Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Nenda Morogoro shuka msamvu, chukua bodaboda akupeleke hadi shule ya msingi kikundi, nauli 1500.
Ukifika pale angalia mlimani kule watu wamejenga mlimani yaani. Sasa unajiuliza hawa watu hata mabati walipelekaje kule!
Kule ndio wenye hela wanajenga,kwa kishua kule,
Barabara zimechongwa safi. Gari yoyote inafika nila shida.
 
Nadhani una maanisha njia panda ya Ipole, wilaya ya Sikonge, Tabora; ukiacha barabara ya kuelekea Mpanda, unayooka kushoto kwako kuelekea Rungwa. Hapo mlipokutana na bonge la joka hapo panaitwa Kitunda. Usipochukua tahadhari unaweza liwa na simba. Mbele kidogo kuna mji unaitwa Kitunda - watu wanachimba madini pale. Ukitoka Rungwa unaelekea Kambi Katoto (upande wa kusini), Chunya kisha unaelekea Mbeya. Unabidi uwe na roho ngumu kiasi ili uweze kuishi kule. Ukitoka Rungwa kuelekea Kaskazini utaingia Itigi, kisha barabara kuu kuelekea Singida au Manyoni.
Asante ww ndo umeelekeza vzuri kabisa kabisa
 
Nadhani una maanisha njia panda ya Ipole, wilaya ya Sikonge, Tabora; ukiacha barabara ya kuelekea Mpanda, unayooka kushoto kwako kuelekea Rungwa. Hapo mlipokutana na bonge la joka hapo panaitwa Kitunda. Usipochukua tahadhari unaweza liwa na simba. Mbele kidogo kuna mji unaitwa Kitunda - watu wanachimba madini pale. Ukitoka Rungwa unaelekea Kambi Katoto (upande wa kusini), Chunya kisha unaelekea Mbeya. Unabidi uwe na roho ngumu kiasi ili uweze kuishi kule. Ukitoka Rungwa kuelekea Kaskazini utaingia Itigi, kisha barabara kuu kuelekea Singida au Manyoni.
Yani Mkuuu mim nikiona joka naweza Kata moto Ile siku sitasahau....... siku tatu nkaona mwezi
 
Msitu wa inyonga
Uzi mzuri sana, huko maporini inaonekana ndipo penye hela. I wish watu wa serikalini wangeona huu uzi labda wangeingiwa huruma kutafuta hivi vijiji na kupeleka services especially kuwachimbia visima vizuri vya maji na zahanati
Wapo busy kununua V8 lakini kutenga million 500 kujenga barabara ya changarawe au kuchimba visima hawana muda na pesa hizo
Such a useless general assembly
 
Yah ni kweli ata Zanzibar kuna maendeleo kushinda Tanganyika, Nimeishi Zanzibar sikuwahi kuona Wamama wakipata shida ya maji na huduma za hospitali na usafiri, umeme upo kila sehemu, sehemu zote za Tanzania Zanzibar hawana shida za huduma za kijamii huduma zote zimewafikia wananchi, tembea Zanzibar kote huwezi kukuta mama kabeba ndoo ya maji kichwani , na uko vijiji huduma zote zipo, yani Zanzibar kuna vitu vingi vya elektroniki mpaki vijijini, Zanzibar mtu kukupa nyumba uishi au kukuazima gari lake uendeshe ni jambo la kawaida tena uko ni mashambani.
Zanzibar INA ukubwa gani?
 
Watu mna unafiki humu hivi mmeshindwa kutaja vijiji vya Singida kweli???
Watu wa singida vijijini ni watu wa ajabu sana. Imagine mtu ana kuku zaidi ya 50 lakini hachinji hata iweje...Ajabu ni kua hua wanauza kuku ili wapate hela ya kununua mlendawa kusagwa. Yaani huo mlenda unakua kama unakula ugali na hina zile za miti.
Mnyaturu akija kwako usimpikie kuku wala nyama pika mabamia wanapenda makamasi kamasi kwente chakula chao[emoji23][emoji125][emoji125]

Acha wivu wa kike hapa hatuzungumzii chakula
 
Mbona unaandika ujinga then haichekeshi
Chato
Najiuliza sana watu wa chato wanaishije.

Kama siyo uchizi lile wazo la kujenga ule uwanja lilitolewaje na fedha zikatengwa.

Sasa kuna mataahira bungeni wakaja na wazo chto iwe mkoa alafu Muleba iwe sehemu ya huo mkoa...
Yaani sisi wahaya tukawe ndani ya mkoa wa chato?

Hii nchi iliingiliwa kinyume na maambile aise
 
Uzi mzuri sana, huko maporini inaonekana ndipo penye hela. I wish watu wa serikalini wangeona huu uzi labda wangeingiwa huruma kutafuta hivi vijiji na kupeleka services especially kuwachimbia visima vizuri vya maji na zahanati
Watu wa serkali nani? Watu wapo busy kuipigania familia zao we endelea kubana pua watu wa serkali
 
Kwa mara ya kwanza kufika kijiji cha Bugamba kilichopo mwambao wa Ziwa Tanganyika Kigoma vijijini nilipigwa na mshangao baada ya kushuka kwenye boti kutokea Kibirizi Kigoma ! Pale boti zinapoegesha sikuona nyumba yoyote ! Mwenyeji wangu kaniambia tunaenda nyumbani yaani ananionyesha juu utafikiri tunaenda mwezini ! Kutoka hapo tunapanda huko juu nilitaka kulia maana chini Ziwa Tanganyika juu ndio kijijini, halooo kupanda ilibidi mpaka nishikwe mkono. Kufika huko juu ndoo nakuta kijiji na shule ya msingi ukitizama chini ziwa Tanganyika liko bondeni ! Kwa kweli inatisha kijiji hicho hakuna shamba la maana sehemu kubwa ni milima tu mihogo wanalima kwenye mitelemko ya milima na ukiteleza unaporomokea ziwani na ziwa lina kina kirefu ni hatari. Pale kijijini hakuna baiskeli maana mazingira hayaruhusu ! Shughuli za uchumi pale ni uvuvi. Ukitaka kwenda kijiji cha jirani cha Zashe au Mwamgongo lazima utumie boti kwa mguu haiwezekani.
Toka siku hiyo nikajua sababu ya waha wengi kukimbilia mikoa ya Jirani kama Mwanza, Geita, Tabora na Katavi maana mazingira ya maeneo hayo ni magumu sana. Kweli maeneo hayo ukifika mpaka unajiuliza kwamba hivi hawa watu huku walifuata nini.
Mkuu hukuona sehemu tambarare ukitoa sehemu zenye milima?
 
Kuna vijiji vipi Bumbuli daah wakuu acheni tu tulienda na gari njian watu wanatushangilia kma ni Raisi anapita tukafika mwisho wa barabara tukaanza kubeba jeneza hadi nyumbani tulichoka zaidi ya masaa6 kule tuwaachie nguruwe pori au wahamishiwe vijiji vya Kilimanjaro kuacha Mwanga.
Nimecheka kwa kelele ha haaa.
 
Siku moja niko na jamaa yangu tunatafuta mashamba ya kukodi ya alizeti tulikua na mwenyeji anatutembeza mashambani. Mchana tunataka kurudi mwenyeji akatuambia twende kwanza kwake tule ndio tuondoke. Tukaona si mbaya.
Tumefika tukaenda sebuleni Chakula kikaja nikasahau kabisa kama Chakula chao kikuu ni mlenda.
Bwana bwana ulikuja ugali mgumu na mlenda mimi nilikua sijawahi kula mlenda wala ugali wa mtama😅

Nilihangaika mwenye ananiambia mbona hauli au chakula kibaya? Mimi naguna guna tu😂, nilishwindwa kula aisee ilibidi nikaupiga picha hii hapa chini.
Yaani utadhani unakula hina. Watu wanawakiwa na jua huko ndio maana miguu yao imekomaa halafu myembamba kama mianzi imechomekwa kwenye mapaja 🏃🏃
IMG_20220428_115158_5.jpg
 
Narudia tena hakuna mkoa masikini kama Dodoma.

Mkoa ule ni hatari huko wilayani.

Nilienda huko Kijiji Cha Chimendeli wilaya ya Bahi, Kwanza hiki Kijiji ndio kinaongoza kutoa omba omba wengi Sana tanzania.

Familia zinashindana kuja mijini kuomba omba. Mzazi anaweza kumtuma mtoto wake aende mjini awe omba au mzazi anaweza kuja mjini na familia nzima waje kuwa omba omba!

Kwa ambao mko Dar Es Salaam kuanzia Leo jitahidi ukikutana na omba omba watoto au wazee wadadisi Kwa maswali halafu waulize wanatoka Kijiji gani. Halafu piga nao story hutakaa uamini !


Kama ulivyo kwenu vijana wanasoma Kwa jihadi zote waje kuwa Madaktari Ila kuna sehemu hii tanzania watu Wana ndoto za kuwa omba omba. Au kama hamuamini Ulizieni hata walimu WA Shule walioko hicho Kijiji. Watoto hawaendi shule.

Sehemu ni kame.


Lile eneo unaweza kudhan upo Pakistan au Kule Yemen.


Eneo lingini ni vijiji vya wilaya ya kongwa.


Acha niishie hapa.
 
Back
Top Bottom