga mlimani yaani. Sasa unajiuliza hawa watu hata mabati walipelekaje kule!
Niliwahi kwenda kijiji kinaitwa Lunenzi, huko wilayani Kilosa. Huko kila kitu kinabebwa kwa kichwa mpaka simenti, nondo, bati etc..
 
Na Kuna Kijiji Cha utengule pembezoni mwa safu za milima ya Kipenge Mkoa wa Njombe Ni Kama Kisiwa wakinga wa kule wakitaka mahitaji wanakuja wilaya jirani ya Kyela sehemu hiyo inaitwa Ngyekye kupitia hiyo milima wakati huo nasoma Shule moja Matema Beach Sec Basi usiku unaona tochi hapo ujue ndo wanashuka Mnadani kufuata mahitaji hasa siku ya alhamisi. Utastaajabu mlima una urefu wa Mita 2600 lakini wanashuka madebe ya ngano kichwani au maharage ndipo auze halafu arudi na madebe ya mchele. Sisi tulipanda ule mlima tukiwa hatuna mizigo lakini tulichoka mpaka tulitoa jasho la njano. Jamaaniiiiiiii usimuliwe tu unakutana wamama mpaka wanavipara nywele zimenyonyoka ktokana na kubeba mizigo wakati huo anapanda mlima akiwa na andasket tu maziwa yote njenje Kama makilikili na hawashtuki. Duuuu Tanzania Ni Pana. Sijui walifuata nini Kule.
Kijij hcho Cha ngiyeke naifahamu Kuna mtu wa kijij. Hicho aliwai nitapeli Kijiji unaacha ipinda kwa nyuma Kisha unaanzaa kuikabili mlima wanyakyusa Ni wengi mno Nan Ni wale wa oh kbsa

Sent from my Infin
 
Ukifika siha na hai Barbara ya kwenda merarani hutatamani

Pia same na mwanga ni pa hovyo mno
Mwanga kwenda wapi? Maana kama ni kwenda milimani usangi au ugweno kuna lami mpaka pale Kikweni... Same napo kumekuwa sanaa
 
Vijiji vya Vunta na Kidunda, Hedaru, wilaya ya Same.

Ni vijiji vilivyo milimani - ktk Safu ya milima ya Usambara.
Ukitokea Mombo, kabla ya kufika Hedaru, unakata kulia na kuanza songombingo la kupanda mlima kuelekea vijiji hivi.
Issue hapa ni barabara ya vumbi yenye slope kubwa ajabu! Dereva akifanya kosa kidogo tu, mmekwisha kwani gari litaserereka bondeni takribani mita 600 - 800 hadi litakapogonga mwamba na kusimama! Bila gari imara lenye 4-W, huwezi kwenda kule.
Wakati wa kurudi toka Vunta, nilimuuliza mwenyeji wangu kuwa kwanini hawa Wapare waliamua kwenda kuishi sehemu hatarishi kama zile? Aliniambia kuwa, Wapare walikimbilia kwenda kule kwa ajili ya maficho kutokana na vita kati yao na maadui zao pamoja na maasidi wao - Wachagga. Ilikuwa zamani sana kabla ya ujio wa Wakoloni.
Baadaye waliweka makazi mpaka leo.
Pia walikimbilia huko milimani ili wasikamatwe utumwa na waarabu..
 
Imagine njombe na Morogoro ni mikoa tajiri Tanzania....

Basi Tz ni maskini sana
images%20(52).jpg
 
Tanzania kubwa sana ndugu yangu, na ina mila na desturi na maisha ya kila namna. Naomba Mungu siku moja nikipata fedha ya ziada nitafanya ziara Tanzania nzima au sehemu nyingi kadiri niwezavyo. Sehemu kama hizo ambazo wengi wamezizungumzia hapa.
Tatizo letu sisi hatupendi kutalii na kujifunza kuhusu nchi yetu na mikoa yetu. Kuna siku nimeshangaa kwenye kundi la watu 10 ni watu 4 tuu ndiyo wametembea nusu ya mikoa ya nchi hii.. Sasa how can one learn na kuona fursa bila kutembea? Babu yangu pale Kijijini alikuwa very smart na mjuzi wa mambo mengi na wengi walikuwa wabamtegemea.. Mara zote nikimuuliza mbona unajua vitu vingi sana kuliko wenzako? Jibu lake lilikuwa mjukuu wangu tembea uone na ujifunze, ukisikia elimu dunia maana yake ni kutembea na kuona na kujifunza kwa wengine.
 
Tanganyika nako sio Mchezo? Kuna vijiji huko Tanganyika tukienda kupora ardhi yaani maarshi yapo ya kumwaga. Tuliendaga kijiji cha Kapanga Tarafa ya Mwese kupora kujigawia ardhi miaka hiyo. Tuliingia kitongoji kimoja, Ng'ombe za wasukuma zikaja na kulizunguka Gari ilikuwa Land cruiser nyeupe na kuanza kuilamba. Tuliendaga Mishamo kwenye kambi za wakimbizi, ukipita Wamama wanakuja kuchukua ule mchanga ambapo tairi la gari limepita eti ni dawa kwa mtoto aliyechelewa kutembea.
Kapanga nimepita majuzi tuu mkuu pamebadilika sana. Mishamo nilifika pia [emoji23] [emoji23]
 
Mwanga kwenda wapi? Maana kama ni kwenda milimani usangi au ugweno kuna lami mpaka pale Kikweni... Same napo kumekuwa sanaa
Nahisi anazungumzia hali ya lile Jangwa pale tambarare ya Mwanga na Same

Huko juu at least hali ya hewa ni nzuri japo udongo mkavu hauna rutuba kabisa, vindizi vinatoka vigumu kama mawe

Kule napo pagumu sana aisee
 
Hapo ndio umefafanua kitaalamu
Ukubwa wa Tanzania ni 945,087 km²... Yaani ukiunganisha Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda labda ndiyo itakaribia... Kwa ukubwa wa hii nchi ili kila eneo lipate maendeleo ya haraka ilikuwa ni vema kuwa na mfumo wa majimbo, yaani mfano Kigoma, Katavi na Rukwa jimbo moja hilo ambalo linapewa mamlaka ya kutumia sehemu ya asilimia from their resources kwa maendeleo yake...
 
Back
Top Bottom