Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki!

Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki!

Vijana tusiwe na ugonjwa wa fikra duni, ni jambo la kipumbavu wewe kama kijana unayejiita msomi na unae tegemewa na jamii yako, kuanza kuvibagua vyuo vingine kwamba si vyuo bali ni taasisi za kuelimishia vilaza, mfano mtu kabisa anasimama na kusema "Tanzania Chuo kikuu pekee ni UDSM", au "Tumaini nacho chuo" "SAUT ndio nini?" au "UDOM ni chuo cha kata" huo kimsingi ni mtindio wa kufikilia unaochagizwa na ujuha wa mawazo na kimsingi elimu yako haijakusaidia, ni jambo la kipuuzi kuvibeza na kuvibagua vyuo kwa reasoning isiyo na mantiki, Tungeonekana wasomi sana na wazalendo kama tungevishindanisha vyuo vyetu katika maswala ya utafiti na uvumbuzi katika tasnia mbalimbali kama Chemical Engineering, Nuclear Physics, Social Science....nk nisiwachoshe na maneno mengi kimsingi, watu makini hupima Ubora wa Mhitimu kwa kuzingatia Uwezo alio nao na si Chuo alichosomea!

Wenye kubeza vyuo au elimu yoyote ile mimi huwaita Wabaguzi wa Ujinga.
 
Humu ndani tunajadili ajira za wasomi ama ubora wa vyuo,mbona mnayachanganya?kwani kukosa ajira nalo ni tatzo la chuo?
 
Mwigulu Chemba kapiga kitabu UDSM na ana busara kweli! Mz*nz sorry mchumi 1st class.
 
Yani Kimsingi swala la ajira ni kitu kingine issue hapa ni the assertion kwamba
"Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki" mimi nawaona wajinga sana wenye tabia hii wanaohitaji kuelimishwa Nyerere aliwahi kusema "Elimu tunayoipata ni lazima itukomboe" sasa ni lazima tutumie tasisi zetu hizi za Elimu ya juu kusukuma maendeleo na mabadiliko katika nyanja za kiuchumi, kisisasa na kijamii, ni lazima tutumie tasisi zetu hizi kwa ajili ya utafiti na uvumbuzi, na vyo vyetu ndio iwe chachu hasa ya kutafuta suruhu ya tatizo la ajira, Mazuzu ni wale wanao turudisha nyuma, kwa kuhodhi mianya ya ufaulu wa watu kwa makusudi na kupunguza na kubana nafasi za vijana na fursa za wanaotaka kujiunga na elimu ya juu hii ni kansa iliyo kuwepo kwa kipindi cha takribani miaka 30 pale UDSM kuanzia miaka ya 1980-2010 hivi , hivi sasa wamebadilika kwa sababu damu changa ya vijana tuko pale, wakiritimba wako on their way na "natural death" na ni lazima tuchagize maendeleo haya kwa kuvipa motisha vyuo vyetu vipya vya binafsi na umma, wewe kusoma UDSM sio sababu ya kumuita mwenzio KILAZA, huyo kilaza ndiye utakae muomba ajira yako au ya mwanao siku za usoni, au bosi wako na atakupima kwa "Content" na "character" yako, na sio origin ya Chuo ulichotoka,
 
mnaangaika sana nyie vijana,hivi ni kweli bachelor holder akufundishe ww undgrduat alafu useme sawa? kitaaluma ipo hyo?
kwani unaifahamu maana ya kufundishwa?
ukiifahamu yoyote anaweza kukufundisha la msingi anakufundisha nini?
 
Yani Kimsingi swala la ajira ni kitu kingine issue hapa ni the assertion kwamba
"Ni uduni na ufinyu wa mawazo kuvibeza vyuo vikuu vingine kwa misingi ya ubora usio wa kimantiki" mimi nawaona wajinga sana wenye tabia hii wanaohitaji kuelimishwa Nyerere aliwahi kusema "Elimu tunayoipata ni lazima itukomboe" sasa ni lazima tutumie tasisi zetu hizi za Elimu ya juu kusukuma maendeleo na mabadiliko katika nyanja za kiuchumi, kisisasa na kijamii, ni lazima tutumie tasisi zetu hizi kwa ajili ya utafiti na uvumbuzi, na vyo vyetu ndio iwe chachu hasa ya kutafuta suruhu ya tatizo la ajira, Mazuzu ni wale wanao turudisha nyuma, kwa kuhodhi mianya ya ufaulu wa watu kwa makusudi na kupunguza na kubana nafasi za vijana na fursa za wanaotaka kujiunga na elimu ya juu hii ni kansa iliyo kuwepo kwa kipindi cha takribani miaka 30 pale UDSM kuanzia miaka ya 1980-2010 hivi , hivi sasa wamebadilika kwa sababu damu changa ya vijana tuko pale, wakiritimba wako on their way na "natural death" na ni lazima tuchagize maendeleo haya kwa kuvipa motisha vyuo vyetu vipya vya binafsi na umma, wewe kusoma UDSM sio sababu ya kumuita mwenzio KILAZA, huyo kilaza ndiye utakae muomba ajira yako au ya mwanao siku za usoni, au bosi wako na atakupima kwa "Content" na "character" yako, na sio origin ya Chuo ulichotoka,

na sasa tunaishukuru TCU kuwachangachanganya hao fresher maana zamani ilikuwa mpaka ufaulu sana ndipo utauona ufalme wa udsm lakini sasa waweza kufaulu sana na ukapelekwa kwenye ufalme wa theofili kisanji na kinyume chake, maana kwa tcu vyuo vyote vinastahili kupata wanachuo la msingi masomo uliyoyahitaji yanapatikana huko!
 
Vijana tusiwe na ugonjwa wa fikra duni, ni jambo la kipumbavu wewe kama kijana unayejiita msomi na unae tegemewa na jamii yako, kuanza kuvibagua vyuo vingine kwamba si vyuo bali ni taasisi za kuelimishia vilaza, mfano mtu kabisa anasimama na kusema "Tanzania Chuo kikuu pekee ni UDSM", au "Tumaini nacho chuo" "SAUT ndio nini?" au "UDOM ni chuo cha kata" huo kimsingi ni mtindio wa kufikilia unaochagizwa na ujuha wa mawazo na kimsingi elimu yako haijakusaidia, ni jambo la kipuuzi kuvibeza na kuvibagua vyuo kwa reasoning isiyo na mantiki, Tungeonekana wasomi sana na wazalendo kama tungevishindanisha vyuo vyetu katika maswala ya utafiti na uvumbuzi katika tasnia mbalimbali kama Chemical Engineering, Nuclear Physics, Social Science....nk nisiwachoshe na maneno mengi kimsingi, watu makini hupima Ubora wa Mhitimu kwa kuzingatia Uwezo alio nao na si Chuo alichosomea!

Mimi nafikili kasumba hii ilikuwa inaenezwa na baadhi ya wahadhili falani pale UDSM, nimegunduwa baadhi ya wahitimu wa UDSM wana kasumba hiyo hiyo - walikuwa wanajaribu kuwa aribia sifa wanafunzi walio soma Ulaya ya Mashariki na Uchina, hivi kweli TANZANIA unaweza kujilinganisha na Urusi au Uchina katika nyanja zote - ziwe tekinolojia nk; majivuno tu.

Kuna wakati UDSM ilikuwa haitaki kabisa vyuo vikuu vingine vianzishwe TANZANIA - hapo zamani DIT ilipata wakati mgumu kukubaliwa kutunuku shahada ya Degree ya kwanza, wanapigana vita wenyewe kwa wenyewe wakati nchi ni moja! Jaribu kumchukua muhitimu wa shahada ya kwanza ya uhandisi kutoka DIT linganisha na wa UDSM tofauti zao ni kama mbingu na dunia - siwasemi vibaya ninacho taka kueleza hapa ni kwamba kasumba haifahi katika TAIFA letu. Wasipo hacha kusumba hiyo vyuo kama KIU cha pale Gongo la mboto kitawapiku siku si nyingi, wenzetu hawa wako makini na wanakwenda na WAKATI, wakati sisi tunazama kwenye makongamano na kupigana vita visivyo na MSHIKO.
 
:smiling: Wachangiaji mumenifurahisha sana na michango yenu siwaoni kabisa wale WAKIRITIMBA WA MAWAZO!:bowl::bowl:
 
kuna lecture ana master holder na anadeliver vizuri kuliko phd/prof darasani.


trust no one,love no one
 
kweli kabisa mdau tena dharau hii imejengeka hadi law xul kitu kinachowafanya vijana toka vyuo vingine wawakimbize sana hao wanaojiona mabingwa
 
Vyuo vyote Tanzania vinasimamiwa na TCU.Hivyo ubora na mitaala ya kufundishia unathibitiwa na TCU.Hivyo wahitimu wanapimwa na nini wanaleta kwenye jamii katika kubuni na kuleta maendeleo.Tusilewe sifa za chuo kikuu fulani lakini tufurahie mabadiliko makubwa ya ongezeko la vyuo hivyo ambalo limeleta ushindani ambapo umahiri wa wahitimu wake ndio kigezo sahihi la kuwapiga mtaani kwa mchango wao kuondoa umasikini na kufanya Tanzania kuwa mahali bora zaidi pa kuishi. Hivyo nawaasa vijana wa kileo kujivunia ushindani huo ambapo ukilala umekwisha kwani mwenzako atachukua nafasi yako.Kuwa mbunifu zaidi kwa elimu uliopata bila kujali umesoma chuo gani kikuu.
 
Kweli kabisa ndugu! Wavivu wa kufikiri ni lazima wasaidiwe kwa kuonyeshwa njia, Mbona kama ni msoto wa kwenye ajira kazi iko pale pale "who cares" about Chuo ulichotoka, hayo ni mwazo mgando yanayotakiwa kupewa mtikiso chanya yayeyuke, watasubiri sana kwa kulewa sifa za kijinga, sitaki kuwa na mawazo kama yao hayo lakini this is the "Note" they must take, Je tangu kuanzishwa kwa UDSM miaka 50 kasoro iliyopita imefanya lipi, ukilinganisha na "impact ya Vyuo vichanga" kama SAUT na Mtandao wake,Tumaini na UDOM kwa kipindi cha chini ya miaka kumi" watafakari kabla ya kukurupuka msomi hasa hawezi kukurupuka na hoja hafifu kama zile!

Tena wengine tulosoma kwenye taasisi ndo tunawakimbiza balaaa wao wanabaki na sifa zao
 
UDSM:home of intellectuals...hutaki kalale.
hata mimi nakubali kwani vyuoni kote ndo wapo mintalectuals.
Je wewe ni interlectual? interlectual anakosoa na ana suggest way foward..sasa wewe zaidi ya kulewa sifa huna msaada.
ni aibu sana kwa wewe kujiita interlectual wa udsm alafu reasoning capacity yako ni kama vidudu.....UDSM ya baba yako?
its public institution amabapo kila mtu anaweza kujiunga na kusoma.
Mgando wa akili ni m,baya sana....kwa akili yako ulitaka nchi hii iendelee kua na chuo kimoja milele...kweli unawaza maendeleo kweli wewe interlectual wa udsm? futa ujinga kwani usipokuisha ukaja nao huku mtaani baada ya kuhitimu hapo mlimani...utasota as jobless mpaka utakataa hukusoma udsm....ua persona competence justify ua destiny usifikiri jina la chuo litakusaida.......vijana wa udom,mzumbe,sua,muccobs,tumaini,ifm etc nawashauri muendelee kusoma kwa bidii na kwa uelewa mkubwa waacheni hawa waendelee kubwata na jina la chuo mkikutana kwa interview ndo watajua ukweli wa mambo kua uwezo binafsi ndo kila kitu na jina la chuo it does not matter.
 
DIT Inaikimbiza UDSM KWA ENGINEERING!FACT...UKIBISHA NENDA FIELD UONE UDSM WANAVOFULIA.
 
Ndugu upo correct kabisa DIT, MUST former MIST Vipo juu kuliko CoET, mi nimemaliza Mist mwaka huu civil Eng. tulikuwa field Estim construction ltd ni kampuni kubwa mjini, tulipewa kaz na supervisor engineer flan Wa Asia, washkaji walichukua 4 weeks na walivurunda, cc wa Mist only 3 days tulishamaliza. Engineer akashangaa sana akasema Mist wanafundisha sana eeh? Ndo hvyo wana coet wanaona wapo juu ila practical, theory all are poor.
 
SAWA CoET WANACHUKUA VICHWA ILAAA PRACTICAL SIO WAZURI SANA KAMA DiT ,ILA USIFANANISHE MIST NA COeT HIVYO VITU HAVIFANANI KABISAAAAAA
 
Ndo ujue jinsi gani walivyo empt headed coz wanaongea vitu ambavyo havina mantiki eti kila kitu Udsm utadhan wana content kumbe limebaki jina tu ndani uozo mtupu kazi kutapatapa kama nyinyi*mu
 
Back
Top Bottom