Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki!

Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki!

Omona Wanyu

Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
51
Reaction score
6
Vijana tusiwe na ugonjwa wa fikra duni, ni jambo la kipumbavu wewe kama kijana unayejiita msomi na unae tegemewa na jamii yako, kuanza kuvibagua vyuo vingine kwamba si vyuo bali ni taasisi za kuelimishia vilaza, mfano mtu kabisa anasimama na kusema "Tanzania Chuo kikuu pekee ni UDSM", au "Tumaini nacho chuo" "SAUT ndio nini?" au "UDOM ni chuo cha kata" huo kimsingi ni mtindio wa kufikilia unaochagizwa na ujuha wa mawazo na kimsingi elimu yako haijakusaidia, ni jambo la kipuuzi kuvibeza na kuvibagua vyuo kwa reasoning isiyo na mantiki, Tungeonekana wasomi sana na wazalendo kama tungevishindanisha vyuo vyetu katika maswala ya utafiti na uvumbuzi katika tasnia mbalimbali kama Chemical Engineering, Nuclear Physics, Social Science....nk nisiwachoshe na maneno mengi kimsingi, watu makini hupima Ubora wa Mhitimu kwa kuzingatia Uwezo alio nao na si Chuo alichosomea!
 
Unachokiongea ni cha kweli mkuu. Inaonesha ulikua unasoma sana post za watu wa UDSM jinsi wanavyojinadi. Leo umeamua utiririke. Karibu jamvini mkuu.
 
Unachokiongea ni cha kweli mkuu. Inaonesha ulikua unasoma sana post za watu wa UDSM jinsi wanavyojinadi. Leo umeamua utiririke. Karibu jamvini mkuu.

Kweli kabisa ndugu! Wavivu wa kufikiri ni lazima wasaidiwe kwa kuonyeshwa njia, Mbona kama ni msoto wa kwenye ajira kazi iko pale pale "who cares" about Chuo ulichotoka, hayo ni mwazo mgando yanayotakiwa kupewa mtikiso chanya yayeyuke, watasubiri sana kwa kulewa sifa za kijinga, sitaki kuwa na mawazo kama yao hayo lakini this is the "Note" they must take, Je tangu kuanzishwa kwa UDSM miaka 50 kasoro iliyopita imefanya lipi, ukilinganisha na "impact ya Vyuo vichanga" kama SAUT na Mtandao wake,Tumaini na UDOM kwa kipindi cha chini ya miaka kumi" watafakari kabla ya kukurupuka msomi hasa hawezi kukurupuka na hoja hafifu kama zile!
 
ni kweli,ila mi naona ni ushamba 2!
Coz huko kwny ajira hata hawaangalii km ww ni udsm au sio!ni vi memo,kamlete nk.na hao sauti,tumaini,cbe wanapeta tu,mtabaki hivyo2
 
wakuuuu nilipata date udsm kuna maprof zaidi ya 45 cbe maprof hawazidi 2 sasa ni wapi wanatowa elimu bora?? Ni kipi ni chuo bora?? 2ongee ukweli halisi 2
 
wakuuuu nilipata date udsm kuna maprof zaidi ya 45 cbe maprof hawazidi 2 sasa ni wapi wanatowa elimu bora?? Ni kipi ni chuo bora?? 2ongee ukweli halisi 2

Hivi kwani siku hz kufundishwa na prof au whatever ina matter! Anachofundisha prof kiko tofauti na atakachofundisha asie prof? Then uprof Tanzania? Hao wasiojihangaisha na chochote zaidi ya matumbo yao? Hao maprof 45 wa udsm wameleta mabadiliko gani ya kujivunia ktk nyanja za kisiasa, uchumi, elimu, afya, kilimo na mawasiliano? Kufundishwa na prof au bila prof haiwezi kuundermine skils na ability za mtu. Ingekuwa huko kazini unaenda na list ya maprof walioko chuo ulichosoma ingekuwa balaa! Mimi niko Udom, sijui idadi ya maprof walioko hapa ila namjua prof osaki mtaalam wa curiculum, siwezi kusema he is a good in teaching au ameimpact maisha yangu ya kielimu kivipi cuz hakunaga jipya! Hana tofauti na akifundisha Kambuga au Ndibalema! Bakini na mentality zenu za kitoto ila sie twasonga mbele! Limtu linajidai natokea udsm halafu huko field mkikutana hayajua hata kuandika report mpaka muombe hao hao mnaosema wa vyuo vya kata! Jamani mie am proud to be at udom, the more u look down this institution is the more watu wake tunapambana kuwa gud intelectuals tunaouza ktk ulimwengu wa ajira. Bla bla za ubora, maprof, ukata, ukilaza hzo ni mbwembwe tu! Mtu wa udsm anaeweza akijiproud kuwa alisoma udsm ni aliesom miaka hyo ya 70 mpaka 90 hao wengne ni mbulula tu!
 
Wazembe wa kufikilia na wanaotumia vichwa kutunzia Macho, mdomo, masikio, pua na kufugia nywere, wata base argument zao in terms of "Character" and not "Content", wewe unadhani idadi ya Ma-prof ndio Content unayopewa hiyo ni credibility tu kwamba nimefundishwa na Prof, lakini hiyo haimanishi Content uliyo nayo. tusiwe na akili kama za mbuni jamani turuhusu vichwa vyetu vifikiri kama Intellectuals, sipingi UDSM ni Home of Intellectuals na ndio mtazamo wangu kwa vyuo vingine vyote UDOM, SAUT, CBE, DIT,TUMAINI, ARUSHA, MOUNT MERU THEOPHILO KISANJI nk vyote ni home of Intellectuals! nenda maofisi kijana ukaone watoto wadogo wa kike na wa kiume wanavopiga kazi kwa umahili wa hali ya juu, Kutoka SAUT, UDOM, MZUMBE n.k vijana wangu wote hapa ofisini ni vijana kutoka katika vyuo hivi, nimegundua tatizo la vijana wanaokuja kutafuta kazi wanatanguliza vyuo vyao mbele na ndio mgogoro unao wakabili wengi wao kutoka UDSM, mfano SAUT inaheshimika nchini kwa MASS COMMUNICATION, kuna vijana wengine baada ya kulewa hiyo sifa wanatanguliza Cho chao mbele kuna vyuo kadhaa vinatanguliza hadhi ya heshima ya kozi flani katika vyuo walivosoma huku ofisini kwenye Panel ya Interview Unasimama peke yako tuna shake Competency na Content uliyo nayo, story za Chuo ulichotoka ni michapo ya baadae baada ya ajira tukiwa pale ofisini.
 
Wazembe wa kufikilia na wanaotumia vichwa kutunzia Macho, mdomo, masikio, pua na kufugia nywere, wata base argument zao in terms of "Character" and not "Content", wewe unadhani idadi ya Ma-prof ndio Content unayopewa hiyo ni credibility tu kwamba nimefundishwa na Prof, lakini hiyo haimanishi Content uliyo nayo. tusiwe na akili kama za mbuni jamani turuhusu vichwa vyetu vifikiri kama Intellectuals, sipingi UDSM ni Home of Intellectuals na ndio mtazamo wangu kwa vyuo vingine vyote UDOM, SAUT, CBE, DIT,TUMAINI, ARUSHA, MOUNT MERU THEOPHILO KISANJI nk vyote ni home of Intellectuals! nenda maofisi kijana ukaone watoto wadogo wa kike na wa kiume wanavopiga kazi kwa umahili wa hali ya juu, Kutoka SAUT, UDOM, MZUMBE n.k vijana wangu wote hapa ofisini ni vijana kutoka katika vyuo hivi, nimegundua tatizo la vijana wanaokuja kutafuta kazi wanatanguliza vyuo vyao mbele na ndio mgogoro unao wakabili wengi wao kutoka UDSM, mfano SAUT inaheshimika nchini kwa MASS COMMUNICATION, kuna vijana wengine baada ya kulewa hiyo sifa wanatanguliza Cho chao mbele kuna vyuo kadhaa vinatanguliza hadhi ya heshima ya kozi flani katika vyuo walivosoma huku ofisini kwenye Panel ya Interview Unasimama peke yako tuna shake Competency na Content uliyo nayo, story za Chuo ulichotoka ni michapo ya baadae baada ya ajira tukiwa pale ofisini.

 
mnaangaika sana nyie vijana,hivi ni kweli bachelor holder akufundishe ww undgrduat alafu useme sawa? kitaaluma ipo hyo?
 
sasa kama sstem haiwataki maprof wafanyeje wao?na katu kama haukuwahi kufundishwa na prof wala hautaelielewa hili
 
Kiukweli wadogo zangu wote kutoka udsm au udom,mna matatizo makubwa pasipo kujua,ubishani wenu tu,tayari unaonesha jinsi gani nyinyi nyote mlivyo na akili za kisekondari,elimu tanzania tulisoma zamani siyo siku hizi.Mimi nimeshawahi kushiriki katika recruitment panel fulani,kwa kweli nathubutu kusema asilimia kubwa ya wanafunzi wa vyuo hivyo hawana uwezo kabisa.Sasa je mwanafunzi mbovu ni matokeo ya kufundishwa na mhadhiri mbovu,hata kama ni profesa au dokta? Someni kwa kuelewa mambo ndugu zangu,hivyo vyuo ni majina tu,mkija katika soko la ajira mtachinjwa tu.Take care wanafunzi
 
Kiukweli wadogo zangu wote kutoka udsm au udom,mna matatizo makubwa pasipo kujua,ubishani wenu tu,tayari unaonesha jinsi gani nyinyi nyote mlivyo na akili za kisekondari,elimu tanzania tulisoma zamani siyo siku hizi.Mimi nimeshawahi kushiriki katika recruitment panel fulani,kwa kweli nathubutu kusema asilimia kubwa ya wanafunzi wa vyuo hivyo hawana uwezo kabisa.Sasa je mwanafunzi mbovu ni matokeo ya kufundishwa na mhadhiri mbovu,hata kama ni profesa au dokta? Someni kwa kuelewa mambo ndugu zangu,hivyo vyuo ni majina tu,mkija katika soko la ajira mtachinjwa tu.Take care wanafunzi

Kweli kabisa ndugu Mwalimu Mwakitobile well said reasoning wafunde vijana!
 
ukweli vyuo vyetu vinazidiana,kama hatukubaliani hilo twende kwenye web upande wa Afrika,wahitimu kuwa vilaza hakuondoi
 
mchango wa chuo pia katika nchi na dunia ni sifa nyingine ya kukifanya chuo kiwe bora,tusiangalie mitihani tu na ajira.
 
Fanya research ya kujua wa UDSM ni wangapi ofisini,credibility yao,na wa vyuo vingine kama UDOM,SAUT MZUMBE,CBE,IFM,TUMAINI,DIT n.k ndo utapata jibu kuwa chuo si kigezo cha wewe kutoka hapo ulipo na kukupaisha kimaisha baba.
 
hivi kwani siku hz kufundishwa na prof au whatever ina matter! Anachofundisha prof kiko tofauti na atakachofundisha asie prof? Then uprof tanzania? Hao wasiojihangaisha na chochote zaidi ya matumbo yao? Hao maprof 45 wa udsm wameleta mabadiliko gani ya kujivunia ktk nyanja za kisiasa, uchumi, elimu, afya, kilimo na mawasiliano? Kufundishwa na prof au bila prof haiwezi kuundermine skils na ability za mtu. Ingekuwa huko kazini unaenda na list ya maprof walioko chuo ulichosoma ingekuwa balaa! Mimi niko udom, sijui idadi ya maprof walioko hapa ila namjua prof osaki mtaalam wa curiculum, siwezi kusema he is a good in teaching au ameimpact maisha yangu ya kielimu kivipi cuz hakunaga jipya! Hana tofauti na akifundisha kambuga au ndibalema! Bakini na mentality zenu za kitoto ila sie twasonga mbele! Limtu linajidai natokea udsm halafu huko field mkikutana hayajua hata kuandika report mpaka muombe hao hao mnaosema wa vyuo vya kata! Jamani mie am proud to be at udom, the more u look down this institution is the more watu wake tunapambana kuwa gud intelectuals tunaouza ktk ulimwengu wa ajira. Bla bla za ubora, maprof, ukata, ukilaza hzo ni mbwembwe tu! Mtu wa udsm anaeweza akijiproud kuwa alisoma udsm ni aliesom miaka hyo ya 70 mpaka 90 hao wengne ni mbulula tu!

mbona kama nakufahamu hiviiiiii
 
The Ranking of top Universities in Africa or Worldwide basically relies on a number of multiple specific criteria, the fact which makes the University of Dar es salaam to rank on top of the other, this involves mainly on Resources (Human Resources with Infrastructures included) and Research, So mambo yote hayo mawili ni dhahiri kwa Chuo chenye Umri wa nusu Karne sasa, ingawaje hata umri huo haulingani na maendeleo ambayo tungetegemea kuyaona UDSM kwa kuzingatia, majo ya matatizo ya Nchi yetu yametokana na ukiritimba wa UDSM kushindwa kuwaandaa na kutoa wasomi wa shahada za Uzamili na Uzamivu kwa kususasua mno na kwa kipindi kirefu tumekuwa mbumbumbu wa kutokumbatia mabadiliko, Idadi ya vyuo vinavoongezeka vinatupa hata uthubutu sasa wa kujiunga na EAC, lakini kwa kipindi sasa tumechelea kwa vile UDSM ilikuwa imehodhi elimu ya juu! na hali hii inasababishwa na watu mbumbu kama nyie mlio kariri kwamba chuo pekee ni UDSM, chukulia mfano mdogo by mwaka 2004, TANZANIA ilikuwa na Mawakili wasiozidi 700, UGANDA zaidi ya 12000, na Kenya mawakili zaidi ya 26000, Unafikili tatizo ni nani hapo kama sio UDSM huo ni mfano mdogo katika fani ya sheria halafu mtu anategemea kushindana na Kenya na Uganda kwenye soko la ajira!
 
mambo kama haya ndio huwa yananifanya nichoke kabisa! kijana wa tanzania wa sasa unashindanisha jina la chuo ulichotoka! ndio maana vijana wenzetu wa afrika mashariki hasa kenya, Uganda na sasa Rwanda wanatuacha na kutuzidi mbali sana inapokuja kwenye suala la ajira na kujiajiri! wenzetu hushindanisha skills na sio chuo alichotoka! eti UDSM ina watu wengi walioleta maendeleo katika nchi hii kulinganisha na SAUT au UDOM! oooops hii ni sawa na kulinganisha uwepo wa ndevu kwenye kidevu cha baba na kijana wake wa kiume wa miaka 16! ni wazi kuwa baba kutokana na umri wake atakuwa na ndevu na kijana atakuwa hana! sasa kigezo kizuri ni kulinganisha uwezo wao wa kuhukumu na ku reason! baba pamoja na umri anaweza asiwe na busara kulinganisha na mtoto! Uwezo na ubora wa chuo ni matokeo pia ya wanafunzi binafsi! so vijana jitahidini ili mshindane na wenzenu wa Kenya, Uganda na Rwanda!
 
Chuo kikuu cha kikatoliki cha St Augustine University na mtandao wake Tanzania ndio Chuo chenye idadi kubwa ya watu kuliko vyote Tanzania kwa sasa kikiwa na jamii ya watu katika meneo tofauti wanaokadiliwa kufikia 36,000, hiki ni chuo cha mfano wa kuigwa kwa maana kwa kipindi cha miaka 14 kimeziba ombwe la wataalamu wa kada mbalimbali katika ajira za ualimu wa ngazi ya Shahada mwaka jana asilimia 36% ya waajiliwa wote katika ngazi hiyo walikuwa kutoka St Augustine University, na mwaka huu wa masomo 2011-2012 walimu 1236 yani BA Education SAUT MAIN CAMPUS watahitimu na shahada zao, na katika fani ya sheria Wanasheria 252 (ukitoa SAUT Ruaha cha Iringa) watapewa shahada zao tarehe 24 ya mwezi huu, huu ndio mfano na ushindani tunao utaka. TUSHINDANE KWA KUTOA WATAALAMU NA WATAFITI ILI TULETE MAENDELEO YA NCHI YETU SIO UKIRITIMBA WA MAWAZO.
 
Back
Top Bottom