Ni Tanzania pekee kukuta watu wanasikiliza nyimbo ya lugha wasiyoijua

Ni Tanzania pekee kukuta watu wanasikiliza nyimbo ya lugha wasiyoijua

Mbongo akifanikiwa kwenda tunchi tuwili tena akakaa jimbo moja muda wote alokuwa huko akifanya tuvibarua twake basi anajikuta anajua kila kitu cha ulimwengu.

Kajifunze Mziki ninini kabla hujatafuta aibu ndogo ndogo kama hizi zinazoweza kuepukika.
Elewa tu kuwa mimi sikutaka kuukana uraia wangu. Namshukuru sana Mungu kwani nimeijua Dunia nikiwa mdogo sana bado. Hebu nenda tu Uingereza uingie restaurant yoyote uniambie utasikia nyimbo mwanzo mwisho za Kijerumani au Kifaransa au Kihindi au Kichina au Kiswahili. Ila Tanzania nenda sehemu yoyote ya Starehe utasikia mwanzo mwisho nyimbo za Kongo na Kiingereza. Ndio maana hata Brenda Fasi nyimbo zake alizoimba Kizulu zilipata umaarufu sana Tanzania kuliko nchi zingine.

Ujinga kama huu huwezi kuukuta Nigeria au hata hapo Kenya tu.

Pia nikuambie tu kuwa huu ujinga tuliuanza zamani sana wakati tv hazijaja nchini hivyo tulikuwa tunakwenda kuangalia sinema kwenye sehemu maalum kwa kulipia AMBAPO ASILIMIA 100 NI MOVIE ZA KIHINDI NA KULIKUWA HAKUNA KUTAFSIRIWA . Kiufupi Wahindi walitupata sana. Nakumbuka na miaka ya 90 ilikuwa kama vile Wakongo hapa ni kwao maani nyimbo zao zilitawala asilimia 95 kuliko nyimbo zozote zile, kwa Africa nyimbo za Kongo zilitawala zaidi Tanzania na tulizijua hata kwa kuimba japo hatukujua maana yake.
Wenzetu Kenya na Uganda walikuwa wanazipiga lakini kwa kiasi kidogo sana, labda kuwe na live show.

NADHANI SIO MUDA MREFU WACHINA WAKIJIPANGA TUTAANZA KUSIKILIZA NA KUKARIRI NYIMBO ZAO.

TUKUBALI TU SISI NI WAJINGA KATIKA MAMBO MENGI TU
 
Juzi kwenye mechi kati ya Ghana na Central Africa, huko Accra ulipigwa wimbo wa Diamond na Jux kipindi Cha mapumziko
 
Fanya kitu moyo unapenda ...binadamu ni kama vidole tunatofautiana wao ni vibe tu wanaenjoy.....ww unawahukumu vingine
Nimefanikiwa kufika nchi kadhaa na sikuwahi kuona watu wa nchi hizo wakisikiliza au kufurahia nyimbo zilizoimbwa kwa lugha za nchi zingine wasizozijua.

Lakini hapa kwetu miaka nenda rudi tangu nakua miaka ya 70 nimekuwa nikishuhudia watu wengi wakisikiliza nyimbo za Kizungu na ukiwafuatilia hata neno moja hawajui maana yake, tena nakumbuka hii ni hadi vijijini ambapo hata salamu ya kiingereza haijui, nakumbuka wengine waliweza kukariri nyimbo yote ya Bob marley au Celine Diana.

Naona kwa nyimbo za Kongo ndio usiseme yaani ndizo zinazobamba kwenye baa na kwenye maharusi. Hata hapa ninapoandika hii mada nipo baa moja kali sana lakini mwanzo mwisho ni nyimbo za Kongo.

Kwa usomi wangu mdogo ninafikiri huenda kuna hujuma tulifanyiwa na wakoloni wetu wakatupatia dawa za kulevya ndio maana wengi tupo kama wajingawajinga sana , na wengine wapo kama mateja hivi NA NDIO MAANA NCHI HII NI RAHISI SANA KWA WATAWALA
 
Umesahau wimbo "Malaika" ulisikilizwa na kuimbwa maeneo mbali mbali duniani hata wasikojua Kiswahili
Mkuu hapa hakuna ubishi wimbo huu alipiga Marehemu Miriam Makeba wa Afrika ya Kusini na baadaye Bendi toka Jamaika ya Boney M walikuja uimba tena.Sasa kwa mleta mada atusaidie au kama alikuwa hajazaliwa basi afahamu hii pia. Kuna wimbo wa marehemu Michael Jackson unaitwa Liberian Girl kuna maneno ya kiswahili alitumia nanukuu " nakupenda pia nakuta pia mpenzi wee". Hizi ni baadhi ya nyimbo chache
 
Back
Top Bottom