Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Mpanda Katavi....mji wa hovyo sana ule
Historia ya mji wa Mpanda ina mizizi yake tangu mwaka 1934 kufuatia ugunduzi wa dhahabu uliofanywa na Mhandisi wa madini na Mjiolojia wa Kibelgiji aliyeitwa Jean Poussin. Awali eneo hilo lilikuwa mojawapo ya Wilaya za Mkoa wa Tabora hadi ilipofika mwaka 1975 ilipohamishiwa Mkoa wa Rukwa na baadaye Katavi mwaka 2012.

Jean Poussin alipata leseni ya uchimbaji baada ya kugundua akiba kubwa ya madini ya Zinki (Zinc) na Risasi (Lead) ambayo yalikuwa na umuhimu mkubwa sana kiuchumi katika kipindi hicho, alianzisha mgodi wa kuzama chini (underground mine). Pamoja na changamoto za Vita Kuu ya pili ya Dunia, Serikali ya wakati huo ilimuunga mkono na kumpatia ushirikiano mkubwa katika biashara yake hiyo, ikizingatiwa kwamba mgodi huo ulikuwa chanzo cha malighafi za vifaa vya kijeshi.

Mgodi wa Ururirwa (Ululilwa?) Mineral Ltd uliorodheshwa kwenye Soko la Hisa la London (London Stock Exchange Market) mwaka 1947 kama njia ya kuwezesha ufadhili wa mchango wake katika ujenzi wa miradi ya bomba la maji na reli iliyohudumia mgodi na mji kwa wakati huo. Ulazima wa kusafirisha makinikia ya madini kwenda bandari ya Dar es Salaam ulilazimu ujenzi wa reli iliyounganisha Reli ya Ujiji-Tabora.

Mbali na madini, eneo hilo lilivuta watu wengi kwa ajili ya kilimo cha mazao ya mpunga, mahindi na tumbaku yanayostawi sana eneo hilo na pia ufugaji wa mifugo hususan Ng'ombe, Mbuzi na Kondoo na hata uvunaji wa mazao ya misitu zikiwemo mbao na asali.
 
Mkuu Tangeni hapo jirani na Mzumbe University? Hiyo labda itakuwa Bunduki au kule Juu kabisa ya Kijiji kinaitwa Nyandira..
Kabla ya Bunduki unapita Mlale Kisha unapanda ule Mlima mrefu kuipata Mgeta Kibaoni, Mgeta Kibaoni Kuna njia Moja inaenda Bunduki na nyingine inaenda Lolo mpaka Nyandira. Bunduki wanafunzi wa sekondari wanatoka mbali na majumbani Kuna Siku wanafunzi wanaenda robo ya Darasa.

Mgeta Kibaoni usiagize supu bila kuuliza Kuna supu ya nguruwe, Gari za Moro Town Kwenda Mgeta kulikuwa na Noah zimeandikwa Mama Mlezi na Toyota Dayna Hiace Double Diff zinaenda mpaka milimani Nyandira, seat ya karibu na dereva nauli ilikuwa inaongezeka elfu 1.
 
Bora hata mpanda, kuna mahali panaitwa MAJIMOTO aisee huko nilipoenda nilijiuliza qatu wamefuata nini, na wengi wao ni wasukuma kule...Ajabu ni kwamba they are making money ile hatari. Ni matajiri wa kutupwa kutokana na kilimo ufugaji na madini.
Majimoto iko wapi hio mkuu?
 
Kijiji Cha kenge,kata ya kiroka milima ya uluguru huko,mita 3000 kutoka chini,yaani huko unayaona mawingu tu,hakuna umeme, chakula ni ndizi tu
Watu wamekomaa vifua na mikono mpaka watoto kwa kupanda na kushusha mlima
Hatari sana nilishangaa mtu kushuka na mbao tatu begani mara kumi kwa siku bila kuchoka!
 
Sehemu nyingine ipo wilaya ya Mbalali mkoa ni Mbeya kule Blonde la Mpunga la Usangu. Kule kuna vijiji vingi Sana. Kuna Kijiji nilikaa pale Miezi nilishangaa Sana.

1. Sikuwahi kusikia Kuna kituo cha police au police . Kule bangi inavutwa kama sigara.

2. Kwa wale wala kitimoto kule inauzwa kama Dagaa.

3. Kwasababu kitimoto ni nyingi Sana na hawaoimi Kwa kilo wanaweka Kwa mafungo kama nyanya. Kitimoto ya 4,000 ukimaliza wewe ni shujaa.

4. Sikuwahi kuona limao, kitunguu , Ndizi za kuiva wala nyanya.

5. Hiyo kitimoto inapikwa Ila bila hivyo vitu hapo juu.


6. Usiku kuisikia Sauti ya wanyama wakali kama Simba na tembo ni kawaida.


7. Kuna Baridi usiku kama uko Yemen au Kwenye Vilima Vya magaidi wa Taliban kule Afghanistan.

8. Sikuwahi kuona kiwanja cha mpira hata kupiga danadana.


9. Kule mchele na wali unaweza Kula Hadi ufe hakuna Kijiji nimetembea tanzania nikakuta kina mchele kama kile.
Karbu na chimala?
 
Niliendaga Kododo na Lukunguni tarafa ya Mgeta kata ya Mgeta. Huko sio Mchezo kwa milima ile. Ni kweli inakosa jibu watu walifuata nini huko Milimani.
Yani nilistaajabu maisha yao ya kila siku wanaendeshaje
Mana hata maduka yako huko bondeni ambako masaa 2 mnashuka
 
Habari za muda huu wana JF,

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji cha Baranga kata ya Sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndio kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu, jua kali ndio kwao, vurugu Sasa ndio chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafiki na timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa na mgogoro wa mpaka wa shamba kati ya ukoo na ukoo huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu nini?
Mbinga
 
Back
Top Bottom