ilore
JF-Expert Member
- Aug 5, 2022
- 963
- 1,248
Ng'apa ya Lindi nimeenda mwezi wa 8 minanzi ni mingi Sana pale nimefika mpaka rutamba aiseeNg'apa ipi?!!km ya Lindi sio kweli
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ng'apa ya Lindi nimeenda mwezi wa 8 minanzi ni mingi Sana pale nimefika mpaka rutamba aiseeNg'apa ipi?!!km ya Lindi sio kweli
Kumbe kijijini nilipokulia pakishua hapatajwa, Arusha..Miaka nakua kilikua poa ila tabia nchi, kwa sasa jua na mvua nadra, vumbi sana.
Vijiji kuzunguka mirerani, Makiba, Valeska,Lositeti, Mbuguni,Migungani,Shambarai...ma hommies.
Kuna sehemu inaitwa sukro, ipo mkoa wa manyara kutoka arusha unafata bara bara ya kuelekea kiteto, ukifika kijiji cha terrat unakunjia maporini huko, wacha kabisa, kuna kijiji kinaitwa narakauo, ukifika utajiuliza binadamu alifata nini huku, ila kuna mchaga amekita biashara ya maana, Ana duka la maana, yeye ndiye bank ya wamasai, yaani huduma zote muhimu wamasai wanapaita hapo, nilikutana na nyoka aina ya kifutu akiingia kwenye kanyumba flani kadogo, nika ita ili kama kuna mtu ndani nimweleze akae macho ila Hakuna aliyeitika, nilipo enda mbele kama mita 50 nikakutana na mmasai akielea uelekeo kilipo kile kibanda, nikamwuliza kama yeye ndiye anayeishi kwenye kile kibanda akasema ndiyo, nikamtaarifu kuwa nimeona joka kubwa likiingia humo kibandani hivyo awe makini, akacheka na kuniuliza "sasa nyoka ina shida gani? Nikamwambia ni kifutu mkubwa kabisa mzee, akasema tena huyo ndio hana shida kabisa! Nika achana nae ila kule hapana. Sehemu nyingine ilinishangaza ni same, gonja mahore kuna kijiji kioo kwenye kilele cha mlima, kinaitwa Mtii, ukifika chini ya mlima ili uanze kupanda kuelekea Huko kijijini kwa piki Piki ni tsh 30000 kupanda na 20 000 kusuka, picha hii hapo chiniKwa kifupi uko ni jangwa sahii
Kuna sehemu inaitwa sukro, ipo mkoa wa manyara kutoka arusha unafata bara bara ya kuelekea kiteto, ukifika kijiji cha terrat unakunjia maporini huko, wacha kabisa, kuna kijiji kinaitwa narakauo, ukifika utajiuliza binadamu alifata nini huku, ila kuna mchaga amekita biashara ya maana, Ana duka la maana, yeye ndiye bank ya wamasai, yaani huduma zote muhimu wamasai wanapaita hapo, nilikutana na nyoka aina ya kifutu akiingia kwenye kanyumba flani kadogo, nika ita ili kama kuna mtu ndani nimweleze akae macho ila Hakuna aliyeitika, nilipo enda mbele kama mita 50 nikakutana na mmasai akielea uelekeo kilipo kile kibanda, nikamwuliza kama yeye ndiye anayeishi kwenye kile kibanda akasema ndiyo, nikamtaarifu kuwa nimeona joka kubwa likiingia humo kibandani hivyo awe makini, akacheka na kuniuliza "sasa nyoka ina shida gani? Nikamwambia ni kifutu mkubwa kabisa mzee, akasema tena huyo ndio hana shida kabisa! Nika achana nae ila kule hapana. Sehemu nyingine ilinishangaza ni same, gonja mahore kuna kijiji kioo kwenye kilele cha mlima, kinaitwa Mtii, ukifika chini ya mlima ili uanze kupanda kuelekea Huko kijijini kwa piki Piki ni tsh 30000 kupanda na 20 000 kusuka, picha hii hapo chiniView attachment 2382645View attachment 2382646View attachment 2382647View attachment 2382648
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Ni kweli katavi hakuna nyumba za nyasi. Nakumbuka 2013 tukiwa na RC Rajab Rutengwe tuliongoza Operation inaitwa ONYAKA i.e Ondoa Nyasi Katavi. Ilisaidia sana.Katavi hapana vijiji vingi vinanyumba zilizobora maji Sasa hivi serikali imejitahidi Sana kwa huduma hii
Si afadhali hapo. Mimi miaka hiyo hiyo sehemu ikiwa inaitwa Musoma vijijini, wakati huo yapo mabasi yaitwa yo Ngoreme bus aka Mwanamara yakiendeshwa na akina Masyane. Wakati wa masika mwisho wa basi ilikuwa hapo Sirorisimba, tulikuwa tunakanyaga kwa miguu kuelekea huko Kenyana, Masinki na Kemugongo kwa muda ya masaa 12. Tulikuwa tuna lala njiani tunalazimika kuomba pa kulala njiani. Watu wa kule miaka hiyo walikuwa wakalimu sana. Maji ya kunywa toka mto Somoche na Nyaruherere yalikuwa machafu sana na tope hasa kiangazi mnago mbania na wanyama poli. Watu wengi walikuwa wana uwawa na nyati. Acha kabisa life la Ngoreme enzi hizo. Hakuna hospital, hakuna Sekondari hata moja shule za msingi hazikuzidi 5 na umbali kati ya shule na shule kwenye km 30 na kuendelea.Mkoa wa Mara wilaya ya Butiama
Hiyo kitu Mkuu niilikuta Galanos tulikuwa tunaita erosion, tulikuwa tunatumia kidawa flani cha chupa ya kijani,kende utatamani uzinyofoe.Kwa hiyo miaka ni agemate wangu, advance nimemaliza 2011 pia,Minaki Sec, pale ilikua joto tu na maji yenye fangasi sijui, pumbu zinawasha mpaka unataka uzitoe.hahah
Hilo jina lako limenikumbusha Miaka hiyo kulikuwa na Hiace zimeandikwa Luchelele mzunguko ebwana maeneo ya Nyamalango,Swear, Fisheries,Nsumba,Nganza,Kijiweni, Rose, mpaka Nyegezi Kona.Duuu mda umeenda lakini.
Kuna siku wanapaita wateja wengi tu, kama kukitokea msiba wa mtu wa Huko basi bodaboda ndiyo heri Kwao,Experience nzuri mkuu
Hiyo alfu thelathini wanapata wateja?
Tetemeko la Ritcher Scale ya 7 likipita pale lazima tuzike zaidi ya 10000Sawa. Ila mwanza sehemu kubwa ni milima na mapango. Ni Mungu tu anawalinda wanaMwanza walio wengi. Yale mawe ukiyaangalia yalivyokaa ndio utajua kuna nguvu kubwa inaulinnda ulimwengu na mabaya
Dar ni Jiji sio mjiDar es salaam huwa najiuliza watu wanawezaje kuishi huo mji!!
Nilipanda mboga mashambani kwenda kuchuma nusura nibakwe na nyani...Sijui zilitaka kunipiga[emoji2955] nilitimuka macho yote nilihamishia mgongoni[emoji17]