Ni suala la muda tu kabla CCM hawajatuletea 'Magufuli' mwingine

Ni suala la muda tu kabla CCM hawajatuletea 'Magufuli' mwingine

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
2,428
Reaction score
3,937
CCM walilazimika kumpa madaraka Magufuli kutokana na mazingira ya wakati ule ila walidhani wangeweza kumdhibiti. Magufuli akawashangaza na kuwafumba midomo hata wale ambao walidhani wangekuwa na sauti juu yake. Mmoja wa watu pekee ambaye NADHANI bado alibaki na kauwezo fulani ka kumkemea alikuwa ni Benjamin Mkapa.

Lakini kwa wengine Magufuli alikuwa too much. Si vigogo si nani, wote waliishi kwa hofu wasijue mzee anaweza akaamka na maamuzi gani juu ya maisha yao.

Sasa hivi CCM wako comfortable, Mama ameweza kuwadhibiti watu wa Magufuli. Polepole kamalizwa kisiasa kwa kupewa ubalozi na wengine kama kina Mwigulu ndiyo wanachafuliwa CV zao za kuwamaliza kabisa kisiasa.

Ila ninachoona CCM ni chama kinachotapatapa. Toka 1995 ni chama ambacho ni nusu mfu. Chochote wanachoweza kujishikizia ili waendelee tu kubaki madarakani, wanafanya hivyo. Siyo tena habari za itikadi au principles. Kwa maneno ya Kolimba, ni chama kilichopoteza dira na muelekeo.

Kesho wanaweza kumtengeneza 'Magufuli' mwingine ambaye watajiaminisha wataweza kumdhibiti tofauti ya yule wa nyuma au mazingira yatawalazimisha kumuunga mkono, na watatulazimisha tumkubali. Na kama kawaida yetu, tutakuwa tunarudia makosa ya nyuma bila kujifunza chochote kwa yaliyopita.
 
BM si kwamba alikuwa anammudu,hapana alikuwa kama mshauri wake.

hawa wengine walijichanganya pale walipotaka kujifanya ni remote,

..hapana.

..matendo ya Magufuli hayakuwa yanaendana na mtu ambaye yuko karibu na anashauriwa na Ben Mkapa.

..Magufuli angekuwa anashauriwa na Mkapa asingeharibu taswira ya nchi kimataifa na kidiplomasia kiasi kile.
 
Ni hatari sana unapokuwa na chama kinachofanya chochote kuendelea kukaa madarakani. Kwa sasa CCM wako tayari kufanya lolote ili kubaki madarakani, na sio kwamba wako kwa ridhaa ya umma, bali wanaunyamazisha umma, na sauti zinazotakiwa kutoka ni zile za propaganda kuwa CCM inakubalika sana.

Wakiona hiyo porojo yao haikai vizuri, wanasema ni kweli CCM haipaswi kuendelea kukaa madarakani, lakini ni chama gani kipewe nchi. Ukiwauliza mbona hapo Kenya vyama ni vipya kila uchaguzi, na Kenya bado wako mbele yetu kwenye uchumi, afya, elimu, siasa nk wanapotezea.
 
..hapana.

..matendo ya Magufuli hayakuwa yanaendana na mtu ambaye yuko karibu na anashauriwa na Ben Mkapa.

..Magufuli angekuwa anashauriwa na Mkala asingeharibu taswira ya nchi kimataifa na kidiplomasia kiasi kile.

Ushauri wa kuwakomoa wapinzani ni kudhibiti kundi la JK ni ushauri aliochokua 100% toka kwa Mkapa. Lakini mambo mengine alikuwa hamsikilizi kabisa. Jambo hilo lilimfanya Mkapa apate msongo wa mawazo maana wenye CCM walimsaka Mkapa kwa kuwachongea kinyago kilichomtisha hata yeye mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mkapa alijitutumua mbele ya Magufuli na kusema, serikali ya Tanzania haipaswi kuitwa ya mtu, bali iitwe serekali ya ccm au ya Tanzania. Toka wakati huo Magufuli kwa aibu sio kwa woga, akawa anajitahidi kwa shingo upande kusema serikali ya CCM, mara ya Tanzania.
 
hao wanatengeneza jpm mwingine soon utaona maana wote wanazidi kuchafuka na atakayekuja hawatoamini atakavyoruka sarakasi na kuwageuka mimi nitafrahi mno kama atawageuka na kuhudumia wananchi maana ccm tanapenda kulindana hata kwa dili fake yenyewe yanataka kila kitu kiende wanavyotaka
 
..hapana.

..matendo ya Magufuli hayakuwa yanaendana na mtu ambaye yuko karibu na anashauriwa na Ben Mkapa.

..Magufuli angekuwa anashauriwa na Mkala asingeharibu taswira ya nchi kimataifa na kidiplomasia kiasi kile.

Bado unaleta hadithi zile zile za kushtakiwa MIGA

Watu wanakunyonya kwenye mikataba ya uwekezaji alafu unaogopa kuwagusa kisa utashitakiwa na utaharibu taswira ya nchi..!??
 
Ushauri wa kuwakomoa wapinzani ni kudhibiti kundi la JK ni ushauri aliochokua 100% toka kwa Mkapa. Lakini mambo mengine alikuwa hamsikilizi kabisa. Jambo hilo lilimfanya Mkapa apate msongo wa mawazo maana wenye CCM walimsaka Mkapa kwa kuwachongea kinyago kilichomtisha hata yeye mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mkapa alijitutumua mbele ya Magufuli na kusema, serikali ya Tanzania haipaswi kuitwa ya mtu, bali iitwe serekali ya ccm au ya Tanzania. Toka wakati huo Magufuli kwa aibu sio kwa woga, akawa anajitahidi kwa shingo upande kusema serikali ya CCM, mara ya Tanzania.

..yule bwana hakufaa kwenye ile nafasi.

..kwanza afya yake haikuwa imara na hali hiyo ilimpelekea kushindwa kutekeleza majukumu yote ya nafasi aliyokabidhiwa.

..pili hakuwa ana uelewa wa dhamana ya uraisi na namna raisi wa nchi hii anavyotakiwa kuenenda.
 
Bado unaleta hadithi zile zile za kushtakiwa MIGA

Watu wanakunyonya kwenye mikataba ya uwekezaji alafu unaogopa kuwagusa kisa utashitakiwa na utaharibu taswira ya nchi..!??

..angekuwa haogopi kuwagusa acacia/barrick angetaifisha migodi yote.

..au angewabana walipe usd 191 billion badala ya kishika uchumba cha usd 300 million.

..hivi unajua hata hizo usd 300 million hatukuzipata yote?

..Unajua kuna deni tuliambiwa tunadaiwa hivyo likatolewa kwenye hiyo 300 million? Unafahamu hilo?
 
Wimbo wa kitambo umeniponyoka wa mashairi haya:CCM alianzisha nyerere sasa imezeeka/sera zaake zimeiharibu hii nchi/na ujamaa ulishindwa kabisa,tuwaondoe madarakani kabisa- iwee/
 
..yule bwana hakufaa kwenye ile nafasi.

..kwanza afya yake haikuwa imara na hali hiyo ilimpelekea kushindwa kutekeleza majukumu yote ya nafasi aliyokabidhiwa.

..pili hakuwa ana uelewa wa dhamana ya uraisi na namna raisi wa nchi hii anavyotakiwa kuenenda.

Kabisa, yule hakupaswa kufikia cheo cha urais kwa nchi yenye katiba mbovu kama hii.
 
Bado unaleta hadithi zile zile za kushtakiwa MIGA

Watu wanakunyonya kwenye mikataba ya uwekezaji alafu unaogopa kuwagusa kisa utashitakiwa na utaharibu taswira ya nchi..!??

Kwani huko MIGA ushitakiwe ni kitu gani aliwapora hao wenye hiyo migodi? Maana kama ni makinikia bado yaliondoka, na hakukuwa na ushahidi wowote wa madai yake kwao. Hao ACACIA waliondoka wenyewe maana walikuwa ni kampuni ya katikati ya Barrick, lakini Barrick hadi leo wapo na madini bado wanavuna. Sasa ukashitakiwe kwa madhara gani uliyowapa?
 
Kabisa, yule hakupaswa kufikia cheo cha urais kwa nchi yenye katiba mbovu kama hii.

..alishakurupuka akiwa waziri na kuisababisha serikali ishtakiwe.

..mara ya kwanza alivunja kituo cha mafuta Mwanza, akashindwa kesi mahakamani, serikali ikalipa 15 billion.

..mara ya pili akakamata meli ya uvuvi aka-mishandle process nzima, akashindwa kesi mahakamani.

..mara ya tatu akavunja mkataba wa ujenzi, akashindwa kesi, akagoma kulipa fidia.

..kwasababu ya kugoma kulipa ndege yetu ikakamatwa Canada. Lissu alipoibua kashfa hiyo wakaona busara ni kumuua.
 
Kwani huko MIGA ushitakiwe ni kitu gani aliwapora hao wenye hiyo migodi? Maana kama ni makinikia bado yaliondoka, na hakukuwa na ushahidi wowote wa madai yake kwao. Hao ACACIA waliondoka wenyewe maana walikuwa ni kampuni ya katikati ya Barrick, lakini Barrick hadi leo wapo na madini bado wanavuna. Sasa ukashitakiwe kwa madhara gani uliyowapa?

..acacia walikimbilia mahakamani.

..waliondoa kesi yao baada ya barrick kununua hisa za minority shareholders.

..lakini yote hiyo ilikuwa ni kucheza na akili za Watz.

..accacia alikuwa mtoto wa barrick.
 
..acacia walikimbilia mahakamani.

..waliondoa kesi yao baada ya barrick kununua hisa za minority shareholders.

..lakini yote hiyo ilikuwa ni kucheza na akili za Watz.

..accacia alikuwa mtoto wa barrick.

Kabisa, maana ACACIA alipata chake ndio akaondoka, lakini kampuni tanzu ya Barrick iko hadi leo. ndio wakalazimisha kuunda kampuni sijui Twiga sijui hata nini kinaendelea kwenye hiyo kampuni ya kina Kabudi.
 
Ushauri wako ni upi katika hili? Au ndio twende tukalitizame
 
Back
Top Bottom