Ni suala la muda tu kabla CCM hawajatuletea 'Magufuli' mwingine

Ni suala la muda tu kabla CCM hawajatuletea 'Magufuli' mwingine

Alikua na mapungufu yake mengi lkn ukweli ni kwamba alikua na nia njema kuona nchi ikisonga mbele.

Nilipenda sana jinsi alivokua akiwadhibiti wapuuzi waliojifanya hii nchi ni Mali yao na familia zao, tunahitaji rais mzalendo na asie yumbishwa na wahuni kwa kujifanya CCM ina wenyewe
Kuna msemo unasema 'the road to hell is paved with good intentions'
 
Mwigulu anachafuliwa cv.? 😳
Trust me, ccm hata ikisimamisha mbuzi, lazima mbuzi ishinde.
Sijawahi kumkubali huyo kabisa kwa ngazi yoyote ile ya uongozi. Ninachomaanisha ni kuwa Mama amewacontrol na kuwazima wale walioonekana wana political ambitions na ambao wangeweza kutumia jina la Magufuli kujineemesha kisiasa.
 
CCM walilazimika kumpa madaraka Magufuli kutokana na mazingira ya wakati ule ila walidhani wangeweza kumdhibiti. Magufuli akawashangaza na kuwafumba midomo hata wale ambao walidhani wangekuwa na sauti juu yake. Mmoja wa watu pekee ambaye NADHANI bado alibaki na kauwezo fulani ka kumkemea alikuwa ni Benjamin Mkapa.

Lakini kwa wengine Magufuli alikuwa too much. Si vigogo si nani, wote waliishi kwa hofu wasijue mzee anaweza akaamka na maamuzi gani juu ya maisha yao.

Sasa hivi CCM wako comfortable, Mama ameweza kuwadhibiti watu wa Magufuli. Polepole kamalizwa kisiasa kwa kupewa ubalozi na wengine kama kina Mwigulu ndiyo wanachafuliwa CV zao za kuwamaliza kabisa kisiasa.

Ila ninachoona CCM ni chama kinachotapatapa. Toka 1995 ni chama ambacho ni nusu mfu. Chochote wanachoweza kujishikizia ili waendelee tu kubaki madarakani, wanafanya hivyo. Siyo tena habari za itikadi au principles. Kwa maneno ya Kolimba, ni chama kilichopoteza dira na muelekeo.

Kesho wanaweza kumtengeneza 'Magufuli' mwingine ambaye watajiaminisha wataweza kumdhibiti tofauti ya yule wa nyuma au mazingira yatawalazimisha kumuunga mkono, na watatulazimisha tumkubali. Na kama kawaida yetu, tutakuwa tunarudia makosa ya nyuma bila kujifunza chochote kwa yaliyopita.
Omba waisihamu wawe marais siku zote...magufuli atakuja tu ila kamwe siyo kutoka kwa waisiharamu ......viongozi wa ovyo hapa tz ni waisiharamu
..chama cha CCM hakuna muislamu bali wamejaa waisiharamu tu ...basi kama kiongozi ajaye atakuwa mkristo jua tu huyo ndiyo anaweza kuwa magufuli
 
Ni hatari sana unapokuwa na chama kinachofanya chochote kuendelea kukaa madarakani. Kwa sasa CCM wako tayari kufanya lolote ili kubaki madarakani, na sio kwamba wako kwa ridhaa ya umma, bali wanaunyamazisha umma, na sauti zinazotakiwa kutoka ni zile za propaganda kuwa CCM inakubalika sana.

Wakiona hiyo porojo yao haikai vizuri, wanasema ni kweli CCM haipaswi kuendelea kukaa madarakani, lakini ni chama gani kipewe nchi. Ukiwauliza mbona hapo Kenya vyama ni vipya kila uchaguzi, na Kenya bado wako mbele yetu kwenye uchumi, afya, elimu, siasa nk wanapotezea.
CCM NI GENGE LA WAHALIFU...TOP CRIMINAL
 
..hapana.

..matendo ya Magufuli hayakuwa yanaendana na mtu ambaye yuko karibu na anashauriwa na Ben Mkapa.

..Magufuli angekuwa anashauriwa na Mkala asingeharibu taswira ya nchi kimataifa na kidiplomasia kiasi kile.
Hizi habari za kidiplomasia huwa mnazipata wapi kuna balozi ilifungwa shida watu design yako ni washamba wa wageni na wazungu. Ukute kwako unakula sahani za bati mgeni akija unampa sahani za udongo au kioo ushamba mzigo sana
 
CCM walilazimika kumpa madaraka Magufuli kutokana na mazingira ya wakati ule ila walidhani wangeweza kumdhibiti. Magufuli akawashangaza na kuwafumba midomo hata wale ambao walidhani wangekuwa na sauti juu yake. Mmoja wa watu pekee ambaye NADHANI bado alibaki na kauwezo fulani ka kumkemea alikuwa ni Benjamin Mkapa.

Lakini kwa wengine Magufuli alikuwa too much. Si vigogo si nani, wote waliishi kwa hofu wasijue mzee anaweza akaamka na maamuzi gani juu ya maisha yao.

Sasa hivi CCM wako comfortable, Mama ameweza kuwadhibiti watu wa Magufuli. Polepole kamalizwa kisiasa kwa kupewa ubalozi na wengine kama kina Mwigulu ndiyo wanachafuliwa CV zao za kuwamaliza kabisa kisiasa.

Ila ninachoona CCM ni chama kinachotapatapa. Toka 1995 ni chama ambacho ni nusu mfu. Chochote wanachoweza kujishikizia ili waendelee tu kubaki madarakani, wanafanya hivyo. Siyo tena habari za itikadi au principles. Kwa maneno ya Kolimba, ni chama kilichopoteza dira na muelekeo.

Kesho wanaweza kumtengeneza 'Magufuli' mwingine ambaye watajiaminisha wataweza kumdhibiti tofauti ya yule wa nyuma au mazingira yatawalazimisha kumuunga mkono, na watatulazimisha tumkubali. Na kama kawaida yetu, tutakuwa tunarudia makosa ya nyuma bila kujifunza chochote kwa yaliyopita.
Kwa hatua CCM walipoifikisha Nchi, njia ni mbili MBELENI.

1. KATIBA mpya na Tume huru ya Uchaguzi. Njia hii itaiua CCM baada tu ya kufanikiwa, bt Taifa litapona.

2. Njia ya kumleta DICTATOR mpya. Njia hii ni njema Kwa wananchi wa kawaida bt ni ngumu Kwa democrasia, maana itabidi kufunga mkanda.

Njia hii yaweza kuwa ngumu sana pia sababu kuwang'oa waovu waliopo, lazima mtikisiko na wapo wataoumia indirect.
 
Huyo JPM mpya aje hata leo.
Maana nchi hii sasa tupotupo tu hata hatuelewi hii gari inepelekwa wapi tumedandia tu.
Na dereva hajui vile vile km anaendesha wala njia.
 
Hahahahaha, mkuu ina maana wewe pekee ndiye hujui kuwa Jiwe alikuwa muuaji na muovu kuliko mtu yoyote Tanzanian?
Ilikuwa ni rahisi kumuhusisha na mauwaji na watu mkaamini hata isipojulikana hao wauliyouliwa wanahusiana vp na Magufuli au kulijulikana walifanya nini chenye kudhaniwa ndio sababu ya Magufuli kuwauwa.
 
Ilikuwa ni rahisi kumuhusisha na mauwaji na watu mkaamini hata isipojulikana hao wauliyouliwa wanahusiana vp na Magufuli au kulijulikana walifanya nini chenye kudhaniwa ndio sababu ya Magufuli kuwauwa.
Ni mbinu za zamani hizo- Kuonyesha kuwa kulikuwa na ukatili wa hali ya juu.- hata hii mada yenyewe inalenga kuendeleza kuchafua legacy yake.
 
Tumuache mh Rais wetu afanye kazi ya kuwatumikia watanzania, Tuna Iman na mh Rais na bado tunamhitaji Sana Kuendelea kututumikia sisi watanzania, habari za Nani atafuata tutakutana 2030 ndio sisi wananchi tutaanza kuwaambia viongozi wetu watuletee jina la Nani kuendeleze kazi iliyotukuka ya mh mama yetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani

Kwa Sasa nchi ipo salama katika mikono salama ya mama Samia suluhu Hassani na tuna Imani Naye ya kutupeleka mbele zaidi
 
Omba waisihamu wawe marais siku zote...magufuli atakuja tu ila kamwe siyo kutoka kwa waisiharamu ......viongozi wa ovyo hapa tz ni waisiharamu
..chama cha CCM hakuna muislamu bali wamejaa waisiharamu tu ...basi kama kiongozi ajaye atakuwa mkristo jua tu huyo ndiyo anaweza kuwa magufuli
Angekuwa Assad ndio rais angekuaje?
 
Nadhani sababu ya Magufuli kuwa Rais makini na moja ya kiongozi bora kuwepo na kukubalika Afrika utendaji wake na misimamo isiyoyumbishwa na magenge kama ni nyeupe ni nyeupe kama nyeusi ni nyeusi.
 
Back
Top Bottom