Ni Tanzania tena Kimataifa! Shirika la Ndege la Kimataifa la Uswisi lazindua safari zake kuja Tanzania

Ni Tanzania tena Kimataifa! Shirika la Ndege la Kimataifa la Uswisi lazindua safari zake kuja Tanzania

Hana maneno mengi kama yule bwana aliyenifanyaga niichukie ccm ila kwa mwendo huu nasema hivi "NIMEREJEA KUNDINI"[emoji847]
Ila kumbuka kabla ya yule bwana mlikua mnaenda kwenye vikao vyenu na.majaketi ama mikoba na vebegi vya kuficha sare zenu ili msipopolewe mawe na kuzomewa kitaa na masokoni. Bwana yule mumshukuru sana pamoja na mambo yake

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Hii ni moja ya sababu iliyonifanya niipende Serikali ya Awamu ya Sita! Hawana kelele sana wala propaganda ni vitendo tu na matokeo yanaonekana.


Baada ya Serikali iliyopita kudharau Sera ya Mambo ya nje jambo lililopelekea Tanzania kutofaidika na Sera Bora ya Mambo ya Nje, Sasa Mabadiliko ya Sera ya Mambo ya Nje tunaanza kuona yanaanza kuzaa matunda.

Kufuata miongozo ya kimataifa juu ya Corona na kuzingatia upya mahusiano bora na mataifa mengine kunaanza tena kuifaidisha Tanzania Kiuchumi.

Leo Shirika la Ndege la Kimataifa la Uswisi limeanzisha Safari zake kuja Tanzania! Na kwa Leo tu wameshusha watalii 270 Uwanja wa ndege wa kia

Kwa msiojua kila Mtalii anapotua tu hapa Tanzania analipia dola 100 kama gharama ya visa. Hapo hujalala hotelini ambapo TRA wanaingiza Tourist tax, Hapo hajaenda mbugani ambapo analipia pia kama dola 100 kwa kuingia tu mbugani. Fedha zote hizi zinaenda kumuhudumia Mtanzania Kwa kumpatia Maendeleo.

Kusema kweli sina budi kumpenda Mama Samia! Ndo mana thamani ya Shilingi ya Tanzania inazidi kuimarika dhidi ya dola ya Marekani. Hongera Kwa Mabadiliko ya Kisera yanayozidi kulinufaisha TaifaView attachment 1969580View attachment 1969581View attachment 1969582
Sahihiaho kidogo!: Watalii walioshuka KIA ni 160 tu waliobaki 110 waliendelea mpaka Zanzibar; hapo tu![emoji2]
 
Ila kumbuka kabla ya yule bwana mlikua mnaenda kwenye vikao vyenu na.majaketi ama mikoba na vebegi vya kuficha sare zenu ili msipopolewe mawe na kuzomewa kitaa na masokoni. Bwana yule mumshukuru sana pamoja na mambo yake

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Alifanya alipoweza kufanya. Huwezi kudharau juhudi za mtu moja kwa moja.
 
Mama anaeleweka muda mrefu, ni mzalendo na mtu sahihi kushika hatamu. Anaupiga mwingi na hana kelele, Kwa mwendo huu 2025 nchi nzima itaimba jina lake
Ngoja nitafte card na sare. Mwenye connection kwa kupata kadi aniambie hapa mbeya🤗 mm ni kijana rasmi sasa🌳🌳🌳
 
Nani kasema iyo ni ndege ya kukodisha?

Umeishia darasa la ngapi?

Shirika la ndege limezindua Safari zake kuja Tanzania na watakuwa wanakuja Tanzania mara mbili kwa wiki wewe unasema ndege ya kukodi?

Ukiitwa msukule utasema unatukanwa!
Tumia lugha yenye staha. Hilo shirika
timetable yake inaonyesha linaleta na kuchkua mizigo Dar. Abiria ni kwa kukodisha. Kama wamebadilisha basi weka ushahidi hapa.

List of Swiss International Air Lines destinations - Wikipedia
 
Mama kasema kwamba leo asubuh pia shirika la ndege la ufaransa limekuja na zaidi ya watalii 300 wametua Kia then Zanzibar..

Uchumi unafunguka mkuu.
 
Back
Top Bottom